Wizi wa aina mpya ukiwa Kariakoo

Wizi wa aina mpya ukiwa Kariakoo

Habari zenu wanajamvi!

Dhumuni la uzi huu ni kutoa taarifa ya tahadhari muwapo maeneo ya Kariakoo mitaa ya Agrey na msimbazi au Agrey yote! Jana baada ya yakutoka katika mizunguko yangu mida ya saa kumi za jioni! Nilipitia maeneo hayo na wadada fulani wawili niliowapa lift wakaniomba niwashushe kuna kitu walikua wanahitaji maeneo hayo!

Sasa baada ya kuwashusha kusogea mbele kidogo nikasikia jamaa akiniita kunieleza kua naitwa ile kugeuka kutizama tu kushoto kwangu jamaa mwengine akaingiza kichwa na kuchomoa simu yangu aina ya s8 galaxy iliokuepo kwenye charge! Kumbe kufunga vioo pia inasaidia sana kupunguza wahalifu kufanya yao!kwahiyo hapa nilipo maumivu yangu ni makali mnoo!hata kazini sijakwenda kwa maumivu ya jana!!

so nawapa angalizo muwapo maeneo hayo!!
wizi ni wazamani ila wamempata mshamba mpya
 
pole sana kaka, wanao kubeza hayajawakuta!yaweza kuwa wengine ni wizi wa siku nyingi ila kwa ambaye hakuwa anaufahamu kama nilivyo mimi ni mpya!asante kwa kutukumbusha kuongeza umakini tuwapo maeneo hayo bila kujali tupo kwenye daladala au private car!!by the way hata daladala wakati fulani huwa ni private!!
 
Kingufunga vioo na milango pia ukigongewa usifungue kioo karikoo wana wizi wa kila aina usalama wa simu yako ni kuweka pembeni ya mlango yaani wasione wakiiona tu watafanya kila njia waikwapue
 
Wizi huu hautuhusu tusio na magari,halafu si wizi mpya huu hapa mjini labda kwako mkuu.... Hata hivyo pole sana.
 
Bado Kuna watu ambao Bado mnatoa lift kwa watu msiowajua jaman,kufunga vioo huwa ni muhimu Sana kwa usalama,usaf na kero za nje ya gari
 
Pole sana mkuu!! hata mimi nilishuhudia mtu ameibiwa mbele ya macho yangu!! juzi juzi tu, actually hua wanakua more than 2 people then m1 anakuja upande wa dereva mwingine upande wa abiria so ukiconcetrate na ambae yupo upande wa dereva yule wa upande wa pili anakuibia!!
 
Back
Top Bottom