Nyakijooga
Senior Member
- Dec 9, 2018
- 123
- 202
Aliyewahi kuwa Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka ambaye ni mtaalamu wa Uchumi na masuala ya mipango miji amesema kuwa kwa siku za hivi karibuni kumekuwepo na ukilitimba wa umiliki wa vituo vya mafuta nchini.
Akizungumza na Radio One Stereo January 24, 2024 amesema kuna watu wachache wanamiliki vituo vya mafuta karibia kila sehemu nchini, amesema kuwa hilo sio jambo baya lakini amedai kuwa inaweza kuwa kikwazo kwa watu ambao Serikali imekuwa ikitaka kujiajiri kushindwa kupiga hatua kutokana na ukiritimba huo.
Amesema kuwa ni muhimu jamii ikafahamu kuwa biashara ya mafuta nchini sio uwekezaji bali ni uchuuzi.
Prof. Tibaijuka ameongeza kuwa ipo changamoto nyingine inayotokana na vituo vya mafuta kujengwa bila kuzingatia mipango miji.
Ikumbukwe hivi karibuni baadhi ya wadau ndani ya JamiiForums wameripoti madai ya vituo vingi vya mafuta kujengwa kwenye maeneo yasiyo rasmi ikiwemo karibu na makazi ya watu hali ambayo imekuwa ikiibua mijadala inayohoji juu ya uwajibikaji kwa mamlaka zinazotoa vibali.
Akizungumza na Radio One Stereo January 24, 2024 amesema kuna watu wachache wanamiliki vituo vya mafuta karibia kila sehemu nchini, amesema kuwa hilo sio jambo baya lakini amedai kuwa inaweza kuwa kikwazo kwa watu ambao Serikali imekuwa ikitaka kujiajiri kushindwa kupiga hatua kutokana na ukiritimba huo.
Amesema kuwa ni muhimu jamii ikafahamu kuwa biashara ya mafuta nchini sio uwekezaji bali ni uchuuzi.
Prof. Tibaijuka ameongeza kuwa ipo changamoto nyingine inayotokana na vituo vya mafuta kujengwa bila kuzingatia mipango miji.
Ikumbukwe hivi karibuni baadhi ya wadau ndani ya JamiiForums wameripoti madai ya vituo vingi vya mafuta kujengwa kwenye maeneo yasiyo rasmi ikiwemo karibu na makazi ya watu hali ambayo imekuwa ikiibua mijadala inayohoji juu ya uwajibikaji kwa mamlaka zinazotoa vibali.