Ni vizuri kupeana uzoefu hata kama ni mdogo hasa kwa mambo mabaya yanayoendelea ktk jamii yetu. Mpendwa kama unakwenda kununua mbao a.k.a treated timber hasa Buguruni na kwingineko weka akili sawa. Kuna wizi kiasi cha kukatisha tamaa. Ukiweza nenda na futi kamba yako,na ikibidi hata calculator,futi zinapopimwa na kusomwa na wewe andika,maeneo wanayopenda kuwaliza watu ni haya yafuatayo.
Moja, watakwambia mita moja(kwa sasa) ni Tsh 1600/ kwa hiyo kwa hesabu za haraka utasema futi ni 1600/3 badala ya Tsh 1600/3.3 kwa hiyo kama ni mbao nyingi hiyo 0.3 ni hela nyingi sana umeibiwa.
pili, zile futi zao wamekata pale ktkt kipande cha kati ya futi moja mpaka mbili na kukiondoa, kama hujashituka kila ubao (one pc) utakuwa umeibiwa hizo futi. Ukifika wanakupa futi kagua, kisha watazunguka zunguka mpaka wakubadirishie futi.
Tatu, wanapotaja futi na point zake,wanaongeza ktk kuandika zile point,kama huandiki wewe,basi utaibiwa hadi basi.
Nne, eneo la kujumlisha ni hatari pia, watakupeleka speed kwa lengo maalum.
Kwa upande wa mabati, kuna wahuni wanachanganya gauges, juu wanaweka 30 na ndani wanaweka 32.
Kama unataka kununua vifaa hivyo, basi usiwe na haraka kabisa.
Moja, watakwambia mita moja(kwa sasa) ni Tsh 1600/ kwa hiyo kwa hesabu za haraka utasema futi ni 1600/3 badala ya Tsh 1600/3.3 kwa hiyo kama ni mbao nyingi hiyo 0.3 ni hela nyingi sana umeibiwa.
pili, zile futi zao wamekata pale ktkt kipande cha kati ya futi moja mpaka mbili na kukiondoa, kama hujashituka kila ubao (one pc) utakuwa umeibiwa hizo futi. Ukifika wanakupa futi kagua, kisha watazunguka zunguka mpaka wakubadirishie futi.
Tatu, wanapotaja futi na point zake,wanaongeza ktk kuandika zile point,kama huandiki wewe,basi utaibiwa hadi basi.
Nne, eneo la kujumlisha ni hatari pia, watakupeleka speed kwa lengo maalum.
Kwa upande wa mabati, kuna wahuni wanachanganya gauges, juu wanaweka 30 na ndani wanaweka 32.
Kama unataka kununua vifaa hivyo, basi usiwe na haraka kabisa.