DOKEZO Kero: Askari trafiki wa Buguruni Sheli na Tazara wanatengeneza foleni kwa manufaa yao

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,275
18,352
Habari wanabodi

Naomba niingie kwenye mada, kama ni mtumiaji wa barabara ya Mandela na mfuatiliaji wa mambo nyakati za jioni utagundua kuna jambo la kutengeneza.

Iko hivi, wakati unatoka Ubungo kwenda Tazara au kinyume chake, mara nyingi utakuta foleni imeanzia mbali sana hata Mwananchi, utasogea kidogo kidogo hadi Njia Panda Tabata na Buguruni Sheli kwa shida sana.

Sasa katika ufuatiliaji wangu nimebaini jambo kwa hawa askari trafiki, ikifika jioni wanajua magari ni mengi kwa sababu watu wanatoka makazini, askari wanajazana mitaa ya Buguruni Sheli hadi maeneo ya darajani wakisubiri gari linalotanua.

Kwa bahati mbaya daladala ndio hutanua sana kupita service road wanazikamata na kula chao ukibisha unaandikiwa. Fedha inayotolewa ni kuanzia Tsh.2,000 hadi 5,000. Kwa gari binafsi mtu anatoa hadi 10K kupunguza kucheleweshwa zaidi.

Kingine nilichobaini hawa askari wa Buguruni sheli wanaongea na Askari wa Tazara (Mfugale flyover) ili magari ya Mandela road yasiitwe badala yake wanaitwa magari ya Nyerere road kwenda au kutoka City center, na askari wa Buguruni wanaita zaidi magari yanayoelekea au kutoka Tabata na mengine yanayoenda au kutoka Ilala.

Huu mchezo inahitaji ufuatiliaji sana mpaka kuubaini kwa sababu ukifanikiwa kuvuka njia panda ya Tabata unakuta huku mbele kati ya Buguruni na Tazara ni kweupe na magari yanayokatiza sio mengi ni ya kuhesabu.

Sasa niziombe Mamlaka zinazosimamia hawa jamaa ziwaambie waache kutunyanyasa na wafanye kazi kwa haki, hii nchi ni yetu sote na tunalipa kodi.

Kila mmoja anayo njaa kwa kipimo chake lakini wasitufanyie hivi wanatuonea sana na wakati mwingine mtu una emergency lakini jamaa wanafanya kusudi wanakuweka wakijua kabisa ukishindwa kuvumilia utatanua service road watakukamata walambe chao.


Asanteni.
 
Township panataka Akilihood

Maisha haya kila mtu anatakiwa kujiongeza ila huku mikoani hamna foleni

Karibuni
 
Habari wanabodi

Naomba niingie kwenye mada, kama ni mtumiaji wa barabara ya Mandela na mfuatiliaji wa mambo nyakati za jioni utagundua kuna jambo la kutengeneza.

Iko hivi, wakati unatoka Ubungo kwenda Tazara au kinyume chake, mara nyingi utakuta foleni imeanzia mbali sana hata Mwananchi, utasogea kidogo kidogo hadi Njia Panda Tabata na Buguruni Sheli kwa shida sana.

Sasa katika ufuatiliaji wangu nimebaini jambo kwa hawa askari trafiki, ikifika jioni wanajua magari ni mengi kwa sababu watu wanatoka makazini, askari wanajazana mitaa ya Buguruni Sheli hadi maeneo ya darajani wakisubiri gari linalotanua.

Kwa bahati mbaya daladala ndio hutanua sana kupita service road wanazikamata na kula chao ukibisha unaandikiwa. Fedha inayotolewa ni kuanzia Tsh.2,000 hadi 5,000. Kwa gari binafsi mtu anatoa hadi 10K kupunguza kucheleweshwa zaidi.

Kingine nilichobaini hawa askari wa Buguruni sheli wanaongea na Askari wa Tazara (Mfugale flyover) ili magari ya Mandela road yasiitwe badala yake wanaitwa magari ya Nyerere road kwenda au kutoka City center, na askari wa Buguruni wanaita zaidi magari yanayoelekea au kutoka Tabata na mengine yanayoenda au kutoka Ilala.

Huu mchezo inahitaji ufuatiliaji sana mpaka kuubaini kwa sababu ukifanikiwa kuvuka njia panda ya Tabata unakuta huku mbele kati ya Buguruni na Tazara ni kweupe na magari yanayokatiza sio mengi ni ya kuhesabu.

Sasa niziombe Mamlaka zinazosimamia hawa jamaa ziwaambie waache kutunyanyasa na wafanye kazi kwa haki, hii nchi ni yetu sote na tunalipa kodi.

Kila mmoja anayo njaa kwa kipimo chake lakini wasitufanyie hivi wanatuonea sana na wakati mwingine mtu una emergency lakini jamaa wanafanya kusudi wanakuweka wakijua kabisa ukishindwa kuvumilia utatanua service road watakukamata walambe chao.


Asanteni.
wanalazimika kifanya ivo ili kupata hela ya mchezo kuna askari wengine kila siku elfu50, 70, laki hadi laki 2 ndio maana pale buguruni wanakuepo had saa4 usiku.

Makumbusho ni kila siku Asubuhi kila basi linaloingia Makumbusho kutokea mwananyamala Lazima akakabizi elfu5 kwa askari. By saa4 hukuti askari hadi kesho Asubuhi tena
 
Nelson Mandela Road, Foleni ya asubuhi na jioni inafanya njia iwe mbaya na yenye kukwamisha mambo mengi kwenye maroli.

Jioni na Asubuhi gari ikipima mzani wa Kurasini Tanroad ikianza Safari ya Kupita Uhasibu,Taifa,Sokota,Tazara,Buguruni,Tabata mpaka Ubungo gari inatumia zaidi ya Masaa mawili. Kiuchumi ni hasara sana gari umbali usiozidi 20km kutumia masaa zaidi ya 2.

Nelson Mandela Road ndio kiini cha mizigo yote ya transit lakini haiangaliwi foleni za malori. Ni hata wageni wanaokuja kuchukua na kupitisha mizigo wakitumia kipande hiki huwa wanachoka sana njia ina foleni kero.
 
Mkuu bado hujaonyesha sababu ya wao kupendelea baadhi ya uelekeo na kubania uelekeo mwingine!.


USHAURI WANGU

Kwenye hii nchi ukiwa na Akili timamu utaishi kwa taabu sana,wanaoifurahia nchi ni mazezeta kama kina Mwijaku na wenzie!


Lakini hii njia inapaswa ipanuliwe na ijengwe Under Ground Roads kutokea Tabata Mataa ikaibukie kule Veterinary,hii itaondoa kabisa tatizo la foleni pale,ukisema ijengwe fly over itakuwa ngumu kwasababu walichelewa na fly over ya SGR ikapita!,Hivyo Suluhisho la Pale ni

1.Under Ground Road kutoka Tabata Mataa hadi Veterinary

2.Pale Buguruni Mataa pajengwe fly over

Tofauti na hapo Vilio vya pale havitokaa viishe!
 
Wanatengeneza foleni ,ukitanua tu
Unakutana nao ,lazima wakutoe pesa

Ova
 
Duuh. Inasikitisha sana. Askari trafiki wanafanya michezo ya kupokea rushwa hadharani kwa sababu wanajua hawachukuliwi hatua yeyote. Walipata hofu kipindi cha NYERERE na anko MAGU
 
Duuh. Inasikitisha sana. Askari trafiki wanafanya michezo ya kupokea rushwa hadharani kwa sababu wanajua hawachukuliwi hatua yeyote. Walipata hofu kipindi cha NYERERE na anko MAGU
Nchi iko vagarant

Rushwa uwizi unafanyika juu

Ndomana wa chini nao wameamua

Kujiongeza nao.....

Ova
 
Habari wanabodi

Naomba niingie kwenye mada, kama ni mtumiaji wa barabara ya Mandela na mfuatiliaji wa mambo nyakati za jioni utagundua kuna jambo la kutengeneza.

Iko hivi, wakati unatoka Ubungo kwenda Tazara au kinyume chake, mara nyingi utakuta foleni imeanzia mbali sana hata Mwananchi, utasogea kidogo kidogo hadi Njia Panda Tabata na Buguruni Sheli kwa shida sana.

Sasa katika ufuatiliaji wangu nimebaini jambo kwa hawa askari trafiki, ikifika jioni wanajua magari ni mengi kwa sababu watu wanatoka makazini, askari wanajazana mitaa ya Buguruni Sheli hadi maeneo ya darajani wakisubiri gari linalotanua.

Kwa bahati mbaya daladala ndio hutanua sana kupita service road wanazikamata na kula chao ukibisha unaandikiwa. Fedha inayotolewa ni kuanzia Tsh.2,000 hadi 5,000. Kwa gari binafsi mtu anatoa hadi 10K kupunguza kucheleweshwa zaidi.

Kingine nilichobaini hawa askari wa Buguruni sheli wanaongea na Askari wa Tazara (Mfugale flyover) ili magari ya Mandela road yasiitwe badala yake wanaitwa magari ya Nyerere road kwenda au kutoka City center, na askari wa Buguruni wanaita zaidi magari yanayoelekea au kutoka Tabata na mengine yanayoenda au kutoka Ilala.

Huu mchezo inahitaji ufuatiliaji sana mpaka kuubaini kwa sababu ukifanikiwa kuvuka njia panda ya Tabata unakuta huku mbele kati ya Buguruni na Tazara ni kweupe na magari yanayokatiza sio mengi ni ya kuhesabu.

Sasa niziombe Mamlaka zinazosimamia hawa jamaa ziwaambie waache kutunyanyasa na wafanye kazi kwa haki, hii nchi ni yetu sote na tunalipa kodi.

Kila mmoja anayo njaa kwa kipimo chake lakini wasitufanyie hivi wanatuonea sana na wakati mwingine mtu una emergency lakini jamaa wanafanya kusudi wanakuweka wakijua kabisa ukishindwa kuvumilia utatanua service road watakukamata walambe chao.


Asanteni.
Makamu mwenyekiti CCM aliagiza matrafiki wasiwe kero.

IGP Wambura amemjibu kwa kuongeza kero maradufu.

CCM imepoteza mvuto
 
Duuh. Inasikitisha sana. Askari trafiki wanafanya michezo ya kupokea rushwa hadharani kwa sababu wanajua hawachukuliwi hatua yeyote. Walipata hofu kipindi cha NYERERE na anko MAGU
Huyo anko wako MAGU alizidi kuwaongezea kiburi, sio hofu. Alisema hii ni pesa ya kiwi tu kwa ajili ya kubrashia viatu.
 
wanalazimika kifanya ivo ili kupata hela ya mchezo kuna askari wengine kila siku elfu50, 70, laki hadi laki 2 ndio maana pale buguruni wanakuepo had saa4 usiku.

Makumbusho ni kila siku Asubuhi kila basi linaloingia Makumbusho kutokea mwananyamala Lazima akakabizi elfu5 kwa askari. By saa4 hukuti askari hadi kesho Asubuhi tena
Hata Tegeta hivyo hivyo, asubuhi wamelundikana kama nzige, saa tatu, nne huwaoni wameshaondoka, maana "wameshashiba"! Washenzi sana hawa!
 
Mkuu bado hujaonyesha sababu ya wao kupendelea baadhi ya uelekeo na kubania uelekeo mwingine!.


USHAURI WANGU

Kwenye hii nchi ukiwa na Akili timamu utaishi kwa taabu sana,wanaoifurahia nchi ni mazezeta kama kina Mwijaku na wenzie!


Lakini hii njia inapaswa ipanuliwe na ijengwe Under Ground Roads kutokea Tabata Mataa ikaibukie kule Veterinary,hii itaondoa kabisa tatizo la foleni pale,ukisema ijengwe fly over itakuwa ngumu kwasababu walichelewa na fly over ya SGR ikapita!,Hivyo Suluhisho la Pale ni

1.Under Ground Road kutoka Tabata Mataa hadi Veterinary

2.Pale Buguruni Mataa pajengwe fly over

Tofauti na hapo Vilio vya pale havitokaa viishe!
Hizo pesa ziko wapi wakati wahusika wanapiga hela zote kwa urefu wa kamba zao? Au mwenzetu husomi hata ripoti za CAG?
 
Habari wanabodi

Naomba niingie kwenye mada, kama ni mtumiaji wa barabara ya Mandela na mfuatiliaji wa mambo nyakati za jioni utagundua kuna jambo la kutengeneza.

Iko hivi, wakati unatoka Ubungo kwenda Tazara au kinyume chake, mara nyingi utakuta foleni imeanzia mbali sana hata Mwananchi, utasogea kidogo kidogo hadi Njia Panda Tabata na Buguruni Sheli kwa shida sana.

Sasa katika ufuatiliaji wangu nimebaini jambo kwa hawa askari trafiki, ikifika jioni wanajua magari ni mengi kwa sababu watu wanatoka makazini, askari wanajazana mitaa ya Buguruni Sheli hadi maeneo ya darajani wakisubiri gari linalotanua.

Kwa bahati mbaya daladala ndio hutanua sana kupita service road wanazikamata na kula chao ukibisha unaandikiwa. Fedha inayotolewa ni kuanzia Tsh.2,000 hadi 5,000. Kwa gari binafsi mtu anatoa hadi 10K kupunguza kucheleweshwa zaidi.

Kingine nilichobaini hawa askari wa Buguruni sheli wanaongea na Askari wa Tazara (Mfugale flyover) ili magari ya Mandela road yasiitwe badala yake wanaitwa magari ya Nyerere road kwenda au kutoka City center, na askari wa Buguruni wanaita zaidi magari yanayoelekea au kutoka Tabata na mengine yanayoenda au kutoka Ilala.

Huu mchezo inahitaji ufuatiliaji sana mpaka kuubaini kwa sababu ukifanikiwa kuvuka njia panda ya Tabata unakuta huku mbele kati ya Buguruni na Tazara ni kweupe na magari yanayokatiza sio mengi ni ya kuhesabu.

Sasa niziombe Mamlaka zinazosimamia hawa jamaa ziwaambie waache kutunyanyasa na wafanye kazi kwa haki, hii nchi ni yetu sote na tunalipa kodi.

Kila mmoja anayo njaa kwa kipimo chake lakini wasitufanyie hivi wanatuonea sana na wakati mwingine mtu una emergency lakini jamaa wanafanya kusudi wanakuweka wakijua kabisa ukishindwa kuvumilia utatanua service road watakukamata walambe chao.


Asanteni.
Mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake.
 
Wakati mwingine utadhani wako vitani
Kuna siku nilikuwa nina dharura bodaboda hakuwa na helmet ya pili kwenye junction ya TAZARA imagine TRAFIKI wenye kijani alimfukuza boda boda naye kwa woga akakimbia kuelekea alikotoka hii ilikuwa ni HATARI sana.
Nashauri kufungwe CCTV za kufuatilia vitendo vinavyodhalilisha JESHI LETU.
 
Hapo ni shida, haswa Buguruni, service road wakikukamata wanadai eti unaendesha gari kwenye njia ya waenda kwa miguu!!! Yaani askari hajui hata maana ya service road, na anasema eti ni foot path akikuandikia fine. wapuuzi sana, Iko siku traffic alinisimamisha nikiwahi matibabu hospital ya Amana, akaniambia kama hauna cha kutoa unakula chuma (fine) maelezo yangu yakawa ni bure na akaandika namba ya gari siku ya pili fine naiona kupitia mtandao. Sio sawa kabisa wanavyofanya, wanachagua na kubagua madereva wa kukamata. Serikali iwapeleke mafunzo, service road sio foot path!!
 
Back
Top Bottom