Wito kwa wana CHADEMA wote!

Wito kwa wana CHADEMA wote!

Masikini Migamba! Nani kakuponza hadi ukaingia mkenge? Au ni hayo yasemwayo kuwa ulipewa ahadi ya kufutiwa kesi na mshiko juu? Unasaliti nafsi yako kwa woga? Umefanya kazi na Lema muda mrefu bado tuu hujajifunza kutoka kwake juu ya kauli mbiu yake kuhusu WOGA?
Lema alisha waonhesha watawala kuwa haiogopi jela kwa kukataa dhamana na kwenda jela kwa kusimamia ukweli na uliona heshima yake ilivyokuwa hapo Arusha na Tanzania nzima. Sasa hivi hata hiyo serikali sasa inamwogopa na kumheshimu na mambo ndani ya Halmashauri ya Arusha yanaenda vema. Juta na kurudia uadilifu na utasamehewa.
 
Unapojadili hakikisha unabaki kwenye hoja.. Hoja ni kwa nini kipengele cha ukomo wa madaraka kwenye uongozi wa juu kimeondolewa katika katiba???

Hoja hii inahitaji majibu kutoka kwa viongozi wa juu.
 
We hate two faced people,ni ngumu kujua wanamtumikia nani even though uko nao!
 
asilimia 90 we ni mchagga na asilimia 10 we ni muiraq na asilimia 100 ww ni mkaskazini

mkuu haya majinamizi tatzo lao hawajibu kile kilicho ulizwa wanajibu ----- tu,mbowe mwenyew ndo huyo ameshikwa pabaya,mpaka sasahv hajajibu watanzania hilo jengo la dubai kalipataje
 
MTOTO KITAA
===>Mimi hapa ndio panaponishangaza,tangu jana suala hili la Mwigamba lilipoibuka watu wengi waliomba kuwa hata kama atafukuzwa je hoja alizotoa pia ni za uongo?
===>Suala la kutofanyika kwa uchaguzi pia ni la uongo?kwa kweli hata sisi mashabiki wa CDM tunaanza kushikwa na ka uoga kuhusiana na hali ya mambo ndani ya CDM,
===>Pamoja na yote haya naanza kuhisi kuwa CDM hasa viongozi hawasikilizi maoni ya wanachama wenzao,na pia inawezekana kabisa ukiongea kitu ambacho hakimfurahishi Mbowe au Dk Slaa basi wewe ni adui na ni muasi wa chama,kwa sababu kwa maelezo aliyotoa Tumaini Makene jana kuwa Mwigamba alikisifia chama kwa kutekeleza ahadi za chama vizuri,na muda huo huo akaposti tamko lililosababisha akaondolewa hii inaonekana kuwa ukisema kitu tofauti na kile ambacho viongozi hawakifurahii basi unaondolewa madarakani
===>Taratiibu naanza kumuna Zitto kama kiongozi makini na mvumilivu sana ndani ya CDM,
===>Mbowe na Dk Slaa tunaamini mnahusika kwa namna moja ama nyingine kwenye mgogoro hasa kwa nyie kuendelea kukaa madarakani bila kufuata taratibu na sheria za chama,mkijifanya mnajua na kuanza kufukuza watu ambao wanahoji yale ambayo mmekuwa mnayakosea basi mkae mkijua CDM itawafia mikononi mwenu,si lazima kwa Mbowe au Dk Slaa kugombea urais mwaka 2015,au kuendelea kukaa madarakani maisha,waacheni wana CDM waamue wenyewe,kama wana CDM wanataka nyie muwe wagombea hilo halina ubishi mtakuwa tu,lakini taratibu zifuatwe ili kukinusuru chama.
===> Kitila Mkumbo,Prof Safari na wengineo wasaidieni hawa viongozi wa CDM na huu ndio wakati wa kuwa pamoja kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2014,kama msiporekebisha haya itakula kwenu mapema sana.

hata mimi nimeanza kuona kuwa chama kinaendeshwa na watu wawili huu ni upuuzi huenda hata zitto huwa tunamuonea tu!
 
Last edited by a moderator:
Samson Mwigamba nini kimekukuta hadi ukafikisha ujumbe kwa njia Mbaya kiasi hicho?

Nilikupenda sana toka umeandika ile makala ya "Wito kwa Askari wote" ilikuletea misukosuko
sana hadi kuwekwa kizuizini kwa kosa la chochezi. Umekuwa mhubiri mzuri sana wa sera safi za CDM
inakuwaje sasa unataka kurudi kwa maccm?
Anyway tafakari kisha andaa Majibu mazuri utakapoitwa kwenye kikao cha hukumu. Nenda ukaseme kkila kitu
kama kuna upande wa pili ulikushawishi kufanya hivyo.

kweli CDM kilianza na Mungu na kitamaliza na Mungu. Mungu mkubwa!
 
Ndiyo maana tunajitahidi kuwafungua wananchi macho kwa kuwaeleza ukweli kwamba CHADEMA ni chama cha kilaghai.
 
Chd sio chama kinachokumbatia mafisadi au uovu ukikosa utaadhibiwa bila kujali ww ni Chenge, Lowassa, Ngeleja au Rostam ndio tofauti na chama cha majambazi. Mtasema sana lakini Mbowe na Slaa ni kiboko yenu. Ilo mnalijua kwani ndio mana maneno mengi na mmejaribu sana kuwahonga lakini hakuna kitu. Mbona hamzungumzii cuf, nccr, tlp tatizo lenu mkikamatwa mnataka kuwachagulia watu viongozi katika vyama vyao. Kwani wanachama wa cdm wamelalamika. Mnapandikiza mamluki mkitegemea kuivuruga cdm, ndio mana mlisema cdm haifiki 2014 mkiwategemea watu kama hao. Yeye ni mwenyekiti tena wa kanda alishindwa nn kuwakilisha mawazo yake kwenye vikao vya chama. Hapa ndio mjue cdm wako juu hakuna alie juu ya sheria. Mtabaki kusema oh Mbowe na Sla ni viongozi wa kudumu na ss wanacdm tunasema watakuwa wa kudumu mpaka Tanganyika ipate uhuru. Hata marehemu baba wa taifa alikaa miaka kibao kabla hajamwachia Mwinyi. Mbona hamsemi unajianya kumbukumbu huna.

maamuzi gani wewe shibuda amefanya mangapi? Ambayo mpaka sasa yanakigharimu chama mkuu!
 
ndg yangu mtotokitaa, katiba ilibalishwa baraza kuu hivyo hakuna ukweli wowote ktk hili la kuweka kinyewela, kuhusu uchaguzi bado viongozi hawajamaliza kipindi ambacho kikatiba kinaisha sept 2014 kutoka uchaguzi ulipofanyika 2009 kwa mara ya mwisho.
 
Unapojadili hakikisha unabaki kwenye hoja.. Hoja ni kwa nini kipengele cha ukomo wa madaraka kwenye uongozi wa juu kimeondolewa katika katiba???

Hoja hii inahitaji majibu kutoka kwa viongozi wa juu.

Mbowe hajabadili hicho kifungu bali ni baraza kuu na ikapitishwa... Ushambenga tu
 
Kwanini wafuasi wa CCM na anti CHADEMA wote wanataka uongozi wa CDM ubadilike?Wenye akili zetu tunajua kwamba huu ndio Uongozi utakaoipeleka CDM ikulu na kutuondoa kwenye utawala wa mkoloni mweusi CCM
PakavuNateleza
===>Hili kila mtu naliombea,hakuna mtu anaetaka kuona CCM inaendelea kutawala lakini tatizo hapa linaloonekana ni kutokufuatwa kwa taratibu za kichama,kwa nini chaguzi zilizopangwa hazifanyiki?
 
Last edited by a moderator:
Inawezekana kabisa Mwigamba alikuwa na hoja nzuri, lakini njia ambayo ametumia ni ileile ambayo yeye mwenyewe aliipinga na kuikemea kipindi kile akina mwampamba walipoitumia.Angeweza kuwasilisha maoni yake kwenye vikao vya chama.Vilevile kama hayo ambayo anayazungumza yapo basi kunatatizo kubwa katika uongozi wa juu wa chama.
 
Huyu Mamluki anayejiita Maskini Mkulima amenaswa leo mtasikia habari zake kesho, Watu wanahatarisha maisha yao kwa kutaka kuleta mabadiliko halafu wahuni wachache wanasaliti dhamira njema.. Tutapambana hadi tone la damu la mwisho.

Mkuu umenena..mimi kama mtanzania wa kawaida ninaiman na cdm na viongoz wake. Wanafanya mambo kisayansi na syo kwa kukurupuka. Kutofanyika uchaguz ndani cdm kuna ishu au siri flani wameiona ndyo wakaweka pozi kwa uchunguzi zaidi haya taratibu wale mamluki kama samson muigamba kanza kuabika mchana kweupe. Mungu mkubwa sana
 
Last edited by a moderator:
PakavuNateleza
===>Hili kila mtu naliombea,hakuna mtu anaetaka kuona CCM inaendelea kutawala lakini tatizo hapa linaloonekana ni kutokufuatwa kwa taratibu za kichama,kwa nini chaguzi zilizopangwa hazifanyiki?

Sababu ni hii

Watu msikirupuke na kulaumu CHADEMA kutokufanya uchaguzi mapema,Issue iko wazi kwamba CCM wameweka mamluki wakutosha CDM so vetting ya kutosha lazima ifanyike in advance kabla ya uchaguzi ili tusiwechague viongozi Mamluki.We unadhani kina wasirra and co plus buku saba fc wanaosema chadema itasambaratika hawana strategy? Chama makini lazima tujiridhishe kwamba wanaochaguliwa ni viongozi makini na hawaongeki ili ukombozi wa pili wa mtanzania utimie.This is just food for thought.

Pili viongozi wako madarakani kihalali na kikatiba. Muda wao unaisha september 2014.
 
m.maranya kumbe watatawala milele kwa sababu wameitoa mbali hakuna tofaut ya sharifu na slaa mrema na mbowe.au cheyo na mbowe kumbe chadema sio mbadala tena kama hoja ni kuitoa mbali basi nyerere angekufa akiwa rais au mtei angebaki kuwa mwenyekiti.

Magamba jaman..wanahaha mbowe n sla waondoke madarakan. Mimi binafsi kama mtanzania wa kawaida kabisaa ninawaunga mkono viongozi wa cdm 100% na nina imani nao sana
 
Kufuatia malumbano yanayoendelea kwenye vyombo vya habari namadhaifu mengi ambayo tumeshayashuhudia kwenye chama kwa sasa, natoa wito kwawana CHADEMA wote nchini kwamba wakati umefika tubadilishe uongozi wa juu wachama.

Nitaendelea kuwadondolea ili muonekwa nini napendekeza tuung'oe uongozi huu chini ya Mbowe.

Ahsanteni kwakunisoma
!

Mkuu Maskini Mkulima, nyinyi Chadema, hamtaki kabisa kuambiwa ukweli!, pole kwa yaliyokukuta kwa kuusema ukweli huu!. Kwenye hili, mimi niko upande wako ingawa kwenye lile la kina Shonza, japo ulijua sheria, taratibu na kanuni hazikufuatwa na ni wewe ndiye aliyeposti hii posti

Kama nilivyoahidi dakika chache zilizopita, naomba kuweka hapa mtandaoni barua ya kufukuzwa uanachama wa BAVICHA Bi. Juliana Shonza aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa".

Kumbuka, what goes around, comes around!, sasa ni zamu yako!, na ili kusimama imara kwenye ukweli, ukiipokea barua yako, pia tupostie humu!.

Hili la Chadema, nililisema ile 2010 kuwa CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga! - na nilishambuliwa sana, nisome kwa makini, nilisema nini kuhusu Mwenyekiti wa Chadema Mhe. Mbowe.

Sasa japo dalili za kujipanga zipo, time is not very friendly, hii dilly dallying won't reach you anywhere!, mtajikuta mnaishia kufanya too little too late!, 2015 November, nitawakumbusha tena nilichowaambia ile November, 2010!.

Pasco.
 
asilimia 90 we ni mchagga na asilimia 10 we ni muiraq na asilimia 100 ww ni mkaskazini

mkuu haya majinamizi tatzo lao hawajibu kile kilicho ulizwa wanajibu ----- tu,mbowe mwenyew ndo huyo ameshikwa pabaya,mpaka sasahv hajajibu watanzania hilo jengo la dubai kalipataje
 
Back
Top Bottom