Wizara zinazofutwa hadharani

Wizara zinazofutwa hadharani

tumpe muda sidhani kama ni busara kumpamba wakati uchumi wetu uko hoi ngoja miaka miwili ndipo tutoe tathimini maana hata akina Kikwete walianza vizuri sana na tukawpa sifa mwishowe hata rafiki wakaribu walimkimbia
Ni kweli.
Hadi Mtumishi mmoja wa Mungu alidiriki kutamka kuwa JK ni chaguo la Mungu.
Lakini namna mzee wa Msoga alivyomalizia kipindi chake cha miaka 10, naamini hata yule mtumishi wa Mungu, ambaye mara tu baada ya kutoa tamko lile alihamishwa kituo cha kazi kutoka Dar na kwenda Bukoba,naamini kuwa Mtumishi yule atakuwa ali-regret sana kutoa matamshi yale ambayo inawezekana hata yeye mwenyewe ali-realize baadaye kuwa maono yale 'hakufunuliwa' na Mungu wetu tunayemfahamu aliye juu.
 
Watendaji waliokuwa waajiriwa wa wizara hizo itakuwaje??? Najaribu tu kupiga picha ya kitakachojiri. Mfano mtu aliye Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo...sijui atapelekwa Idara ya Habari Maelezo, ama BMT ama Idara ya Utamaduni huko Halmashauri??? Wale wa Mazingira pale kwa Makamu wa Rais nao vipi????

Japo kuna tija katika kuzipunguza ila kwa watumishi walioko katika hizo Wizara nadhani matumbo joto.
 
Ni vyema pia akafuta baadhi ya idara na wakala wa Serikali ama zingine akaziunganisha kwa pamoja.Pia nashauri angefuta cheo cha Mkuu wa Wilaya ili Wakurugenzi wa Halmashauri wakapewa meno na nguvu zaidi.Sambamba na hili Watendaji wa Vijiji na Mitaa wangelipewa meno na uwezeshaji zaidi kwa kuwa kuanzia kwao ndio Maendeleo yanapatikana...Nakubali kukosolewa.
 
aweke mawaziri wataalam kwa wizara husika,atuondolee na manaibu mawaziri makatibu wakuu wanatosha coz ndio watendaji
 
Kama hautakuwa moto wa mabua basi idadi kubwa ya baa zitafungwa pamoja na uimara wa familia kwa kupungua nguvu za nyumba ndogo!
 
THE PUBLIC HEALTH ACT, 2009

Hii ni sheria ya kupambana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindu pindu na haya ndio majukumu wa wizara ya afya

4.-(1) The Minister shall promote, preserve and maintain acomprehensive, functional and sustainable public health system inMainland Tanzania for the pUrpose of -(a) securing improvement in the health habits and lifestyles ofpeople living in Tanzania;(b) securing environmental sanitation and hygiene;(c) preventing and controlling living infectious or communicableand other diseases; and(d) providing guidance to the Authority and other authorities inregard to matters affecting public health.

Haya ni majukumu ya regulator

5. Every Authority shall-(a) take lawful, necessary and reasonable measures to preventthe occurrence of or deal with any out-break or prevalenceof any infectious or communicable and non-communicabledisease;(b) cause an appropriate Environmental Health ImpactAssessment Study to be conducted for all activities as maybe provided for under the Environmental Management Act;(c) safeguard and promote the public health standards;(d) issue notices for rectification of any breach of public healthstandards;(e) implement and enforce public health standards through bylaws;(f) promote public health standards in its area through creationof awareness and educational campaigns;(g) carry out inspections; and(h) exercise the powers or perform duties in respect of the publichealth in accordance with this Act or any other written law.

Hapo wizarani pia wana kitengo cha quality management; bado unataka kuniambia uzembe wa chini ni tatizo wakati wazi jamaa wanapwaya kwenye nafasi zao sio kwamba awaoni waendesha masoko ni machafu, TFDA inatoa vibali ya biashara ya vyakula vinavyouzwa sehemu chafu and all the nonsese wanazofanya huko juu.

Afadhali basi wangeseme wanakwama kutokana na resources zao. Lakini unapopewa majukumu wewe ndio unatakiwa uwe na mikakati ya kufikia malengi usitafute sababu; vitu vya ajabu hivi halafu juzi katibu mkuu wa wizara ya afya anajifanya anahamasisha usafi huu usani sasa umezidi na lawama wanataka kuwatupia wasio na sauti pia kisa wao ndio washauri wa kisera; the problem is at the top not the botton those are just outcome of poor management to implement government strategies.

Tazama hili sakata na sheria husika



Hiyo jana katibu mkuu wa wizara baada ya tamko la raisi hapo sasa anatafuta mchawi kwa makosa yao wao wenyewe



Hali halisi ya kila siku kwa mtanzania na afya, sio hapo tu mahala kibao watu wanaishi na health hazards au ufisadi na sheria zipo. Ata sheria ya manunuzi sio tatizo bali wasimamizi wa sheria yenyewe na management issues tu ukisoma mwongozo wake.

Sasa yanapotokea matatizo utasikia muhusika mkuu anapita nakuanza kulaumu watu wa chini. Hila hakuna wakuwauliza wao hiko wapi procedure framework ya sheria husika kusimamia usafi kutoka wizarani (au ata manunuzi ya serikari), system ya usafi ikoje na procedue zake, nani anajukumu lipi kuanzia serikari za mitaa na wamepewa expectations zipi na wizara, nani anakagua mazingira ya usafi kama sheria inavyotaka na kwa muda upi kuhakikisha sheria inafikia malengo.

Likitokea sakata au ugonjwa anatafutwa mchawi ndio utasikia mkuu wa mtaa au serikari za mitaa sijui manispaa wanapewa lawama; wakati hakuna framework ya wizara inayotoa mwongozo au TFDA kuhusu usafi, afya na usimamizi wake in the first place as part of standardization of the policy procedures anywhere; matokeo yake ndio haya.

Management Tanzania ni tatizo kwa sasa kufuta wizara ya raisi na utawala bora kabla ya kutatua tatizo sugu itakuwa ni makosa makubwa sana uzembe umezidi kila sehemu na sheria zipo. Wakishafanya uzembe wahusika kinachofuata ni kutafuta wanyonge kwa kushindwa kutimiza wajibu wao, raisi anatakiwa kujua all the time uzembe unapotokea taratibu zikoje na chanzo kiko wapi watu wapewe adhabu stahiki.

Isitoshe uzembe mwingine unaenda kuongeza nyongeza ya utoaji wa huduma ambapo gharama zake zingeweza kwepeka kabisa kama hilo tatizo la Magu wakati sheria hiko wazi nini kilitakiwa kifanyike ili hayo mambo yasitokee kabisa na waliopewa hayo majukumu wanajulikana kisheria.
 
Last edited by a moderator:
Uzuri mawizara hayana issue wala hayana sheria ya kuyaanzisha kama zilivyo idara, mamlaka, mikoa, wilaya na wakala za serikali. It's just by the President's pleasure that ministries are established and, in the same means, can be dissolved without any query or issue.

Sina uhakika na maidara lakini mikoa na wilaya ni maamuzi tu ya raisi na pm wake. Mi nafikiri asiishie hapo tu, ukweli hata lengo la kuanzisha mikoa kama Geita, Njombe, Katavi binafsi naona haikufanywa kwasababu ya kumsaidia mwananchi, ilifanywa ili tu kuasaidia washkaji tu, naishi kwenye mkoa mpya mmoja wapo, kipya nilichokiona na magari mapya ya serikali lakini usaidizi hasa kwangu kama Mtanzania sijaona. Napendekeza nayo aipunguze tu.
 
Napendekeza Venance Mwamoto awe waziri wa michezo!

Kwenye orodha ya wizara zake na ya michezo IPO? Jamaa ni kama sio fun sana wa michezo, ni kama Mkapa na Nyerere tu.
Binafsi nina amini hivi, ili tupige hatua kwenye sekta ya michezo tunatakiwa kuzifanya hizo instutions za michezo kua very strong, TFF, BMT, BFT nk. Alikuwepo waziri wa michezo mnazi kweli wa Simba (Juma Athuman Kapuya) lakini hatukupiga hatua yoyote zaidi ya kushuhudia mgogoro mkubwa ndani ya FAT (sasa TFF)
 
Mfano bunge la bajet ck zake zitapungua. Hata kipindi cha maswali na majibu nacho mda wake utapungua. Bado ucseme ile bajet ya kila wizara
 
Yaan sijui kwa nini kila nikimkumbuka jamaa aliyepita huwa najisikia hata kutapika.
 
Kupunguza wizara 15 siyo mchezo. Wanaouliza pesa za elimu zitatoka wapi hawakuyajuwa haya. Nadhani tutaheshimiana tuu. Eti kuna watumishi walikuwa hawauhesabu mshahara wanakula posho tuu. Maguuuuuu! Bado Tanesco.
safari za nje zimewaneemesha wasafiri, wapo wanaomiliki billions na milions benki. Gari za kifahari Na majumba hadi kwa michepuko. Mshahara utawidraw lini au Wa nini. Asante mhe JPM kwa kutumbua majipu.
 
Wizara ya Michezo iwe peke yake iwe kama wizara ya fedha, wizara ya maji yaani michezo iwe na wizara ya pekee isichanganywe na vitu vingine kabsa. Hii itasaidia michezo kukua kwa kasi kubwa.

Nguvu ya thoooda
 
Sina uhakika na maidara lakini mikoa na wilaya ni maamuzi tu ya raisi na pm wake. Mi nafikiri asiishie hapo tu, ukweli hata lengo la kuanzisha mikoa kama Geita, Njombe, Katavi binafsi naona haikufanywa kwasababu ya kumsaidia mwananchi, ilifanywa ili tu kuasaidia washkaji tu, naishi kwenye mkoa mpya mmoja wapo, kipya nilichokiona na magari mapya ya serikali lakini usaidizi hasa kwangu kama Mtanzania sijaona. Napendekeza nayo aipunguze tu.

Kaka mambo mengi hufanywa kisiasa na kumpendezesha mtu. Baadhi ya mikoa mipya haikua na sababu. Huwez kuniambia mkoa wa Iringa unauzidi Morogoro lakini Iringa imekatwa na kuzaliwa mpya wa Njombe. Lengo linatajwa ni urahisi wa huduma kwa Wananchi, ni lengo zuri ila utekelezaji wake ndiyo tatizo.
 
Back
Top Bottom