beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Serikali imeruhusu mazao ya chakula kuuzwa nje ya nchi ili kutoa fursa kwa Wakulima kunufaika na mazao mbalimbali wanayoyazalisha.
Imesema kuwa itakuwa ikitoa vibali kwa wafanyabiashara wa mazao.
Hayo alisemwa juzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Kusaya, walipokuwa kwenye ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya kilimo iliopo mkoani Morogoro, ambapo aliwataka wakulima kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi.
“Serikali kupitia wizara yangu imeamua kufungua fursa kwa wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi kulingana na mahitaji ya soko la nchi husika ili kuwapa faida wakulima hao na kuwaimarisha kiuchumi zaidi,” alisema Kusaya.
Kusaya alisema Wizara ya Kilimo inawataka wafanyabiashara wa mazao hasa ya chakula kujitokeza kufanya biashara nje ya nchi kwani serikali itakuwa bega kwa bega kutoa vibali kwa wafanyabiashara wanaotaka kuuza mazao yao nje.
Katibu Mkuu huyu alisema serikali imeruhusu mazao kuuzwa nje nchi ili kutoa fursa ya kuongeza soko kwa wakulima kupata faida zaidi kutokana na kutumia nguvu nyingi katika uzalishaji wa mazao mbalimbali hasa ya chakula.
Imesema kuwa itakuwa ikitoa vibali kwa wafanyabiashara wa mazao.
Hayo alisemwa juzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Kusaya, walipokuwa kwenye ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya kilimo iliopo mkoani Morogoro, ambapo aliwataka wakulima kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi.
“Serikali kupitia wizara yangu imeamua kufungua fursa kwa wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi kulingana na mahitaji ya soko la nchi husika ili kuwapa faida wakulima hao na kuwaimarisha kiuchumi zaidi,” alisema Kusaya.
Kusaya alisema Wizara ya Kilimo inawataka wafanyabiashara wa mazao hasa ya chakula kujitokeza kufanya biashara nje ya nchi kwani serikali itakuwa bega kwa bega kutoa vibali kwa wafanyabiashara wanaotaka kuuza mazao yao nje.
Katibu Mkuu huyu alisema serikali imeruhusu mazao kuuzwa nje nchi ili kutoa fursa ya kuongeza soko kwa wakulima kupata faida zaidi kutokana na kutumia nguvu nyingi katika uzalishaji wa mazao mbalimbali hasa ya chakula.