mwali wa giningi
Member
- Nov 14, 2013
- 67
- 42
World Hijab Day ni siku maalum ya uhamasishaji wa vazi la hijab kwa wanawake. Binafsi naona ni alama nzuri ya kuhimiza uvaaji wa mavazi ya stara kwa wanawake, maana wengi wetu tumejisahau kabisaa. Imefikia wakati tunaenda maofisini na mavazi ya kulalia au hata yale ya kuogelea. Heshima ya mwanamke ni kujihifadhi. wanaokubaliana na mimi watoe maoni yao juu ya mavazi sahihi kwa mwanamke wa kitanzania. Karibuni