Mganguzi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2022
- 1,032
- 2,759
Ilikuwa mwanzoni kabisa mwa mwaka 2000 nikiwa nyumbani pamoja na wazazi wangu katika mji mdogo wa tunduma karibu kabisa na shule ya msingi maporomoko.
Sitasahau wakati huo nilikuwa nikiishi na mama wa kambo baada ya kumpoteza mama yangu mzazi .maisha nyumbani yalibadilika ghafla na baba akawa ni mtu wa kulewa na kurudi usiku wa manane.
Ilikuwa akifika tu basi wote mtaamshwa kupigiwa makelele usiku kucha ,Mimi na wadogo zangu ambao wengine walikuwa wadogo kabisa, ilifika mahari tunalala njaa.
Yule mama wa kambo alibadilisha kabisa maisha na tabia za baba akawa ni mtu wa hovyo sana. Wanakula kilabuni wanarudi usiku Mimi nabaki napambana na wadogo wazangu na nilikuwa nataka kwenda chuo lakini Mzee kasema hawezi kupoteza pesa yake kunisomesha natakiwa nipambane mwenyewe.
Niliamua kujiongeza kufanya vibarua mchana jioni nikipata kitu napelekea wadogo zangu ndio hapo nilikutana na jamaa Mmoja anaitwa Alfred akanipa mchongo wa kwenda kuvua samaki ziwa rukwa.
Nilijichangachanga nikapata nauli nikawaaga wadogo zangu Kwa uchungu sana ilikuwa hakuna namna lazima nikapambane na Kwa vile jamaa alinipa matumaini ya kupata pesa nyingi Kwa muda mfupi nikaamini kabisa naenda kutoboa, tuliondoka Tunduma Kwa usafiri wa fuso kuelekea bonde la ziwa rukwa kupitia laela, Kalambanzite na usiku karibia Saa nne tukafanikiwa kufika Kijiji Cha Ilemba ambapo ndio mwisho wa gari.
Tukalala asubuhi mapema tukaanza kutembea Kwa mguu nakumbuka tuliamka Saa 12 mapema.
Kuendelea bonyeza kiungo hapo chini
Sehemu ya pili
Sehemu ya tatu
Sitasahau wakati huo nilikuwa nikiishi na mama wa kambo baada ya kumpoteza mama yangu mzazi .maisha nyumbani yalibadilika ghafla na baba akawa ni mtu wa kulewa na kurudi usiku wa manane.
Ilikuwa akifika tu basi wote mtaamshwa kupigiwa makelele usiku kucha ,Mimi na wadogo zangu ambao wengine walikuwa wadogo kabisa, ilifika mahari tunalala njaa.
Yule mama wa kambo alibadilisha kabisa maisha na tabia za baba akawa ni mtu wa hovyo sana. Wanakula kilabuni wanarudi usiku Mimi nabaki napambana na wadogo wazangu na nilikuwa nataka kwenda chuo lakini Mzee kasema hawezi kupoteza pesa yake kunisomesha natakiwa nipambane mwenyewe.
Niliamua kujiongeza kufanya vibarua mchana jioni nikipata kitu napelekea wadogo zangu ndio hapo nilikutana na jamaa Mmoja anaitwa Alfred akanipa mchongo wa kwenda kuvua samaki ziwa rukwa.
Nilijichangachanga nikapata nauli nikawaaga wadogo zangu Kwa uchungu sana ilikuwa hakuna namna lazima nikapambane na Kwa vile jamaa alinipa matumaini ya kupata pesa nyingi Kwa muda mfupi nikaamini kabisa naenda kutoboa, tuliondoka Tunduma Kwa usafiri wa fuso kuelekea bonde la ziwa rukwa kupitia laela, Kalambanzite na usiku karibia Saa nne tukafanikiwa kufika Kijiji Cha Ilemba ambapo ndio mwisho wa gari.
Tukalala asubuhi mapema tukaanza kutembea Kwa mguu nakumbuka tuliamka Saa 12 mapema.
Kuendelea bonyeza kiungo hapo chini
Sehemu ya pili
Sehemu ya tatu