Ya Zombe na ustawi wa mob justice Tanzania

Mimi sisikitiki kuachiwa kwa zombe na team yake. Pengine kweli hawana hatia kwa mujibu wa sheria. Pengine wana JF mnisaidie kujua nani mkweli kati ya vyombo hivi vya dola: Plisi au tume iliyopeleleza hiyo kesi na jaji masati aliyetoa hukumu. Nani anaamini kipi kati ya hivi viwili na kwa nini? Mimi nadhani baada ya hukumu kutolewa jana serikali inawajibika kupitia vyombo vyake husika kuwaeleza wananchi kuwa nani waliwaua hao vijana au hatua zipi zinafata baada ya wale iliodhani walihusika kugundulika kuwa siyo!!!. Vinginevyo wananchi wataanza kukosa imani na ama polisi kwa kutoa upelelezi fake ama mahakama. Tujiandae kusikia pia kesi zote za mauji ya ndugu zetu albino zimekosa wa kutiwa hatiani!!!

Tafadhali mwenye nafasi ya kujibu swali langu la msingi "nani mkweli wapelelezi au jaji mtoa hukumu na kwa nini unaamini hivyo?"
 
Wataalam wa sheria hapa JF mko wengi,hebu niambieni maana sio mjuzi wa sheria.Iwapo askari waliohusika kwenye tukio wamekiri wenyewe kuwa waliuwa kwa maelekezo ya Bosi wao na eneo la tukio wamewapeleka waheshimiwa wa tume iliyoundwa kufuatilia tukio je ni ushahidi gani mwingine unaohitajika kama sio kuona wananchi kama majuha kuchezea akili zao.Na wale askari wenye silaha nzito waliokuwa pale kabla na baada ya hukumu kusomwa si maana yake matokeo yalishajulikana ila ilikuwa zuga tu?
 
Sheria imechukuwa Mkondo wake!
Haki ni kitu kingine!
Tuanze na DPP. Watakata rufani,lakini wameshashindwa kwenye mahakama ya "watu" tayari.Hawana credibility(wapandaji daladala mmeyasikia!). Watu kujichukulia sheria mikononi kutaongezeka.Imekuja wakati mbaya sana hususan swala hili linachanganywa na jambo lingine kabisa la Spika6
 
Kevo na libidozy,

Elimu ya kutosha kuhusu sheria ni ipi? Binafsi naomba ufafanuzi kwenye hilo!

Nahisi nyote wawili mmekaa kwenye madarasa ya Vyuo Vikuu na "mkasomea SHERIA", kwahiyo badala ya kuwaita wachangiaji "vilaza" na majina mengineyo tuchambualie mwenendo wa hii kesi kwa faida ya forums nzima

Kukaa pembeni na kusema "nyie ni vilaza" na "hamjuai sheria" ni tabia ya ubinafsi na kutaka kujionyesha unafahamu jambo kuliko wengine! (Anyways, ..ndivyo Tulivyo)

Mwisho, Wakili wa Serikali hakusema kuwa watakata rufaa, bali alisema anawapelekea WAKUBWA (ingawa naye anaifahamu sheria) ile hukumu hili watoe uamuzi ndani ya siku kumi na nne!

Walichokifanya wanasheria WA serikali ni wametoa notisi ya ku-appeal ambayo inatolewa ndani ya 14 days then appeal ndio inakuwa lodged mahakamani ndani ya 40 - 60 days.
 
Sifikirii kama kuna cha kulalamika dhidi ya maamuzi yaliyotolewa.

hakika kazi ya hakimu/jaji (mahakama) ni kuamua kile kilicholetwa nbele yake na sio kumuhukumu mtu kwa kosa asiloshitakiwa nalo.

hakika wakina zombe wana hatia lakini sio kwa kosa la mauaji bali labda DPP angewashitaki kwa kosa la kupanga njama za kuwauwa wafanyabishara na kupora mali zao ikiwemo pesa.

Kosa lipo kwa DPP kuwashitaki kwa kosa mbalo sio lao.
 
Courts everywhere in the world are the sole architect of MOB JUSTICE!! by Mshiiri 2009
 
ndo maana sikupoteza muda kufikiria hukumu ya zombe itakuwaje,that is the real situation ya Law firm in tanzania, hakuna jipya wote njaa tupu.
 
Sifikirii kama kuna cha kulalamika dhidi ya maamuzi yaliyotolewa.

hakika kazi ya hakimu/jaji (mahakama) ni kuamua kile kilicholetwa nbele yake na sio kumuhukumu mtu kwa kosa asiloshitakiwa nalo.

hakika wakina zombe wana hatia lakini sio kwa kosa la mauaji bali labda DPP angewashitaki kwa kosa la kupanga njama za kuwauwa wafanyabishara na kupora mali zao ikiwemo pesa.

Kosa lipo kwa DPP kuwashitaki kwa kosa mbalo sio lao.

Sawa kabisa!
 
Mimi sisikitiki kuachiwa kwa zombe na team yake. Pengine kweli hawana hatia kwa mujibu wa sheria. Pengine wana JF mnisaidie kujua nani mkweli kati ya vyombo hivi vya dola: Plisi au tume iliyopeleleza hiyo kesi na jaji masati aliyetoa hukumu. Nani anaamini kipi kati ya hivi viwili na kwa nini? Mimi nadhani baada ya hukumu kutolewa jana serikali inawajibika kupitia vyombo vyake husika kuwaeleza wananchi kuwa nani waliwaua hao vijana au hatua zipi zinafata baada ya wale iliodhani walihusika kugundulika kuwa siyo!!!. Vinginevyo wananchi wataanza kukosa imani na ama polisi kwa kutoa upelelezi fake ama mahakama. Tujiandae kusikia pia kesi zote za mauji ya ndugu zetu albino zimekosa wa kutiwa hatiani!!!

Tafadhali mwenye nafasi ya kujibu swali langu la msingi "nani mkweli wapelelezi au jaji mtoa hukumu na kwa nini unaamini hivyo?"

Unapotoa maoni ukiwa na data ni jambo jema sana. Tume ya Kipenka ilisema kuwa watuhumiwa 15 wafikishwe mahakamani. Kwa bahati mbaya watuhumiwa watatu (ambao ndio wauaji) walitoroka na hawakufanikiwa kufikishwa mahakamani. Ushahidi wa Lema wa maelezo aliyotoa polisi (statement) ambaye alishuhudia victim wakiuawa haukupewa uzito kwa sababu alifariki kabla ya kutoa ushahidi mahakamani. Kwa upande wa polisi walipeleka washtakiwa waliowakuta ila sio walioua (walisaidia hata hivyo kutenda kosa na baadhi yao walikuwepo eneo la tukio). Jaji kwa upande wake alisema kulingana na sheria kwamba huwezi kumhukumu mshtakiwa kwa kumsaidia mtenda kosa (principal offender) wakati huyo mtenda kosa hajatiwa hatiani! Sasa unapouliza nani mkweli unamaanisha nini? Polisi na Tume ya Kipenka walifanya fact finding wakati Jaji Masati alikuwa anataka kuprove guiltiness au innocence ya washtakiwa kwa kulinganisha na facts pamoja na ushahidi!
 
Ndiyo kwanza Zombeeeee anatanua mitaani. EID mosi alisali sala ya Eid pale Mnazi mmoja na alikuwa Row ya tatu, ya kwanza our president na ya pili his son Riz (of course na watu wengine). Hapo nimetaja maarufu tu kwa kila row japo na akina Kova alikuwa row ya pili pia??

Kwa kawaida imtuhumiwa wa mauaji ana mambo muhimu kuachiwa huru au kunyongwa hadi kufa. Ili anyongwe ni lazima u-prove beyond doubt kuwa aliua, ukishindwa tu ku-prove ujue kuachiwa huru ni must. Ndicho walichoshindwa k-prove watu wa Mwendesha Mashtaka.

By the way ile appeal vipi?? Bado ipo au ni viini macho as usual?? I ama fraid kama wata apeal watashindwa tena. Kilichopo wanatakiwa wa-frame case nyingine dhidi yao ambao kama wakikutwa na makosa basi watapata adhabu nyinginezo nje ya kunyongwa na maisha.
 
Ndiyo kwanza Zombeeeee anatanua mitaani. EID mosi alisali sala ya Eid pale Mnazi mmoja na alikuwa Row ya tatu, ya kwanza our president na ya pili his son Riz (of course na watu wengine). Hapo nimetaja maarufu tu kwa kila row japo na akina Kova alikuwa row ya pili pia??

Kwa kawaida imtuhumiwa wa mauaji ana mambo muhimu kuachiwa huru au kunyongwa hadi kufa. Ili anyongwe ni lazima u-prove beyond doubt kuwa aliua, ukishindwa tu ku-prove ujue kuachiwa huru ni must. Ndicho walichoshindwa k-prove watu wa Mwendesha Mashtaka.

By the way ile appeal vipi?? Bado ipo au ni viini macho as usual?? I ama fraid kama wata apeal watashindwa tena. Kilichopo wanatakiwa wa-frame case nyingine dhidi yao ambao kama wakikutwa na makosa basi watapata adhabu nyinginezo nje ya kunyongwa na maisha.
tatizo na sisi wa Tanzania tunahukumu watu kwenye magazeti, na vyombo vya habari...ndo maana eti tunaamini kuwa zombe mpaka haki itendeke lazma angefungwa. Nakubaliana nawewe mkuu kuwa hizi kesi si rahisi kabisa...mpaka mtu u prove beyond reasonable doubt..
 
tatizo na sisi wa Tanzania tunahukumu watu kwenye magazeti, na vyombo vya habari...ndo maana eti tunaamini kuwa zombe mpaka haki itendeke lazma angefungwa. Nakubaliana nawewe mkuu kuwa hizi kesi si rahisi kabisa...mpaka mtu u prove beyond reasonable doubt..

Tatizo halikuwa kuprove kesi ila ni kwamba wauaji (polisi Saad na James ambao walitoroka na hawajulikani walipo) hawakuwepo mahakamani. Sasa utamhukumu aliyesaidia kutenda kosa wakati mtenda kosa mwenyewe hakuhukumiwa? Sio sheria isemavyo!
 
Back
Top Bottom