Simiyu: Mtendaji Kata afikishwa Mahakamani kwa Wizi wa Tsh. 1,628,000

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,119
Afisa Mtendaji wa Kata ya Sagata katika Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Solomom Dunga Mbise, amefikishwa Mahakamani kwa mashtaka 4 ikiwemo Wizi wa Tsh. Milioni 1.62, Ubadhirifu na Ufujaji, Matumizi Mabaya ya Madaraka na Kuisababishia Serikali Hasara.

Katika Kesi ya Msingi, mtuhumiwa akijua ni Mtumishi wa Umma, anadaiwa kufanya Wizi kwa kukusanya fedha za mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Itilima kwa kutumia mashine za Point Of Sale (POS).

Mshtakiwa alikana makosa yote na kuomba mazungumzo ya 'Plea Bargaining' katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambapo Kesi imeahirishwa hadi Februari 19, 2024 ili aweze kukamilisha hatua hizo.
 
Hii nchi maigizo ni mengi sanaaa.. unaweza kukuta aliyemshitaki huyu mtendaji kwa kuiba 1m alishawahi kuiba 200m na nyingine nyingiii na hajawahi kukamatwa, inawezekana kabisaa amemshitaki kwasababu labda dill ilikua yake mtendaji akamuwahi. Yani hii nchi kuna watu wameiba billions of money bt wanaitwa waheshimiwa, maskini huyu ka milioni kamoja kamamtia matatizoni.... Hii ndo Tanzania
 
Wezi wa mabilioni wanaendeshwa kwenye V8 NYEUSI zenye plate no za kipekee 🤣🤣🤣
 
Alichokikosea ni kukusanya mapato ya Halmashauri na kula badala ya kuyaweka kwenye akaunti ya Halmashauri husika.

Halmashauri za Wilaya zinakunya fedha nyingi sana.

Inasikitisha kuona Mtendaji Kata anakula 1.6 milioni mali ya Serikali wakati hiyo pesa angeweza kuipata kwa njia nyingine halali.

Kwenye POS mashine hela ikishatolewa risiti ni lazima iende benki hakuna mjadala.

Ni wapumbavu na wajinga tu watafunguliwa kesi kwa kula hela za mapato.
 
Back
Top Bottom