Yametimia, ndege ya ATCL, Dash8-Q400 angani

Yametimia, ndege ya ATCL, Dash8-Q400 angani

Ndege zenyewe watakuwa wanapanda wao wenyewe tu, sisi walalahoi tutaendelea na malori yetu

Usiwe na roho ya kukata tamaa kiasi hicho ipo siku utapata uwezo,ukishindwa wewe basi mtoto wako,wakishindwa si haba hata mjukuu waka atapanda.
 
Mkuu barafu, binafsi nikupongeze sana kwa clarifications unazozitoa juu ya aviation industry. Pia naona ni jambo jema kwa serikali ya awamu ya 5 kujaribu kuifufua ATCL, hopefully shirika lita-excel.

Mimi nina mambo ambayo huwa sipati majibu:

Je, ATCL imewahi ku-lebel ndege zetu with 'KILIMANJARO' ? If NO, kwanini neno KILIMANJARO haliwekwi kwenye ndege zetu iwe kama njia mojawapo ya kujitangaza kiutalii?

Why tunashindwa kuutangaza Mlima wetu kwa kila namna iwezekanayo? Tuna matatizo gani sisi watanzania?

Natamani sana hapo nyuma karibu na picha ya Twiga, paandikwe neno 'KILIMANJARO'.

-Kaveli-
Mkuu Kaveli raha ya JF ni kujadiliana,haimaniishi mi najuwa sana kuhusu Aviation Industry ila na-share tu na wadau.

Kiukweli miaka ya nyuma tulikuwa na ndege zenye majina tofautitofauti sana,Kulikuwa na Boeing737 yetu iliitwa Kilimanjaro,kulikuwa na Serengeti,Ngorongoro,Tarangire nk.Hizi ndege zilipaa kote duniani na kuitangaza nchi yetu.

Yalikuja "manyang'au" fulani yakitajirisha na kuliibia shirika mpaka sisi wengine tukaikimbia nchi na kutoa michango yetu ktk nchi jirani.Tulikuwa na Boeing ya kwenda Addis Ababa kupitia Entebe mara mbili kwa week.Tulikuwa na moja ya kwenda London-Heathrow!!Mpaka kuna wakati tulikuwa tunaenda hadi Ulaya Mashariki.Hii anga dunia ilitambua Call Sign yetu kama "Tango Charlie".

Wahuni fulani wakalila shirika,tunaojuwa tunaona juhudi za kurirudisha,hatukumpigia kura JPM...ila kwa hili tunampa pomgezi....Tunaiona heshima ya "Tango Charlie" katika anga ya dunia ikirudi.

Kwa swali zuri uliloniuliza,nakuzawadia picha ya BOEING737 iliyopewa jina la "KILIMANJARO" tazama katika picha(Kutoka maktaba ya kumbukumbu zangu) mali yetu sisi Watanzania miaka hiyo sisi tukiwa Vijana.Iwe kumbukumbu kwako na wengine,kuwa Taifa hili la Tanzania liliwahi kuwa ni Taifa la watu wenye akili sana na mawazo mapana...Lakini walikatishwa tamaa na wanasiasa,kama watapewa nafasi basi nchi hii itakuwa kimbilio la masikini wooooote wa Afrika na Dunia

Nakupa picha hii kukupa uthibitisho kuwa "SIBAHATISHI" ktk maelezo yangu(NA KULA SIKUMPA MAGUFULI NA CCM KUANZIA NGAZI YA UDIWANI HADI URAIS)

Cc eddy MOTOCHINI UncleBen Belo Adharusi Papa Mopao
image.jpeg
 
Licha ya kununua hizi ndege still ATCL inapaswa kupewa support kubwa sana kutoka kwa serikali na wanapaswa kuweka staff wapya kabisa
 
Heko.
Ndiyo leo nimemsikia Waziri wa Uchukuzi akitetea ununuzi wa hizo ndege kwa kusema ni nzuri kwa mazingira ya Tanzania: zitatua katika viwanja vya changarawe (akatoa mfano kiwanja cha Musoma), viwanja vyenye runway fupi n.k.
Sasa nimejiuliza, hivi kwa soko na wateja gani hao wa kufanya shirika la ndege lipeleke ndege kila mahala Tanzania? Kwanini serikali isingenunua ndege za kuweza kushindana na FastJet (Airbus au Boeing) na kuanza na sehemu zenye soko na wateja wa ndege? Sasa kupeleka ndege Musoma (kama mfano) kuna ulazima gani?

Nadhani serekali imejitahidi walau kwa kuanza kununua ndege hilo tu limenifurahisha.Pili bei ya Airbus & Boeing ni kubwa ukilinganisha na Dash8-400.Tatu muda wa kutengeneza Dash8-400 ni mfupi ukilingansha na Airbus & Boeing kama tungeamua kununua Boeing au Airbus labda tungeletewa mwaka 2018 au 2020.Nne gharama za uendeshaji Dash8-400 ni ndogo ukilinganisha na Boeing & Airbus mwisho Dash8-400 ina uwezo wa kutua katika viwanja vingi Tanzania ukilinganisha na Boeing au Airbus.

Ni vyema tukawa na utaratibu wa kupongeza pae serekali inapofanya vizuri.Katika suala la kuifufua ATCL naipongeza serekali kwa kutuondolea aibu ya muda mrefu.Nina amani huu ni mwanzo mzuri ipo siku tutanunua ndege kubwa na bora zaidi iwapo suala la nidhamu ya matumizi bora ya mapato na matumizi ya serekali yatazingatiwa.

Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika.
 
Inapendeza sana kama mtu anajadili mada kama hizi,awe na ABC ya usafiri wa anga na changamoto zake.
Fastjet tunaenda kukimbiza sana sana.Kwa sbb yeye anatumia ndege aina ya A319 inayobeba abiria 156.
Sisi tunaenda kuwa na Dash8-400 abiria 78.Safari ya Mwanza to Dsm,ATCL inatumia saa 1.20 hadi 25 wakati Fastjet anatumia saa 1.10 hadi 15.ATCL anatumia tani 1.2 kwa safari hiyo,wakati fastjet anatumia tani 3.1 za mafuta JET A1 kwenda Mwanza.

ATCL anatuwa viwanja vyote Tz vyenye lami na vile vya vumbi,wakati Fastjet anatuwa viwanja vitano tu Tz kwa maana ya Mwanza,KIA,Dsm,Znz na Mbeya.Huku ATCL akituwa Kigoma,Tbr,Mbeya,Lindi,Mtwara,Arusha,Iringa,Songea,Musoma,Dodoma,Mpanda nk

Ili fastjet atuwe na kuruka,Runway ya kiwanja inatakiwa iwe km 2.3 wakati ATCL anatuwa kwenye kiwanja chenye 1.2 km,ambavyo ndo viwanja vingi vilivyopo Tanzania.

Kwa kulitambua hili,Fastjet ameamua kuanza kuuza ndege zake zooote,ili anunue walau E190 aendane na ushindani wa soko.Kuepuka ghalama za mafuta na vipuri.

Sasa hapo ni nani anamtishia mwenzake?Muwe mnafanya utafiti kabla ya kutoa mchango
Ahsante barafu kwa kuendelea kutoa ufafanuzi ila Kuna watu akili zao zinashida kidogo kuelewa kwao, mpaka aseme Tundu Lisu au Mbowe
 
Zingenunuliwa hizo CT ungeanza kukosoa vile vile. Watu wamejitahidi kujenga madawati tayari wengine wameanza kukosoa, eti oh kwa nini tusingeanza kwa kuboresha vyoo n.k.
Kuwa rais kwenye nchi kama Tanzania ni shughuli pevu kila mtu mjuaji,mtu hajawahi hata kuigusa ndege lakini anatoa ushauri juu ya ndege,wacha tu JPM atukimbize maana akiyafuata maneno ya watanzania hatafanya lolote.
 
Nadhani serekali imejitahidi walau kwa kuanza kununua ndege hilo tu limenifurahisha.Pili bei ya Airbus & Boeing ni kubwa ukilinganisha na Dash8-400.Tatu muda wa kutengeneza Dash8-400 ni mfupi ukilingansha na Airbus & Boeing kama tungeamua kununua Boeing au Airbus labda tungeletewa mwaka 2018 au 2020.Nne gharama za uendeshaji Dash8-400 ni ndogo ukilinganisha na Boeing & Airbus mwisho Dash8-400 ina uwezo wa kutua katika viwanja vingi Tanzania ukilinganisha na Boeing au Airbus.

Ni vyema tukawa na utaratibu wa kupongeza pae serekali inapofanya vizuri.Katika suala la kuifufua ATCL naipongeza serekali kwa kutuondolea aibu ya muda mrefu.Nina amani huu ni mwanzo mzuri ipo siku tutanunua ndege kubwa na bora zaidi iwapo suala la nidhamu ya matumizi bora ya mapato na matumizi ya serekali yatazingatiwa.

Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika.
Aksante sana mkuu, Taifa linahitaji watu kama wewe....Binafsi napenda mtu ambaye anasema ukweli bila kuegemea upande wowote wa kisiasa, kweli ukweli tuuseme bila hofu.
 
Ahsante barafu kwa kuendelea kutoa ufafanuzi ila Kuna watu akili zao zinashida kidogo kuelewa kwao, mpaka aseme Tundu Lisu au Mbowe
Jamaa we we akili uliyonayo inakuyosha kuvukia Barabara tu! Msome tena Barafu alichoandika kuhusu haya maNYANG'AU yaliyoua ATC
 
Jamaa we we akili uliyonayo inakuyosha kuvukia Barabara tu! Msome tena Barafu alichoandika kuhusu haya maNYANG'AU yaliyoua ATC

Mkuu dolevaby Tanzania inahitaji taasisi imara,tukianza na mahakama,taasisi za kupambana na rushwa,Polisi,mkurugenzi wa mashtaka......Hapo tutakuwa tumepiga hatua lakini tukitegemea mtu badala ya taasisi naona ni jambo la hatari sana.

Fikiria Mwl Nyerere aliweza kununua Boieng enzi hizo hakuwa na dhahabu wala gesi,wamekuja viongozi wa ajabu ajabu wakaliuza shirika letu kwa makaburu walinyongelea mbali,wakauza nyumba za sererekali leo majaji,makamishna... wanaishi mahotelini.Kama tungekuwa na taasisi imara naamini mizengwe mingi ingezuiliwa au kupungua.
 
Mimi hofu yangu ni muda wa safari kuwa mrefu hivyo kushindwa kushindana na Fastest katika same root na hivyo kukosa faida na kushindwa kukua kibiashara. Sio mikoa yote ina idadi kubwa ya wananchi wanaweza kumudu kupanda ndege. Jamaa waumize kichwa na kufanya restructuring ya shirika sasa
Acha hofu na tafuta facts!
 
Inapendeza sana kama mtu anajadili mada kama hizi,awe na ABC ya usafiri wa anga na changamoto zake.
Fastjet tunaenda kukimbiza sana sana.Kwa sbb yeye anatumia ndege aina ya A319 inayobeba abiria 156.
Sisi tunaenda kuwa na Dash8-400 abiria 78.Safari ya Mwanza to Dsm,ATCL inatumia saa 1.20 hadi 25 wakati Fastjet anatumia saa 1.10 hadi 15.ATCL anatumia tani 1.2 kwa safari hiyo,wakati fastjet anatumia tani 3.1 za mafuta JET A1 kwenda Mwanza.

ATCL anatuwa viwanja vyote Tz vyenye lami na vile vya vumbi,wakati Fastjet anatuwa viwanja vitano tu Tz kwa maana ya Mwanza,KIA,Dsm,Znz na Mbeya.Huku ATCL akituwa Kigoma,Tbr,Mbeya,Lindi,Mtwara,Arusha,Iringa,Songea,Musoma,Dodoma,Mpanda nk

Ili fastjet atuwe na kuruka,Runway ya kiwanja inatakiwa iwe km 2.3 wakati ATCL anatuwa kwenye kiwanja chenye 1.2 km,ambavyo ndo viwanja vingi vilivyopo Tanzania.

Kwa kulitambua hili,Fastjet ameamua kuanza kuuza ndege zake zooote,ili anunue walau E190 aendane na ushindani wa soko.Kuepuka ghalama za mafuta na vipuri.

Sasa hapo ni nani anamtishia mwenzake?Muwe mnafanya utafiti kabla ya kutoa mchango

Unaweza kuwa ume fanya utafiti sahihi kabisa, hongera sana. Ila sijui tofauti za ndege ila nahisi unaweza kua ume tu potosha au vyombo vya habari vime tupotosha kidogo , Mwananchi ili tuambia kwanza ndege zitakazo kuja ni Bombardier Q 400, wewe ume tuambia bombadier dash 8-400 , siwezi li zungumzia hili kwa kua si mtaalamu, ila nadhani research yako kwa kua ulikua una lengo la kutu elimisha tusio fanya tafiti unge kua una tupa walau reference tujifunze zaidi.

Na kwa uelewa Mdogo usio wa kitaalamu wa mambo ya Anga, nadhani uwezo mkubwa wa kusafiri kwa haraka na uwezekano wa kupata abiria wengi ndio mafanikio ki biashara, ume toa tofauti za kukaa angani kwa ndege kwa safari ya MNZ - DAR , ume toa na uwezo wa ndege yetu kutua mahali kwingine, je vipi kuhusu soko la njia hizo zingine? Hivi wanao panda wana panda kukimbizana na muda au ili wasafiri na ndege? Mi nihisi kwamba biashara hii ina tegemea wingi wa abiria ( market) uharaka wa safari ( muda wa angani) na Huduma bora, bado naamini katika hili la HUDUMA bora tuta wapiku vibaya Fastjet kwa maana wana Huduma mbovu kwa wateja hasa wanapo hairisha safari au abiria akitaka kubadiri muda au siku ya safari....lakini si vinginevyo tuna hitaji kukimbizana na uli mwengu ili kesho tuweze kusogea hata nchi jirani.

NB : mimi si mtaalamu wa mambo ya anga najifunza tuu toka kwako
 
Mkuu Kaveli raha ya JF ni kujadiliana,haimaniishi mi najuwa sana kuhusu Aviation Industry ila na-share tu na wadau.

Kiukweli miaka ya nyuma tulikuwa na ndege zenye majina tofautitofauti sana,Kulikuwa na Boeing737 yetu iliitwa Kilimanjaro,kulikuwa na Serengeti,Ngorongoro,Tarangire nk.Hizi ndege zilipaa kote duniani na kuitangaza nchi yetu.

Yalikuja "manyang'au" fulani yakitajirisha na kuliibia shirika mpaka sisi wengine tukaikimbia nchi na kutoa michango yetu ktk nchi jirani.Tulikuwa na Boeing ya kwenda Addis Ababa kupitia Entebe mara mbili kwa week.Tulikuwa na moja ya kwenda London-Heathrow!!Mpaka kuna wakati tulikuwa tunaenda hadi Ulaya Mashariki.Hii anga dunia ilitambua Call Sign yetu kama "Tango Charlie".

Wahuni fulani wakalila shirika,tunaojuwa tunaona juhudi za kurirudisha,hatukumpigia kura JPM...ila kwa hili tunampa pomgezi....Tunaiona heshima ya "Tango Charlie" katika anga ya dunia ikirudi.

Kwa swali zuri uliloniuliza,nakuzawadia picha ya BOEING737 iliyopewa jina la "KILIMANJARO" tazama katika picha(Kutoka maktaba ya kumbukumbu zangu) mali yetu sisi Watanzania miaka hiyo sisi tukiwa Vijana.Iwe kumbukumbu kwako na wengine,kuwa Taifa hili la Tanzania liliwahi kuwa ni Taifa la watu wenye akili sana na mawazo mapana...Lakini walikatishwa tamaa na wanasiasa,kama watapewa nafasi basi nchi hii itakuwa kimbilio la masikini wooooote wa Afrika na Dunia

Nakupa picha hii kukupa uthibitisho kuwa "SIBAHATISHI" ktk maelezo yangu(NA KULA SIKUMPA MAGUFULI NA CCM KUANZIA NGAZI YA UDIWANI HADI URAIS)

Cc eddy MOTOCHINI UncleBen Belo Adharusi Papa Mopao View attachment 390180


Mkuu barafu, shukrani sana kwa nondo zako. Salute kwa 'maktaba ya kumbukumbu zako', angalau sasa nimepata japo ABCs kidogo ni wapi ATCL ilipotokea. Kumbe hili shirika lilikuwa well established kabisa, tena with intercontinental flight (to London)?!! Daah ama kweli nchi hii imetafunwa sana walahi. Ahsante kwa zawadi hii mkuu wangu.

Mkuu, hayo ''manyan'gau'' yaliyoliibia shirika na kulifirisi, bado yapo? yanafahamika? kuna jitihada zozote zilizochukuliwa by serikali ili nayenyewe kuyafirisi kisha kuyapeleka ngome yakanyee ndoo?

Hakika mkuu nimeguswa sana na maneno yako haya:

''...Taifa hili la Tanzania liliwahi kuwa ni Taifa la watu wenye akili sana na mawazo mapana...Lakini walikatishwa tamaa na wanasiasa,kama watapewa nafasi basi nchi hii itakuwa kimbilio la masikini wooooote wa Afrika na Dunia''.

-Kaveli-
 
Ndege ya ATCL angani ikipasua anga na mawingu kwa ajili ya Test Flight. Sasa ni tayari kwa safari ya kuja nyumbani.

Alama ya Twiga wetu inaenda kuruka na kutambaa katika milima na mabonde ya Tanzania. Tunarudi tena katika anga la Tanzania. Nia ya dhati iliyotumika kulifufua shirika hili, itumike pia kutuweka watanzania kama wamoja, kwa chuki na uhasama wa "kuminywa demokrasia", turudishwe na tuwe wamoja.

Tunaenda hatua kwa hatua,kwa ile kanuni yetu ya "JF be the first to know", welcome back home.

The Wings of the Kilimanjaro

View attachment 390071
Namwona Fast Jet akitafutiwa mlango wa kutokea taratiiibuuu.......
 
Jamani hivi mmiliki wa fastjet ni mtanzania au ? kama ni mtanzania mbona tunamwombea mabaya hivi na wakati anatusaidia sana kwa sasa? kama ni mtanzania tuendelee kumpa moyo , biashara ni ushindani , tazama Tanesco wanavyotutesa sababu tu hawana mshindani
 
Back
Top Bottom