Yahusu wafufuao wafu na misukule

Yahusu wafufuao wafu na misukule

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,681
Reaction score
830,653
Hili jambo miaka mitatu nyuma lilikuwa maarufu sana, yaliibuka makanisa ya mitume na manabii kwa kasi ya ajabu yaliyokuwa kila wakati yakituonyesha picha za wafu waliokufa kimazingara na baadae kufufuliwa nao.

Karata hii isiyo na chembe ya haya wala soni ya udanganyifu ikawapatia waumini wengi na umaarufu mkubwa.

Gwajima bingwa wa haya mazingaombwe kwa kujiamini kabisa aliutangazia uma wa waumini wake kuwa angemfufua Marehemu Amina Chifupa RIP, watu wakausubiri kwa hamu muujiza huu, Chifupa mpaka leo hajafufuka.

Maumivu yalibaki kwa mtoto wake na ndugu zake ambao jina la ndugu yao lilitumika kwa malengo binafsi huku magazeti ya udaku yakiwa kichocheo kikuu

Watu wote tuliowaona wakifufuliwa hatujawahi kuonyeshwa ndugu zao na historia zao, sijawahi kuona mtu wa Dar akifufuliwa au mtu ninayemfahamu, bali mtu wa dar alifufukia Arusha, wa mwanza alifufukia dar nk.

Upofu wa imani ukawafanya wengi wakimbilie kwenye haya makanisa, lakini sasa mambo yamebadilika na uongo wao umejulikana! Siku hizi kufufua misukule sio dili tena, kilichopo ambacho nacho kinakufa ni kutoa mapepo! Hivi mapepo yanakaa kwa akina mama tuuu!?

Imani ni kitu kizuri pale tu unapojitambua kuwa unaamini nini na kwa nini! Hawa manabii na mitume wa uongo wamechuma Mali nyingi kwa waumini wapumbavu! Serikali iliangalie hili kwa makini yasije kutokea yaliyotokea Uganda, Kenya na ulaya kule watu waliojiuwa kwa maelfu kwa maagizo ya viongozi wao wakiamini kwa kufanya hivyo watakwenda peponi.
 
Wewe mtani wangu acha tu,
Wapo watu hata leo hii wanaamini kuwa wakienda
kwa gwajima mfu wao atafufuka.
Hata wasomi wazuri wa Biblia usishangae unapoambiwa
kuwa wakifiwa wanapeleka maiti huko ili ikafufuliwe,
cha ajabu ni kwamba wanarudi na mfu wao.

Hili la mapepo, hawa wahubiri huwa wanatumia mbinu moja
anapokuwekea mikono anakupush nyuma kiasi kama hauna
balance ni lazima utaanguka tu.

Na ndiyo maana akina mama wengi ndio wanaanguka
si hatuna nguvu sana.
 
yan hapa arusha ndousiseme...wa mama wanadanganyka na hayo makansa kwa arusha kansa lnalojulkana kwa ss ni kwa nabii malisa...wanaambiwa njoen mtolewe majin kahaba
 
Umeongea ukweli yani hadi inakera wakristu wamekua bendera fuata upepo,neno lnasema jaribuni kila roho inayodai inatoka kwa Mungu siyo unaenda tuu kama gari bovu
 
wachungaji wa makanisa ya kiroho

Ni sawa kabisa na makalmanzila
Wanachokifanya ni kucheza na akili za wateja wao

Siku hizi kuna maji ya upako vitambaa vya baraka nk nk imani imehamia kwenye vitu vya kidunia kuliko uchaji wa rohoni

Siku hizi mtu akihubiri vizuri madhabahuni anatunzwa na kwakweli mahubiri yenyewe si lolote bali mipasho

Siku hizi huna haja hata ya kwenda kanisani unafungulia TV halafu unamwangalia kidume anavyomwaga mbwembwe kishapo anaweka namba za simu halafu unatuma sadaka/ mchango wako naye anakuombea
 
ukweli wote wanaujua wahubiri wa hayo makanisa
 
Ndugu mshana jr Unabii sharti utimie.

Bwana Yesu alitutahadharisha kuwa siku za mwisho watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo watapotosha wengi..na bado tutashuhudia mengi zaidi ya haya na waathirika wakubwa ni akina mama.
 
Last edited by a moderator:
Mtaani kwetu lilikuja kanisa la mungu bendera,

acha wamama walivyopapatikia,
wanaambiwa wapeleke mafuta ya vaseline
ili wakapwe eti kuondoa mikosi,
sasa uliza hayo mafuta wanapakwa wapi, ni aibu.

hapo ndipo mioyo ya wengi ufungwa hasa wanawake aisee ... ila wamama tunaendeshwa na hisia zaidi kuliko uhalisia
 
Back
Top Bottom