Wizi wa Bank ya CRDB

Wizi wa Bank ya CRDB

Status
Not open for further replies.
Ndugu wana JF!

Je mnajua jinsi Bank inayosikiliza "CRDB" inavyoibia wateja wake? Fikiria kila ukitoa pesa kwenye ATM wanakata shs. 700.00. Wanasema kwa siku unaweza kutoa shs. 1,000,000.00. Lakini huwezi kutoa hiyo million moja mara moja utatoa mara tatu na kila ukitoa unakatwa shs. 700/=, kwa ujumla utakatwa shs. 2,100/=, hizo ni hela nyingi sana.

Na ujue kila mwezi unakatwa shs 1,500/= kama reja fee. Sasa huu ni wizi kama ule wa ESCROW.

Watanzania tuamke na tukatae wizi wa mchana mchana.

Naomba kuwasilisha!

Kama unaona kuweka hela benki ni gharama weka ndani kwako tuje tuzichukue mchana kweupe.
 
Kimbembe kingine ni SIM Banking, kuna makato ya 200 kila ukitaka kujua salio ama ukiingia tu huko

Hapo ndo nachoka kabisa eti simu isipokuwa na hela huangalii salio wakati nmb mobile hata simu ikiwa empty bado salio unachek
 
Benki sio charity nyie makauzu. Wekeni hela kwenye mtungi basi.
 
acha upoyoyo!! unataka upewe huduma bure!!? nani wa kukuwekea pesa zako bure? ATM zinafanya kazi bila gharama!!!? katoe pesa zako uweke kwenye kibubu!

Unaweza kujifanya unajua lakn wewe ndo ----- na poyoyo kuliko wote.Mtoa mada hakusema watoe huduma bure.Fairnes ktk biashara ni jambo muhimu sana.Tozo km n kubwa kwa malengo ya kulazimisha faida kubwa mwisho wa mwaka huo ndo upoyoyo na wizi.Km inaruhusiwa kutoa mlıon kwa siku,ya nn iwe vpandevpande.Unaonyesha udhaifu mkubwa kiakili pale unaposema akatoe pesa zake aziweke kwenye kibubu.Elewa CRDB ipo kuhudumia umma na wewe km unafanya kaz hapo usijione ndo mwenye CRDB.
 
Unaweza kujifanya unajua lakn wewe ndo ----- na poyoyo kuliko wote.Mtoa mada hakusema watoe huduma bure.Fairnes ktk biashara ni jambo muhimu sana.Tozo km n kubwa kwa malengo ya kulazimisha faida kubwa mwisho wa mwaka huo ndo upoyoyo na wizi.Km inaruhusiwa kutoa mlıon kwa siku,ya nn iwe vpandevpande.Unaonyesha udhaifu mkubwa kiakili pale unaposema akatoe pesa zake aziweke kwenye kibubu.Elewa CRDB ipo kuhudumia umma na wewe km unafanya kaz hapo usijione ndo mwenye CRDB.
povu lote hilo hamna cha maana umesema! hiyo pesa inakatwa ni ndogo tu. kama mnaona ni kubwa, ilinganisheni na nyingine.
 
CRDB ukiangalia salio tu simbanking, wanakata, lakini NMB-mobile sijaona haya mambo. Kweli watanzania tunanyonywa.


Anayekata vocha ni mtandao wa simu, cjajua kama CRDB wanamiliki ntandao wa simu!! Ila ukita kumtumia mtu Meseji, kama mama yako, crdb, tcra, ....kooote unataka unayemtumia Meseji usikatwe?? Haijakaa saw a, mkuu ukitumia simu lazima Vodacom au AIRTEL watakutoza , iyo sio watu wa benki ni mtandao
 
Hapo ndo nachoka kabisa eti simu isipokuwa na hela huangalii salio wakati nmb mobile hata simu ikiwa empty bado salio unachek

suala la simu kutokuweza kutumia simbanking kama hamna salio sio tatizo la benki, ni suala la mtandao wenyewe. kwa mfano kununua luku tigopesa ni bure ila mpesa ina makato.
 
Hawa jamaa wezi kabisa na nilimalizana nao kitambo.

Niliweka serving ya vijipesa vyangu wao kumbe kila mwezi wanakwangua tu kujipatia faida za lazima.

Umeona wapi serving account inakatwa makato kila mwezi badala ya kupata faida.

Hawa jamaa pumbavu sana hawana maana kabisa. Mijizi mikubwa
 
Aisee tengeneza likibubu weka mkwanja wako lisukume uvunguni hizo pesa haztakatwa hata mia
 
Anayekata vocha ni mtandao wa simu, cjajua kama CRDB wanamiliki ntandao wa simu!! Ila ukita kumtumia mtu Meseji, kama mama yako, crdb, tcra, ....kooote unataka unayemtumia Meseji usikatwe?? Haijakaa saw a, mkuu ukitumia simu lazima Vodacom au AIRTEL watakutoza , iyo sio watu wa benki ni mtandao

Mkuu we inaonekana ndo wahusika,

Inakuwaje hao makampuni ya simu wadikukate ukitumia NMB? Sijajua unataka kujenga hoja gani hapa.

CRDB nawapenda sana kwa huduma nzuri na haraka, ila makato wamezidi, mtu unaangalia tu kama mshahara umeingia lazima uwe na mia mbili kwenye simu, kweli tutafika? Ukitoa hela ndo usoseme kwenye ATM, na mtandao wao unavosumbua ikifika sa 12 majanga, utafikiri unakopa kumbe za kwako.

Mkuu Kimei!! Tuhurumie kwa kupunguza makato, kwann usiige NMB?
 
Km vp kaishi km wazee wetu zamani kachimbe shimo ndani mwako uwe unafukia hapo hamna makato kaka kila muda no makato.
 
Bank charges sawa, lakini mbona kila siku wanapandisha tena bila kumjulisha mteja.

Hivi nani huwamonitor hawa bankers. Tunajua EWURA, BRELA, SUMATRA,CRB et al wanamonitor wadau wao. Hata kama BOT wanaratibu ila naamini siyo kiivyo hasa inapokuja suala la charges kwa wateja
 
Mtoa maada naomba unisaidie kitu weka makato ya bank nyingine hapa ili tuweze kuringanisha wapi pana nafuu ila haya masuala ya watu kulalamika wakati hatuna uchunguzi wa kutosha nadhani si sawa.Na unaposema makato ni makubwa ina maana umeringanisha na sehemu nyingine sasa tuwekee na hizo bank nyingine.Mind you kila bank kuna sehemu inayombana mteja wake
 
Wabongo mfumo wa ujamaa umetuharibu kweli.. Kama ukitoa milioni kwenye Mpesa unakatwa TShs. 7,000/= unaona kukatwa TShs. 2,100/= kwa ajili ya huduma ya ATM ni wizi kweli..?

Msamehe bure. Ndiko anakopitishia pesa ya boom
 
Ndugu wana JF!

Je mnajua jinsi Bank inayosikiliza "CRDB" inavyoibia wateja wake? Fikiria kila ukitoa pesa kwenye ATM wanakata shs. 700.00. Wanasema kwa siku unaweza kutoa shs. 1,000,000.00. Lakini huwezi kutoa hiyo million moja mara moja utatoa mara tatu na kila ukitoa unakatwa shs. 700/=, kwa ujumla utakatwa shs. 2,100/=, hizo ni hela nyingi sana.

Na ujue kila mwezi unakatwa shs 1,500/= kama reja fee. Sasa huu ni wizi kama ule wa ESCROW.

Watanzania tuamke na tukatae wizi wa mchana mchana.

Naomba kuwasilisha!

Si hivyo tu pia kuangalia salio pale counter wanakata 500
"Ulipo tupo"
 
nilikuwa na akaunti 3 nafunga 2 nibaki na moja tu
siwezi kuibiwa waziwazi ivi
 
mnatakiwa kuwa feya kwa wateja wenu
sio kuwakamua tu kisa awana pa kutunzia
poor business strategy

Business strategic kiukweli kwa mabank mengi ya TZ ni poor sababu wanategemea bank charges kama main source ya income yao kitu ambacho siyooo kabisaa for me what I knew main source ya bank income ni mikopo
...$$$$...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom