Ww unakumbuka ulianza na simu ipi????

Ww unakumbuka ulianza na simu ipi????

mie siemens c21 kama sikosea ndo watu wa kwanza kwanza sikumbuki hata kampuni ya simu iliitwaje
 
Nilianza na C25, then nika upgrade kwa 3210, nikamrithisha ndugu yangu, then nikaenda 1100, huko mbeleni mimesahau.
 
Siemens c25 nimeitundika kiunoni hahahahaaaa umenikumbusha kuna jamaaa nilimuomba nim-bipu kaka ili anipigie jamaa akanijibu kuwa simu yake haina button ya kubipia.....I can not forget this till i die

Mpwa huyo jamaa katili sana !
 
Mimi nilianza na simu 1, aka jeneza sasa nipo na Nokia C3
 
Kuna dada mmoja kipindi hicho alikuwa anatamba kuwa mchumba wake anamiliki mobiteli (akimaanisha simu ya mkononi) jamaa yake huyo alikuwa akija lazima aiweke mezani kwa mikogo du! tumetoka mbali
 
Siemens c25 nimeitundika kiunoni hahahahaaaa umenikumbusha kuna jamaaa nilimuomba nim-bipu kaka ili anipigie jamaa akanijibu kuwa simu yake haina button ya kubipia.....I can not forget this till i die

nimecheka mpaka basi
 
mi nilianza na ka motorola sijakaons hapo.. mh nilikua naringaje shuleni!
 
Dah mmenikumbusha mwaka 2000 pale nikiwa hom TRM bro wangu alikua likizo DSM si akaja na cmens kidole juu, kwa wakati huo vocha ilikua ikipatikana kwa Tsh 2000, ivyo alikua akiwekewa vibandani hapo yeye alikua MWALIM MKUU shule flani pia kuangalia salio ilikua Tabu,ivyo mimi nilikua nikimtegea akiingia bafuni mi nachukua cm napiga, akija tayari mi nisha maliza, ivyo nilimtesa sana ndipo mwaka 2001 nikanunua cm kwa ada ya shule2.
 
Back
Top Bottom