Extrovert
JF-Expert Member
- Feb 29, 2016
- 67,106
- 173,889
Wanapigaga pakiwa busy jioni ile saa 2/2 hivi magari mengi !Ndio hao hao
Wanapigaga pakiwa busy jioni ile saa 2/2 hivi magari mengi !Ndio hao hao
jana mbichii... nimeenda petro station. nikamwambia weka elfu 30, basi akaclear number akaandika 3,000... nikamwangalia tu akachomeka mpira wake mafuta yakaanza kutoka akajifanya bize akazunguka upande wa pili... mashine imeshakata yeye anajifanya bize.... akaenda funga kifunik akatoa risiti akaniletea, nikampa 30,000 akapokea na kuniambia karibu tena... akashangaa siondoki nikamwambia bado mafuta yangu hayajakamilika umeweka ya elf tatu.... bila hata kuangalia akajifanya kujichangamsha eti samahani daaa kumbe nimeandika elfu tatu.... dah... nina mawazo.... akakuta nimekunja uso namwangalia tu.... nikafungua tank akaandika 27,000 akajaza yaliyobaki..... nikaondoka bado anajichekesha mie simjibu kitu. Huu ni wizi kuweni waangalifu.
Hii nilishapigwa Segera pale kuna kakituo mshenzi😂😂😂 mafuta ya 20K sikufika nayo Mombo yameshakata halafu highway ambako gari inakula vizuri😝😝😝 matusi niliyomtukana yule mshenzi dereva wangu alikuwa anakufa mbavu maana nilisema nijazie tu ili nimalizie safari 😁 gauge ikishuka sana economy inapunguaWizi wao kwasasa ni kua na pampu ilio jikunja ndefu mafuta yanabaki kwenye pampu na anarudisha pampu vizuri tu ukiondoka anamimina kwenye dumu dogo la lita tano likija wanauzia bodaboda ndo wizi wao kwa wasasa.
Haya wanafanywa kwenye vituo ambavyo supervision sio nzuri, hao pampu attendants hawakosi 20,000 to 30,000 kwa siku hususani wanao fanya night shift wanahudumia walevi wengi na watu wakusafiri usuku.
Mimi iliwahi kunitokea,ameweka mafuta gauge yangu haikuamka ikawa inasoma zero,nikamshukia nikawasha moto vibaya kuwa hakuingiza mafuta,yule dada akasema ngoja aingize tena labda pump ina shida,wakati naondoka ilikuwa imenyanyuka kidogo sana,nikawa naondoka huku maneno yananitoka kuwa ni wezi sana wale wahudumu,ilipofika kama km 1 hivi gauge ikapanda mara mbili ya kipimo cha kwanza,nikabakia naona aibu mimi...Kuna siku nilimsingizia muhudumu hapo kaniibia mafuta kumbe gauge yangu ina tabia za ajabu. Baadae nikagundua hakuniibia ilibidi siku ingine nirudi nimuombe samahani.
Hakikisha huwi na haraka wala madoido ufikapo kituo cha kujaza gari mafuta.
Usizubaishwe na uzuri wala story za kuzuga za mhudumu...
Epuka kukodolea macho msambwanda wa mhudumu Miele yako.
Macho yako yote kwenye pump reader hakikisha kabla hujawekewa mafuta isome 0000
Kaka tatizo sisi tunaozipata kwa kuungua jua na kunyeshewa mvua tuna hasira sana, ingekuwa zinakuja kwa ulaini wala isingekuwa tatizo, ingekuwa ni kugawana neema tu, lakini sasa jinsi tuzipatavyo ni mtihani ndio maana tuna hasira sana!Hela za kutafuta kihalali hazitoshi. Ukisikia kujiongeza ndiyo huko.
Tatizo ni pale mtu unagundua kwamba pale fulani kanipiga. Wapo wanaojenga kwa pesa za sheli.
Maisha ni kupigana na kupiga ndiyo huko uonavyo
Mafuta hayawezi kuuzwa bila mashine ya risiti kurekodi. Ndo mana huwezi hata cku moja kumharibia kazi pump attendant kwa kumchongea kwa manager kwasababu manager anajua anaibiwa ni mteja sio bossKwa hesabu za haraka haraka ni kwamba: anaibiwa mwenye kituo cha mafuta kwa sbb yale mafuta yameuzwa bila mashine ya risiti kurekodi, pia anaibiwa mwenye chombo anaewekewa mafuta maana analipia mafuta ambayo hakuwekewa! Hii kwa kifupi inaitwa DOUBLE IMPACT!
Hatari na nusu.
Kwa hiyo kuna uwezekano pia wa kupewa risiti isiyo ya kwako?
Yaani ndio hivyo hivyo, na sijui ni nani aliebuni mbinu ya kuweka hawa wahudumu wa jinsi ya kike, maana akijichekesha tu unamsamehe, mimi nimeshikwa sana na hasira asubuhi, nikatamani kumpa walau kelbu mbili aamke, nikawaza jela, nikakumbuka familia yangu nikajikuta narudisha moyo nyuma!
Yaani we acha tu.... nilikuwa napigwa 27,000/ kweupeeeeeHii kipigo chake ni cha Mbwa koko 😂😂😂 usingeona yangekukuta ya Vocha za Voda 😝😝😝
... how possible is this? Kwa sababu, unless ulimkuta ile handle kaishikilia mkononi, ila ikisharudishwa mahali pake na kunyanyuliwa tena automatically ina-clear digits zote to zero. Yaani anawezaje kuanzia kiwango tofauti na zero? Naomba kuelimishwa.
... nikiingia sheli macho breki ya kwanza kwenye meter reading; nakuwa interested sana kujua aliyetangulia kanunua lita ngapi (sijui kwanini). Then nashusha kioo huwa salamu zao siitikiagi natoa order ya kiasi nachohitaji na kwa kutaja kabisa aina ya mafuta (mf. weka petroli ya elfu 30) huku macho yamekomalia kwenye reading na kuhakikisha ananyanyua handle sahihi (petro vs diesel); meter imeanzia 0000 na kaingiza kiasi sahihi.Huwa wanaitegesha tu ukija wanakupa maneno mazuri na porojo ukizubaa wanaliunga zipo sana hizo.
Sawa tajiriElfu 5 tu unalialiaaaa. We tip huwa unaacha kweli
.Hivi ni Umeandika bila kujua unachoandika na sijui hujui kweli au unafanya makusudi kupotosha ili uchangamshe jukwaa..
Wizi unaosema haupo na hakuna namna yoyote uneweza ukaibiwa Kwa staili hiyo uliyoileta .mkono wa pampu ukirudishwa kwenye mashine wakati wa kutoa unaanza zero mpaka bei uliyoset au utakapoishia
Kuibiwa ni kama ataendelea kupima bila kurudishwa mkono kwenye mashine tena ikiwa mwanzoni hakuset bei wakati anampimia mteja wa kwanza
Elfu 5 tu unalialiaaaa. We tip huwa unaacha kweli
Hapo ndio uwezo wake wa mwisho kufikiria, msamehe bure!Ukiwa shabiki wa ccm na akili zinakua mgando. Angalia ulichoandika!
Tips ilikuwa kipindi kileee, siyo sasa.Elfu 5 tu unalialiaaaa. We tip huwa unaacha kweli
Mkuu unaweza kukuta huyo jamaa ndo hao hao wezi wa hapo kituoni ndiyo maana KakomaaaNdugu yangu, naomba tutafutane, twende pamoja pale na tukawahoji walioniibia kwa style hiyo watupe uzoefu, najua yaweza kuwa ngumu kupata ushirikiano, ila nakuhakikishia mimi ntawapa hata pesa ya kula waweze kutupitisha kwenye uzoefu huo.
Mie Moro huwa najazia TOTAL pale Msamvu, hakuna janja janja kabisa...Hizo Petrol Station za ajabu ajabu huwa sijazagi mafuta labda itokee gari imenizimikia karibu na hizo sheli. Kwa sasa sheli za uhakika ni Oryx na Total zimekaa ki proffessional zaidi ila kwengine ambako napaamini ni Lake Oil!