Sidhani kuna sehemu yeyote umeshurtishwa kusoma sasa kuchoshwa huko umechoshwaje? Au ndo nyie wa kucomment ili mradi mcomment. Just coz u have an ability to write it doesnt mean u should write even when not required to.
wewe na hao wenzio mtaendelea kuibiwa kila siku kwa style hio hio na ubwanyenye wenu! kila mara hapa hii mada inajadiliwa kuhusu aina hii ya wizi na bado mnaibiwa, ni hivi ukienda kuweka mafuta hakikisha kabla hajakuwekea inasoma zero au shuka kabisa kwenye gari hawezi kukuwekea mafuta kabla hujamwambia!
OilCom ya chini barabara ya Kawe (Karibia na Raibow) wamekithiri hii michezo
na mi hapa ndo napahitaj hasa. mana mi nilishachoka vipgo vya kuwekewa hewa hasa. nahofia hata sheria ya kutowekewa mafuta kwenye dumu ilifinyangwa kulinda wiz huu maana kama mtu kadhamiria kuchoma moto kwa mafuta hata kwenye pikipiki atafyonza.Naomba kujua.
Unajuaje kama machine inaingiza hewa na sio mafuta?
Nilipiga kuomba delay.niliweka elfu 26 huwa najua ya adios wapi siku zote.alianza zero lakini akiweka hewa.yalipofika elfu 18 ndiyo nikawa Nasikia yanaingia alipomaliza nikamwambia njoo Mbona fuel haijafikia kipimo akasema labda ni gari yako gage problem nikamwambia unaona hii gari ni mpya na ni digital kilakiu kinafanya kazi ni yangu wewe huijui.akasema nimeweka nikamwambia good.where is your manager akaja muarabu from next office opposite Na uchumi supermarket.nikamwambia weka fuel ya same unit elfu 26 kwenye dumu.halafu haya uliyoweka nafungua koki chini naweka kwenye ndoo yakiwa sawa nalipa zote uliyoweka kwenye gari yakiwa pungufu unaingia kwenye gari nakupeleka kawe polis kwa kosa la wizi. Kijani Akaogopa.manager akaagiza wakaweka fuel mpaka pale mshale wangu ninapojua siku zote.
Muda wangu ulienda about 2hrs lakini mpaka Leo nikienda hapo wanasema shomile amekuja muwekeeni fuel msifanye mchezo.na mimi wala sio shomile
Hakikisha unapigania haki yako usiondoke.ikiwezekana mchukue muache polisi kwa maelezo kisha mahabusi.hapo waajifunza
Mpendachapati
Hawaangalii hata tanki ya gari ina ujazo gani wezi watupu. unashangaa tenki la vitz linaingia lita 50 limekuwa basi hilo? cha muhimu ukifika petrol station shuka angalia pump isome zero na itoe mafuta sio hewa.
Haaa hii oilcom ya opposite na uchumi Segerea ni komesha. Gari yangu full tank ni elfu 60 niliwapa 40,wakaanzia 0.0 but huwez amini mshale haukupanda ukaishia robo tank. Normally huwa naweka lake oil sanene ya elfu 30 mshale unapanda had nusu tank!! Yaan hawa oil com wanamchezo mchafu na sirudi pale napaona km police station