Wizi wa mafuta Petrol Stations

Wizi wa mafuta Petrol Stations

Nilipiga kuomba delay.niliweka elfu 26 huwa najua ya adios wapi siku zote.alianza zero lakini akiweka hewa.yalipofika elfu 18 ndiyo nikawa Nasikia yanaingia alipomaliza nikamwambia njoo Mbona fuel haijafikia kipimo akasema labda ni gari yako gage problem nikamwambia unaona hii gari ni mpya na ni digital kilakiu kinafanya kazi ni yangu wewe huijui.akasema nimeweka nikamwambia good.where is your manager akaja muarabu from next office opposite Na uchumi supermarket.nikamwambia weka fuel ya same unit elfu 26 kwenye dumu.halafu haya uliyoweka nafungua koki chini naweka kwenye ndoo yakiwa sawa nalipa zote uliyoweka kwenye gari yakiwa pungufu unaingia kwenye gari nakupeleka kawe polis kwa kosa la wizi. Kijani Akaogopa.manager akaagiza wakaweka fuel mpaka pale mshale wangu ninapojua siku zote.
Muda wangu ulienda about 2hrs lakini mpaka Leo nikienda hapo wanasema shomile amekuja muwekeeni fuel msifanye mchezo.na mimi wala sio shomile

Hakikisha unapigania haki yako usiondoke.ikiwezekana mchukue muache polisi kwa maelezo kisha mahabusi.hapo waajifunza

Mpendachapati

Tembeeni na vidumu wajameni..
 
Khaa kutembea na vidumu aibu hasa sie kina mama ila hilo la kujua kama anaingiza hewa au la ndo shida ipo. Ngoja nitafute swahiba mwenye sheli.....
 
Hivi wanaojaza mafuta kwenye genereta wanafanyaje. Labda ..
 
Kituo kimojawapo ni Engen ya mbezi makonde Kuna jamaa alinipiga buku 10 akaweka ya 20 wkt nimempa 30....ilipanda mishale miwili badala ya mi3.

Acha uongo aliwekaje 20wakati umempa 30pump za pale engen hazina ujanja wakuunganisha ukisha seti tu nakuweka zikimaliza huzima kabisa hamna shell ninayo ikubali kama engen ya mbezi beach wako vizuri jamaa kiukweli
 
Hili ni kweli, usipokuwa makini unaibiwa, angalia pampu ainze 0000 kabla hajaweka mkono kwenye tundu la tenki

kuna mmoja alituambia juzi hapo ubungo yani yeye anachukua10% hivi kila akiweka mafuta kwenye gari na pump huwa anairest inaaanza 0000.
yaani basically pale wanapokuekea mafuta huku wameshika pump handle wanaiba ile wanavyobonyeza na kuachia huwa wanabana mafuta yanarudi inaingia hewa kwahiyo mwambie muhudumu ASISHIKE PUMP aachemafuta yaingie yenyewe na wala asiweke kifuniko kwenye ile handle ya pump ategeshe ile handle yenyewe tu.( we angalia tuu mkono wake utaona wanafinya na kuachia mkono au anasimama position ambayo humwoni akiweka kutumia side mirror ili afinye pump vizuri)
Pia asiache mafuta ya kimbie haraka mara nyingi speed ya ela haendani na flow ya mafuta kwa hiyo aweke speed ndogo yaani zile tarakimu ziende taratibu sio kwa kasi. na wale walio temper na mashine yaani hawa hata uende na kidumu hawaweki utasikia tuu haturusiwi kuuza kwenye vidumu
 
Mh! Hii nchi kila mtu anajifunza wizi tuatafika kweli? Wakati mwingine akianza kukuwekea unaona hela inaenda lkn mafuta inaanza kuesabu badae. Duh hata cjui tukimbilie wapi,kuna siku ntashuka nimpasue mhudumu had ashangae. Nakerwa na wizi ile mbaya,na hizi bei mbaya za mafuta ni km tumebaki yatima bila mtetezi.
 
Haaa hii oilcom ya opposite na uchumi Segerea ni komesha. Gari yangu full tank ni elfu 60 niliwapa 40,wakaanzia 0.0 but huwez amini mshale haukupanda ukaishia robo tank. Normally huwa naweka lake oil sanene ya elfu 30 mshale unapanda had nusu tank!! Yaan hawa oil com wanamchezo mchafu na sirudi pale napaona km police station

Unatumia gari gani? Mie haka katoyo full tank lazima niache 200k,elfu 15 unapanda mshale mmoja,elfu10 hata mshale haupandi.
 
Acha uongo aliwekaje 20wakati umempa 30pump za pale engen hazina ujanja wakuunganisha ukisha seti tu nakuweka zikimaliza huzima kabisa hamna shell ninayo ikubali kama engen ya mbezi beach wako vizuri jamaa kiukweli

Ndio hivyo walinipiga,huwa nikiweka mafuta ya 30 vimshale vi3 vinapanda alivyoweka vikapanda vi2 nikaona nishaliwa Ila sijagombana nae coz Nilikuwa na family, siku nyingine nikaweka ya 30 kituo kingine vikapanda vimshale vi3 nikasema nishaconfirm kwamba engen walinipiga nikaenda pale engen nikampa 30 akaweka vikapanda vi3 maana Nilikuwa nimeangalia kwa umakini,Ile siku walinipiga kwasababu Ile kumpa hela mara akaja Dada kwa mbele kunizuga na kunipoteza maboya kwamba anaosha kioo cha mbele na mopa yake na sabuni kumbe kunipoteza maboya nisiangalie readings za pump.
 
Well kwa mujibu wa serikari ya Tanzania the right way to ensure standardization ya huduma za jamii kutoka kwenye taasisi za serikari na watu binafsi ni kutoa ahadi ya uadilifu; sasa nchi gani umewahi kuona ahadi inawekewa mwongozo wa regulations na regulator wa kusimamia standards.

Hayo mambo ayazuiliki bila ya sheria na sanctions zitakazo wafanya wahusika kuchukua hatua thabiti za usimamizi na kuhakikisha mteja au raia anapata stahiki zake halali. Sasa serikari inapoimiza standardization ya huduma kwa ahadi ya uadilifu given the social circumstances and challenge forget about the principles of ethics particularly justice, watu watafanya wajisikiavyo simple as that provided they can get away with it.
 
Nilipiga kuomba delay.niliweka elfu 26 huwa najua ya adios wapi siku zote.alianza zero lakini akiweka hewa.yalipofika elfu 18 ndiyo nikawa Nasikia yanaingia alipomaliza nikamwambia njoo Mbona fuel haijafikia kipimo akasema labda ni gari yako gage problem nikamwambia unaona hii gari ni mpya na ni digital kilakiu kinafanya kazi ni yangu wewe huijui.akasema nimeweka nikamwambia good.where is your manager akaja muarabu from next office opposite Na uchumi supermarket.nikamwambia weka fuel ya same unit elfu 26 kwenye dumu.halafu haya uliyoweka nafungua koki chini naweka kwenye ndoo yakiwa sawa nalipa zote uliyoweka kwenye gari yakiwa pungufu unaingia kwenye gari nakupeleka kawe polis kwa kosa la wizi. Kijani Akaogopa.manager akaagiza wakaweka fuel mpaka pale mshale wangu ninapojua siku zote.
Muda wangu ulienda about 2hrs lakini mpaka Leo nikienda hapo wanasema shomile amekuja muwekeeni fuel msifanye mchezo.na mimi wala sio shomile

Hakikisha unapigania haki yako usiondoke.ikiwezekana mchukue muache polisi kwa maelezo kisha mahabusi.hapo waajifunza

Mpendachapati

Mkuu, nipe maujuzi ya kujua hapa mhudumu anaweka upepo au hapa anaweka mafuta sbb huwa nashindwa kutofautisha.
 
Victoria station DSM weka mafuta yako kwa uhuru kabisa.. wale hakika ni watumishi wa Mungu.. na pump zao hazina haraka
 
oilcom ni zote!kiboko niya pale ubungo,nenda na kigaloni uone!hawaku pimii mafuta hata ungezimikiwa mt.5 kutoka kwenye pump!

Duh! Kama ndiyo hivyo inabidi tuchukue tahadhari na vituo vya mafuta vya OILCOM !
...lah! kumbe ndiyo maana wanashusha bei zao kidogo!
 
Duh hili ni janga, mafuta yenyewe bei kali halafu bado wanapiga!!
 
Mbona ni rahis display si inaonekana pale mwambie azime aanze 0 tatizo lenu wengi wakishafika station wanakuwa na shughuli nyingi mara afungue tank mara akague tairi, mara taa , na kumwacha atte pekee hapo ndip hupigwa
 
Back
Top Bottom