Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa


Hapo mkandara i agree with you, huwezi kutekeleza mambo ya kwako binafsi kwa niaba ya taifa lazima yawe documented ili yeyote atakaepewa madaraka aweze kutekeleza na wananchi wampime ya aliyoyaeleza. CHADEMA wameeleza kila kitu kwenye Katiba, ilani ya uchaguzi na sera zao pia. kama kama hukubaliani nadhani unatakiwa kukosoa kwenye hizo documents zao. Then what??? zipelekwe kwenye hizo sera na zionyeshwe mapungufu yake ili Then what??? ipate majibu kwa kukosoa na kutoa ALTERNATIVES.
 

Mkuu MMKJ,

Nashukuru hatimaye umejitokeza na kuweka msimamo wako! Lakini kutokana na quote hapo juu nini ilikuwa lengo la CCJ? Unataka kutueleza mlitaka kueneza itikadi tuuuuuuu, halafu basi?!! Kama sikosei mliwahi kusema CCJ itafanya nini ndani ya siku 100 ikipata kuingia magogoni!!! Kama nakumbuka sawa, moja ya mkakati ilikuwa kuwafikisha mahakamani wote waliohujumu nchi hii katika ufisadi tunaoendelea kuuona!!

Hebu tueleze kama CCJ ingepata usajili wa kudumu ndani ya muda huu ingefanya nini pia? Maana kuna post moja uliwahi sema mabadiliko nchi hii yatatokea Oct 2010, what did you really mean? Maana muda si mrefu tukaona CCJ, mara tukajua wewe ni kati ya wanachama waanzilishi!!!

Je unataka kutueleza CCJ ingepata usajili isingekuta na vikwazo unavyotueleza hapa!!! TUME YA UCHAGUZI, DOLA, WIZI WA KURA...et cetera!!!

Mkuu mimi nadhani kuna haja na kusubiri uthubutu wa CHADEMA tuone!!! Niliwahi kusema hapa, kwamba sikibezi kamwe CCJ, ila disappointments ndizo zinazoumiza, specifically nilizitaja zile za 1995!!! Sasa mnatuelezaje CCJ?

Kwanini msiingie/msitoe ushauri kwa CHADEMA wa kuvuka mstari unaouongelea!!! Namna hii CCM imeshansinda mkuu. Maana inaanzia kushinda kwenye fikra zetu!!!
 
Ukweli utabaki palepale, watanzania wanahitaji kiongozi anayeweza kubadilisha hali zao kuwa bora zaidi. Na huyu lazima aweze kuwaambia atafanyaje hili. Na aweze kuwaambia kwa lugha rahisi sana na si huendelea kuorodhesha matatizo wanayoletwa na uongozi uliopo. Hili wanalijua vyema pengine kuliko hao wanasiasa. Hili la vipi watafanya hilo vizuri kuliko CCM na kipi so far wamefanya kuelekea huko ni muhimu kwa wapiga kura wasikie.

Ukilalamika kwa mwenye njaa kuwa chakula kipo humu ndani ila tu nimenyimwa ufunguo wa chumba ningekupatia haimsaidii chochote mwenye njaa. Anakuona nguvu yako na yake ni sawa. Ukiweza kuvunja huo mlango au ukamweleza mbinu atakazoziamini utakazotumia kumpatia hicho chakula anaweza kukulinda utumie hizo mbinu. Mwamuzi mpiga kura
 

Mkuu MMKJ,

Nashukuru hatimaye umejitokeza na kuweka msimamo wako! Lakini kutokana na quote hapo juu nini ilikuwa lengo la CCJ? Unataka kutueleza mlitaka kueneza itikadi tuuuuuuu, halafu basi?!! Kama sikosei mliwahi kusema CCJ itafanya nini ndani ya siku 100 ikipata kuingia magogoni!!! Kama nakumbuka sawa, moja ya mkakati ilikuwa kuwafikisha mahakamani wote waliohujumu nchi hii katika ufisadi tunaoendelea kuuona!!

Hebu tueleze kama CCJ ingepata usajili wa kudumu ndani ya muda huu ingefanya nini pia? Maana kuna post moja uliwahi sema mabadiliko nchi hii yatatokea Oct 2010, what did you really mean? Maana muda si mrefu tukaona CCJ, mara tukajua wewe ni kati ya wanachama waanzilishi, tukaunganisha dots tukaelewa maneno yako!!! Sasa mara hii yamebadilika...!!!

Je unataka kutueleza CCJ ingepata usajili isingekuta na vikwazo unavyotueleza hapa!!! TUME YA UCHAGUZI, DOLA, WIZI WA KURA...et cetera!!!

Mkuu mimi nadhani kuna haja na kusubiri uthubutu wa CHADEMA tuone!!! Niliwahi kusema hapa, kwamba sikibezi kamwe CCJ, ila disappointments ndizo zinazoumiza, specifically nilizitaja zile za 1995!!! Sasa mnatuelezaje CCJ?

Kwanini msiingie/msitoe ushauri kwa CHADEMA wa kuvuka mstari unaouongelea!!! Namna hii CCM imeshansinda mkuu. Maana inaanzia kushinda kwenye fikra zetu!!!
 
 

Mkuu,
Asante, mchango wako umeonekana. May i say, hii ndo rai ya wengi kwako. Yawezekana CHADEMA wamekosa techinical team kwenye hili. Ndo maana tunataka kuunganisha nguvu. Umetueleza ulikuwa unafahamu uwepo wa mazungumzo kati yenu (CCJ na Chadema). Kwani hamku-identify mapungufu yao, ushauri wenu kabla ya kuwaruhusu to layer waende?

Issue mkuu wangu, why not joining forces against the common enemy?
 

Inamaana chadema hawana sera? Kama ni vyama vyote nafikiri vinazo.
 
Msiulize ulize maswali mengi kwenye kazi za watu!. Wata wanauliza tuu, wanauliza tuu, wanauliza tuu na hawajibiwi, hivi hamuelewi tuu!.
Na wewe endelea kuuliza.

Pasco nimekusoma mkuu, mimi nahisi Mkuu MKJJ ni aidha yuko kazini au ni selfish! Mimi sioni tofauti ya kuwashauri wale walio kwenye nafasi ya kupambana na adui na kung'ang'ania lazima uwe wewe. Hivi kuna nini kwenye hili swali la MKJJ? CCJ imeshindwa kuchomoza, si ungetumia nafasi ya amzungumzo kuwapa CHADEMA terms za CCJ kuungana nao; mkaelezea benefit watakazopata mkijoin forces, maana CCJ mlikuwa na mikakati mizuri!!! Nini tatizo?

Wewe si ndiyo ulitueleza mabadiliko ni 2010 na siyo 2015!!! What happenend mkuu? This hurts mkuu!! So baada ya kushindwa mmeshindwa hata kutoa press conference kuelezea way forward?
 

Salaam,

You are right kuwa America as a nation doesn't go anywhere without knowing watapata nini BUT what MM is trying to say kwa uelewa wangu ni kuwa waliwa-underestimate Iraqis and now angalia death toll and the whole region is not stable.
 
we MM, please usiwachanganye wana JF... kubali ulichemsha kuunga mkono mawazo yaliyodhoofu kiasi cha kufa yakiwa na umri wa miezi mitano tu.....

najua mbegu ikianguka ardhini, lazima ife na ioze kiasi ili iweze kuota na kumea... lakini inachekesha kuwa ccj imeoza kiasi cha kutoweza kumea tena..... hahaha... MM tafakari upya kuhusu siasa za TZ...
 

Well said!!
 
katibu wa muda wa CCJ Renatus Muabhi amesema haya:
1. kuhama akina mpendazoe, ngihili na kiyabo si kuhama kwa chama kizima
2. si lazima kila mwanasiasa agomee ubunge
3. waliojiunga CCJ kwa ajili ya kugombea ubunge ama urais bila malengo ya muda mrefu na chama waanze sasa kuonda kuwafuata hao akina mpendazoe wanaotangatanga kutafuta ubunge na maarufu wa kujidanganya
4. CCJ bado ipo na bado ina wanachama
5. CCJ itaendelea kushrikiana na msajili wa vyama vya siasa ili kuhakikisha kinapata usajili wa kudumu
6. kana lengo la mpendazoe lilikuwa kugombea ubunge, ni heri angebaki CCM
7. kwa umaarufu mpendazoe alioingia nao CCJ, kuondoka kwake kumekipa CCJ ahueni kubwa

my take:
mpendazoe (aka mpendazote) ni mrema mwingine hatari zaidi kutoka kishapu. ni mrema wa awamu ya nne. kama mrema alivyojiunga NCCR mageuzi akaksambaaratisha na kuhamia TLP na kukia umaarufu wa muda kabla ya kukisambaratisha pia na kurudi nyumbani (CCM) ndivyo alivyofanya mpendazote. karukia chama-mimba (CCJ) kakisambaratisha na sasa kaparamia chadeA. NAWATAHADHARISHA CHADEMA WASIJE WAKAJIDANGANYA KUMPA CHEO CHOCOTE. ABAKI KAMA MWANACHAMA WA KAWAIDA TU A KAMWE WASIMKABIDHI MIKE KUKISEMEA CHAMA,. wasithubutu hata kumpa u-MC katika sherehe za chama, histoia itakulakwao.

hongera muabhi kwani angalau umedhihirisha kuwa wewe na wenzio wachache ndio mlijua nini mnakifanya na harakati za kisiasa kupitia CCJ

ole wenu chadema. hukumu ya NCCR mageuzi inawanyemelea, huyo mliyempokea jana ni "mrema mpya"....

ni mtazamo tu..
 
Wale wote wakina mpendazote ni najaa nakikundi chake kwani hapa tanzania tunahitaji upinzani waweli sio upinzani njaa!!
 

this makes sense. Lakini nadhani sera za Chadema zipo wazi! Labda kwa sasa hawajazipa kipaumbele...lakini mimi najua 100% kuwa wao wana mipango gani baada ya kumuondoa CCM. Kwa hiyo sidhani kama ni Chama kisicho na mbele wala nyuma...chenye dhumuni la kuiondoa CCM tu...au kwa kutumia mfano wako...kuokoa watu tu! nadhani kwa sasa wewe umeumia sana kutokana na tarumbeta nyingi ulizopuliza juu ya CCJ. Kwa hiyo unajaribu kwa hali na mali kuwapa wenzako jeraha. Ivi CCJ ilikuwa na sera gani tofauti? Kushtaki mafisadi?

Tuaangalia mfano wa moja ya sera za Chadema:
Sera ya Utawala

Utawala wa Ukiritimba na Urasimu, ukoje?​
Ii this not good enough as an answer to your 'what then' question? Labda tatizo ni wewe kudhani kuwa unajua zaidi ya wengine!
 
Mzee Mwanakijiji,

Binafsi nakupata kwa nguvu ya mia! Tangu nilipoona kwenye TV kwamba hawa ndugu zetu wameamua kutoka CCJ na kujiunga na CHADEMA nilipatwa na mshangao mkubwa. Kumbe wenzetu hao wao walikuwa wakiwaza namna ya kupata ubunge tu zaidi ya kitu kingine chochote?

Mabandiko mengi yanayong'ang'ania ulazima na umuhimu wa kuungana na CHADEMA ili kuing'oa CCM yanadhihirisha jinsi ambavyo bado mawazo yetu yamejikita kwenye madaraka na kutaka kutawala zaidi ya ni kwa mbinu gani na namna gani tunapanga kuuendesha utawala huo ili uweze kukidhi haja iliyopo ya utawala uliotukuka utakaonufaisha wananchi wetu na kulitoa Taifa letu katika lindi la tope.

Tunao mfano hai wa namna ambavyo Watanzania wengi kwa miaka mingi sana tulikuwa hatuelewi ama hatutaki kukubali ukweli wa yale tuliyokuwa tukiyasikia na kuyasoma kwenye hotuba za Mwalimu Nyerere juu ya mambo mengi yanayohusu mustakabali wa nchi yetu. Wapo wengi ambao walifika mbali na kudiriki hata kumkejeli Mwalimu kwamba Mzee huyu 'mchonga' naye tumechoka anaongea sana n.k. Wale wale waliokuwa wakimbeza Mwalimu, baada ya Mwalimu kuondoka kwenye ulingo wa siasa na kutoweka duniani, wamerudi na kuanza kushangaa kuona kwamba mengi aliyokuwa akiyasema Mwalimu yalikuwa ni sahihi na yenye manufaa makubwa kwa mustakabali wa nchi yetu, Afrika na hata dunia kwa ujumla.

Swali ni lilelile, watu wenye imani na mitazamo tofauti ya kisiasa tukishaungana na CHADEMA na kuiondoa CCM nchi tunaiendesha kwa mfumo upi? Au ndio ili mradi tumepata huo ubunge na urais basi itakuwa 'bora liende'. Tutakuwa hatujajitendea haki wala kutendea haki wananchi na Taifa kwa ujumla.

Mie kwa 'ujinga' wangu nilidhani kwamba hata kama CCJ kimenyimwa usajili wa kudumu, kazi iliyopo ni kujipanga upya na si kukimbilia kujiunga na vyama vingine kwa ajili ya kuwania ubunge ambao unaweza usipatikane!
 
Boramaisha,
Mkuu maelezo yako yanaweza kuonekana yana mantiki sana kifikra lakini mkuu wangu haya ndio mawazo ya Wadanganyika..Mawazo ya Kisoshalist ambayo yametufunga Tanzania kwa miaka 50 chini ya utawala wa chama kimoja pasipo maendeleo na kila siku tukifikiria labda kesho au mimi ndiye mwenye suluhisho..

Wala sioni ajabu kwa Wadanganyika kwani ubishi ni utamaduni wetu. Fikra za kupaka rangi juu ya rangi ya zamani tukifikiria ndio ukarabati, kushindwa kuziba ufa kwa kuhofia gharama zake..lakini hata siku moja hatuwezi kukubali moja kwa moja hofu yetu isipokuwa kutunga sababu za kutaja wachawi.

Ni kwa mtaji kamahuu tumeshindwa kuunda jumuiya imara za Kitanzania nchi zote za nje isipokuwa kwa makundi makundi..kila kundi likilaumu kundi jingine kwa kutokuwa na sera zinazokubalika. Kila mmoja wetu ana mawazo yake, nia yake na mengine mengi ya kibinafsi hadi siku wanaposhikwa na shida ndipo hutafuta umoja wa watanzania ambao haupo isipokuwa kwa kualikana ktk Facebook na Michuzi.

Hapa nilipo tumeshindwa kuunda Jumuiya ya Watanzania kwa UMOJA isipokuwa tumegawanyika kwa makundi wengine wakifikiria wao ni wasomi na wenye nguvu ya kuunda jumuiya kuliko wengine. Matokeo yake tuna Jumuiya tatu za Kitanzania mji mmoja na hakuna hata mojawapo iliyojijenga kukabiliana na maswala yoyote ya kimaendeleo isipokuwa majungu na kurushiana maneno baada ya..It's sad!

Wadanganyika kwa umaskini wetu tuna wivu, inda na hasira za kwa nini hasa kutokana na Ujinga, umaskini na maradhi ambayuo kama huna wewe basi ndugu zako wapo ktk hali hiyo. Na kila mmoja wetu anajitahidi yeye mwenyewe atoke kama samaki kaa waliokusanywa ndani ya tenga. Mwisho wa yoote haya kaa wote watachomwa na mafuta ya moto na kuishia mezani.

Mkuu wangu haya maswala hayakuanza jana, nakumbuka uchaguzi wa mwaka 2005, hibvi hivi tulianza karibia na uchaguzi tukiipinga Chadema kwa kuanzisha mijadala inayowadhalilisha Chadema ili mradi kuwapa nguvu CCM. Na hakika naweza sema Mzee Mwanakijiji anatumia nafasi hii kwa fikra zile zile za Kidanganyika..ili mradi Chadema kionekane ni chama dhaifu badala ya yeye mwenyewe kujiunga nao na kukiimarisha chama hiki. Nakumbuka vizuri Mbowe akizungumzia fikra za mwalimu ktk uchaguzi uliopita akabezwa na matusi kibao sikuwaona mkijitokeza kumpa support kama kweli nyie mlikuwa wafuasi wa mwalimu.

Mimi sii mvivu wa kufikiri wala mchovu wa kumbukumbu..kwani nakumbuka hata kijiwe hiki cha JF kilipoanza kilipigwa vita sana tena vibaya sana tukabakia watu wachache sana tukiendelea kuchangia mawazo yetu na kushirikiana na wahusika pamoja na vishindo vyuoote vilivyokuwepo. Tulibezwa kwa maneno ya kila aina lakini JF survived na leo hao hao Wadanganyika wamerudi na wengine ndio wasemaji wakubwa na hakika wamesahahu kwamba walisema hiki ni kijiwe cha watu 1,000 tu, has no impact to the nation.

Kwa hiyo mkuu wangu nakuelewa sana unapozungumza hoja yako. Na hakika hakuna mtu hapa JF ambaye alikuwa mshabiki wa fikra za mwalimu kama mimi toka tumeanza nimekuwa nikizitetea hata kabla ya kuona mapungufu ya Utawala uliopo. Toka nimejiunga JF na kabla hya hapa nimetetea fikra za mwalimu pamoja na kushindwa kwake Kiuchumi, leo hii nawaona mkirudi na kukubali matokeo baada ya miaka 20 kupita. Sikujiweka pembeni na Watanzania wenzangu kwa sababu nyote mlimkubali Mwinyi, Mkapa na hata JK na falsafa zao zinazotupeleka ktk utandawazi na soko huria mikono mitupu kama vile tupo ktk maonyesho ya sabasaba.

Wakuu zangu najua wapo watu wangu wa karibu sana kina Rev.Kishoka, Brutus, Kichuguu, Nyani Ngabu na wengine wengi ambao wana mashaka na utaratibu wa uongozi wa Chadema. Na mimi wala siko mbali nanyi, ila kinachoniunganisha nao sio kujua nani ni nani ktk utawala isipokuwa swala zima tunalokabiliana nalo sasa hivi. Trust me, I would rather deal with Chademna tomorrow kuliko kuona CCM wakichukua madaraka tena mwaka 2010. Na hakika nitajikata kabisa na maswala haya kama nilivyokata tamaa ktk kuunda jumuiya za Kitanzania.

Pengine hii ndio aliyokuwa akizungumzia mwana JF mmoja kwamba UJAMAA na KUJITEGEMEA haviwezi kuwa pamoja kwani nachokiona ni kizazi cha (mwalimu) Watanzania WABINAFSI wanaotaka kuunda UMOJA - Haiwezekani....
 

Mkuu sometimes huwa unaniacha hoi sana,huwa nashindwa kukupata unachokisimamia hasa..Unaenda mbele halafu unarudi nyuma..
 
Here is the problem that I see with Mwanakijiji. First, I've got to give it up to him...the phrase 'giving up' does not exist in his book. Secondly, and this is what I see is his main problem (not necessarily a bad problem). He has a propensity for ballyhooing things. I often say it to myself that this guy would've made a good salesman (if he's not one already). He has a way with words that he can persuade just about anyone into believing in something he believes in. I remember when he launched his KLHNews...man...you should've heard how he was hyping it up...but where is it now? It's defunct. And the same thing goes for this CCJ thing. He almost got me sold into believing they were for real.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…