Wizara ya Vijana imeundwa kimakosa na woga tu

Wizara ya Vijana imeundwa kimakosa na woga tu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,247
Reaction score
16,169
Baada ya sekeseke la Oct29 kuunda wizara ya vijana kulionekana kama sehemu ya majibu na tiba ya kilichotokea na kilichosababisha vijana wakubali kutumika.

Hata hivyo, vijana ni nani na wako wapi?. Vijana ni wale wenye umri chini ya miaka 40 hivi. Vijana hawa wengi wao wako kwenye familia, mitaani, shuleni, vyuoni, majeshini, kwenye ajira za umma na watu binafsi binafsi, na wengine wengi wamejiajili wenyewe kwenye kazi mbalimbali; lakini lipo kundi ambalo hawana ajira kabisa.

Hii maana yake vijana tayari wako kwenye wizara ambazo tayari zipo, ilikuwa ni maswala tu ya kila wizara na kila sekta itimize wajibu wake katika kuwahudumia wadau ambao wengi wao ni vijana. Mfano, TAMISEMI, wizara ya ulinzi, ujenzi, usafirshaji, maendeleo ya vijana, wazee na wenye ulemavu, habari, michezo, utamaduni wanafanya nini kwa vijana wao walioko kwenye secta zao?

Kuunda wizara ya vijana itasababisha mkanganyiko wa kimajukumu na wizara nyingine kwasabu vijana ni haohao wanaohudumiwa kwenye wizara zote kama kilimo, ufugaji, elimu, usafirishaji, tamisemi, nk. Labda jina la wizara lingekuwa Wizara ya vijana wasiokuwa na ajira.
 
Screenshot_20260216-115515~2.png
 
Baada ya sekeseke la Oct29 kuunda wizara ya vijana kulionekana kama sehemu ya majibu na tiba ya kilichotokea na kilichosababisha vijana wakubali kutumika.

Hata hivyo, vijana ni nani na wako wapi?. Vijana ni wale wenye umri chini ya miaka 40 hivi. Vijana hawa wengi wao wako kwenye familia, mitaani, shuleni, vyuoni, majeshini, kwenye ajira za umma na watu binafsi binafsi, na wengine wengi wamejiajili wenyewe kwenye kazi mbalimbali; lakini lipo kundi ambalo hawana ajira kabisa.

Hii maana yake vijana tayari wako kwenye wizara ambazo tayari zipo, ilikuwa ni maswala tu ya kila wizara na kila sekta itimize wajibu wake katika kuwahudumia wadau ambao wengi wao ni vijana. Mfano, TAMISEMI, wizara ya ulinzi, ujenzi, usafirshaji, maendeleo ya vijana, wazee na wenye ulemavu, habari, michezo, utamaduni wanafanya nini kwa vijana wao walioko kwenye secta zao?

Kuunda wizara ya vijana itasababisha mkanganyiko wa kimajukumu na wizara nyingine kwasabu vijana ni haohao wanaohudumiwa kwenye wizara zote kama kilimo, ufugaji, elimu, usafirishaji, tamisemi, nk. Labda jina la wizara lingekuwa Wizara ya vijana wasiokuwa na ajira.

kwa hiyo miaka >30 bado ni kijana? una matatizo nafikiri, ujana unaishia miaka 18, baada ya miaka 18 kuanzia miaka 19 ni mtu mzima ana weza kuanzisha familia na pia anaweza kushitakiwa akifanya makosa kama kama mtu mzima akiuwa atanyongwa, akibaka atafungwa miaka 30 etc

hivyo kusema kwamba kijana ni chini miaka 40 inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa mtoto kiakili atleast ...
 
Tuliambiwa waandamanaji sio watz, ajabu tumeundiwa wizara ya vijana eti ndio suluhu ya matatizo yaliosababisha vijana wakaandama oktoba 29 ..hii nchi tumeikabidhi kwa watu wajinga kwelikweli halafu tunawaita WAHESHIMIWA!.
 
Nenda kawaambie kwenye mabaraza yenu ya CCM huko , sisi hiyo unayoita wizara hata hatuitambui wala huyo mbwatukaji.
 
Suluhisho la hayo yote ingekuwa katiba inayoweka ukomo wa idadi ya wizara na mawaziri au inayolipa bunge mamlaka ya kuridhia kuanzishwa kwa wizara.
 
kwa hiyo miaka >30 bado ni kijana? una matatizo nafikiri, ujana unaishia miaka 18, baada ya miaka 18 kuanzia miaka 19 ni mtu mzima ana weza kuanzisha familia na pia anaweza kushitakiwa akifanya makosa kama kama mtu mzima akiuwa atanyongwa, akibaka atafungwa miaka 30 etc

hivyo kusema kwamba kijana ni chini miaka 40 inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa mtoto kiakili atleast ...
Duhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Sasa wananchi wanalialia bila mpango unategemea nini kutoka kwa serikali kama si kufanya zimamoto
 
kwa hiyo miaka >30 bado ni kijana? una matatizo nafikiri, ujana unaishia miaka 18, baada ya miaka 18 kuanzia miaka 19 ni mtu mzima ana weza kuanzisha familia na pia anaweza kushitakiwa akifanya makosa kama kama mtu mzima akiuwa atanyongwa, akibaka atafungwa miaka 30 etc

hivyo kusema kwamba kijana ni chini miaka 40 inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa mtoto kiakili atleast ...
chini ya miaka 40 huwezi kuwa Rais wa nchi hii, unajua ni kwanini?
 
Tuliambiwa waandamanaji sio watz, ajabu tumeundiwa wizara ya vijana eti ndio suluhu ya matatizo yaliosababisha vijana wakaandama oktoba 29 ..hii nchi tumeikabidhi kwa watu wajinga kwelikweli halafu tunawaita WAHESHIMIWA!.
Lilikuwa swala la kuagiza kila wizara iwatendee haki vijana, wanawake, wazee na walemavu walioko kwenye wizara husika. Namna hii iko siku tutaunda wizara ya wazee kwakuwa wazee wameleta fujo pahala.
 
kwa hiyo miaka >30 bado ni kijana? una matatizo nafikiri, ujana unaishia miaka 18, baada ya miaka 18 kuanzia miaka 19 ni mtu mzima ana weza kuanzisha familia na pia anaweza kushitakiwa akifanya makosa kama kama mtu mzima akiuwa atanyongwa, akibaka atafungwa miaka 30 etc

hivyo kusema kwamba kijana ni chini miaka 40 inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa mtoto kiakili atleast ...
Umekosea sana inaonekana hujui maana ya kijana. Chini ya miaka 18 ni mtoto. Ujana unaanzia miaka 18 hadi 35. Wewe unataka kutuaminisha kuwa wale wanafunzi wa chuo wenye miaka 18+ sio vijana?
Ukisema "Kijana" ni neno ambalo tayari lipo kwenye kamusi ya Kiswahili na lina maana yake tayari ambayo imekubalika kutumika. Sio kujitungia tu definition zako mwenyewe
 
Serikali imefanya sahihi, kinacho takiwa hiyo wizara idumu.

Pia serikali itimize majukumu yake ki science and technology. Waachane na political propaganda science.

Hakuna nchi duniani iliyo stawi kiuchumi kwa kufanya siasa za uongo.

Mfano mradi wa mwendokasi.
Pesa zilikopwa WB na serikali, aliejenga miundo mbinu ni mchina.( Kosa la 1).

(Kosa la 2). Anapewa muaarabu kuendesha mradi(project ina kila kitu , mabasi , barabara.)

Kosa la 1 ,2 lina haribu mnyororo wa fedha kwa Wananchi ambapo vijana ni asimilia <70%.
 
Baada ya sekeseke la Oct29 kuunda wizara ya vijana kulionekana kama sehemu ya majibu na tiba ya kilichotokea na kilichosababisha vijana wakubali kutumika.

Hata hivyo, vijana ni nani na wako wapi?. Vijana ni wale wenye umri chini ya miaka 40 hivi. Vijana hawa wengi wao wako kwenye familia, mitaani, shuleni, vyuoni, majeshini, kwenye ajira za umma na watu binafsi binafsi, na wengine wengi wamejiajili wenyewe kwenye kazi mbalimbali; lakini lipo kundi ambalo hawana ajira kabisa.

Hii maana yake vijana tayari wako kwenye wizara ambazo tayari zipo, ilikuwa ni maswala tu ya kila wizara na kila sekta itimize wajibu wake katika kuwahudumia wadau ambao wengi wao ni vijana. Mfano, TAMISEMI, wizara ya ulinzi, ujenzi, usafirshaji, maendeleo ya vijana, wazee na wenye ulemavu, habari, michezo, utamaduni wanafanya nini kwa vijana wao walioko kwenye secta zao?

Kuunda wizara ya vijana itasababisha mkanganyiko wa kimajukumu na wizara nyingine kwasabu vijana ni haohao wanaohudumiwa kwenye wizara zote kama kilimo, ufugaji, elimu, usafirishaji, tamisemi, nk. Labda jina la wizara lingekuwa Wizara ya vijana wasiokuwa na ajira.
Kijiwe kipya cha malezi ya chawa na kifo cha uzalendo kwa taifa
 
kwa hiyo miaka >30 bado ni kijana? una matatizo nafikiri, ujana unaishia miaka 18, baada ya miaka 18 kuanzia miaka 19 ni mtu mzima ana weza kuanzisha familia na pia anaweza kushitakiwa akifanya makosa kama kama mtu mzima akiuwa atanyongwa, akibaka atafungwa miaka 30 etc

hivyo kusema kwamba kijana ni chini miaka 40 inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa mtoto kiakili atleast ...
na mtoto ni yupi?
 
Lilikuwa swala la kuagiza kila wizara iwatendee haki vijana, wanawake, wazee na walemavu walioko kwenye wizara husika. Namna hii iko siku tutaunda wizara ya wazee kwakuwa wazee wameleta fujo pahala.
wazee walete fujo pahala wana nguvu gani? Labda ulogi
 
Hujaelewa kusudi, nia na lengo la kuundwa wizara hiyo naomba nikueleweshe

Wizara hiyo imeanzishwa kuwa sauti ya vijana ambao ni wasomi au ni nguvukazi na haijaweza kutumika katika ujenzi wa Taifa.

Lengo la wizara hiyo sio kuingilia wizara nyingine bali kutambua fursa na kuzitumia kwa maslahi mapana ya vijana.

Halikuwa lengo la Serikali kuwaondoa vijana waliopo wizara nyingine kuwepo wizara ya vijana ila kutumia maarifa na ujuzi wa vijana mahali mbalimbali kutatua changamoto za vijana

Wizara ya vijana ni wizara pana inayogusa kila wizara ila sio inayoingilia kila wizara.

Wizara ya vijana inabaki kuwa ni chombo rasmi Cha kusimamia maendeleo ya vijana katika kila sekta.
 
Hujaelewa kusudi, nia na lengo la kuundwa wizara hiyo naomba nikueleweshe

Wizara hiyo imeanzishwa kuwa sauti ya vijana ambao ni wasomi au ni nguvukazi na haijaweza kutumika katika ujenzi wa Taifa.

Lengo la wizara hiyo sio kuingilia wizara nyingine bali kutambua fursa na kuzitumia kwa maslahi mapana ya vijana.

Halikuwa lengo la Serikali kuwaondoa vijana waliopo wizara nyingine kuwepo wizara ya vijana ila kutumia maarifa na ujuzi wa vijana mahali mbalimbali kutatua changamoto za vijana

Wizara ya vijana ni wizara pana inayogusa kila wizara ila sio inayoingilia kila wizara.

Wizara ya vijana inabaki kuwa ni chombo rasmi Cha kusimamia maendeleo ya vijana katika kila sekta.
Umejikanyaka kaka, hizo fursa ambazo vijana wanatakiwa kuzitambua na kuzitumia ziko kilimo, ufugaji, uvuvi, afya, ulinzi, uhamiaji, madini, utalii, biashara, ujenzi na usafirishaji. Huko kote walipaswa kujua namna na kuhangaika na vijana kwenye fursa zinazopatikana huko. Wizara ya fedha ilitakiwa kujua namna ya kuhangaika na vijana.

Kazi ya wizara ya vijana ni nini? Yaani wizara ya vijana itakwenda wizara ya ulinzi au kilimo, au afya, au biashara au viwanda au madini au utalii kuwaambia nini kuhusu vijana? Hii ni duplication ya hali ya juu.
 
Baada ya sekeseke la Oct29 kuunda wizara ya vijana kulionekana kama sehemu ya majibu na tiba ya kilichotokea na kilichosababisha vijana wakubali kutumika.

Hata hivyo, vijana ni nani na wako wapi?. Vijana ni wale wenye umri chini ya miaka 40 hivi. Vijana hawa wengi wao wako kwenye familia, mitaani, shuleni, vyuoni, majeshini, kwenye ajira za umma na watu binafsi binafsi, na wengine wengi wamejiajili wenyewe kwenye kazi mbalimbali; lakini lipo kundi ambalo hawana ajira kabisa.

Hii maana yake vijana tayari wako kwenye wizara ambazo tayari zipo, ilikuwa ni maswala tu ya kila wizara na kila sekta itimize wajibu wake katika kuwahudumia wadau ambao wengi wao ni vijana. Mfano, TAMISEMI, wizara ya ulinzi, ujenzi, usafirshaji, maendeleo ya vijana, wazee na wenye ulemavu, habari, michezo, utamaduni wanafanya nini kwa vijana wao walioko kwenye secta zao?

Kuunda wizara ya vijana itasababisha mkanganyiko wa kimajukumu na wizara nyingine kwasabu vijana ni haohao wanaohudumiwa kwenye wizara zote kama kilimo, ufugaji, elimu, usafirishaji, tamisemi, nk. Labda jina la wizara lingekuwa Wizara ya vijana wasiokuwa na ajira.
 
Back
Top Bottom