Wito kwa wana CHADEMA wote!

Wito kwa wana CHADEMA wote!

Hoja siyo tu kwa nini wabadilishe kipengele cha katiba kinyemela, bali why are they ruling with an iron hand and kangaroo committee.

Chama kilichoanzishwa kwa misingi ya kilaghai hata utendaji utakuwa niwa kilaghai.

Kwa hiyo ulitaka mamluki mliowatuma tuendelee kuwachekea? well well done mr.mbowe &dr slaa kutusafishia chama chetu.HATUWEZI KUYARUHUSU MAFISI KUONGOZA CHAMA CHETU.
 
Magamba jaman..wanahaha mbowe n sla waondoke madarakan. Mimi binafsi kama mtanzania wa kawaida kabisaa ninawaunga mkono viongozi wa cdm 100% na nina imani nao sana

ALIYEANDIKA POST HII NI MWANACHADEMA, MWENYEKITI WA CHADEMA ARUSHA

humo humo..magamba hawamo humu

mtaisoma
 
I can see tatizo ni lilelile la siku zote Team Zitto.

Inshallaah mwenyezi Mungu ampewepesi Huyo Mbowe na akae pembeni na Kupisha wengine maana hiki chama kilipofikia sasa ni vita ni vita na ni vya wenyewe kwa wenyewe.
 
Tulingo'a madiwani,Tukang'oa bi shonza na sasa ni Mwigamba.
" @Our way or highway''
meningitis
===>Hili suala ni muhimu likafanyiwa kazi,moto ulioshindwa kuzimwa jana leo ndio unazidi kuwaka,mkiendelea kufanya kazi kwa makundi hakika hamtapona CDM.
 
Last edited by a moderator:
Samson Mwigamba nini kimekukuta hadi ukafikisha ujumbe kwa njia Mbaya kiasi hicho?

Nilikupenda sana toka umeandika ile makala ya "Wito kwa Askari wote" ilikuletea misukosuko
sana hadi kuwekwa kizuizini kwa kosa la chochezi. Umekuwa mhubiri mzuri sana wa sera safi za CDM
inakuwaje sasa unataka kurudi kwa maccm?
Anyway tafakari kisha andaa Majibu mazuri utakapoitwa kwenye kikao cha hukumu. Nenda ukaseme kkila kitu
kama kuna upande wa pili ulikushawishi kufanya hivyo.

kweli CDM kilianza na Mungu na kitamaliza na Mungu. Mungu mkubwa!
iPad ya Apple
===>Hata mimi siamini maana huyu jamaa tunamsikia kila siku,mimi nafikiri CDM kuna matatizo makubwa sana,sema wanayaficha ficha kila siku,
===>Ila haya makundi wanayoyaendeleza ndani ya chama ni hatari sana,ni bora wayafanyie kazi,siku hizi naanza kushikwa na wasiwasi na viongozi wa juu wa CDM,inaonekana wamejisahau na kuna watu wanajiona ni waungu watu,
 
Last edited by a moderator:
Kifupi, huyu Mwigamba ni pro-Zitto, na huenda kahongwa na Zitto kwa manufaa ya kisiasa. Kimsingi CHADEMA haikuungana na CCM vs Zitto, na wala CHADEMA hakijamshamulia Zitto bali chama kilijitetea kawaida dhidi ya Kamati ya PAC. CHADEMA mulikeni wasaliti hapa. Kuna kila dalilii kuwa kauli ya Zitto ina uhusiano na hii ya Mwigamba. Na lengo la Mwigamba na Zito ni moja. Kwa maneno mengine, kauli ya Mwigamba inaendeleza na kufafanua kauli ya Zitto
 
iPad ya Apple
===>Hata mimi siamini maana huyu jamaa tunamsikia kila siku,mimi nafikiri CDM kuna matatizo makubwa sana,sema wanayaficha ficha kila siku,
===>Ila haya makundi wanayoyaendeleza ndani ya chama ni hatari sana,ni bora wayafanyie kazi,siku hizi naanza kushikwa na wasiwasi na viongozi wa juu wa CDM,inaonekana wamejisahau na kuna watu wanajiona ni waungu watu,

yote haya sababu kuu ni zitto na tamaa ya uenyekiti
 
Last edited by a moderator:
I can see tatizo ni lilelile la siku zote Team Zitto.

Inshallaah mwenyezi Mungu ampewepesi Huyo Mbowe na akae pembeni na Kupisha wengine maana hiki chama kilipofikia sasa ni vita ni vita na ni vya wenyewe kwa wenyewe.

hakika haya ni kutokana na team zitto na nasema jamaa mbowe akitoka na zitto kuingia ndio mwisho wa cdm.
 
"Ndiyo maana kuna tabaka la viongozi - kwamba mambo fulani ni ya viongozi kutatua na kuwekana sawa ili kuendeleza harakati na vile vile kuna mambo ya kuwashirikisha wananchi wote!

Cha ajabu hapa Tanzania (sijui ni ulimbukeni na ugeni kwenye teknolojia?) waliopewa dhamana ya uongozi wanafikiri kwamba mitandao ya kijamii ndo maeneo maalum ya kutatulia tofauti zao! Kuna viongozi wanakesha kupost maamuzi ya ndani kwenye vikao vyao sijui kwa faida ya nani sasa? Nachelea kusema kuwa umaskini wa mawazo unatusumbua sana nchi hii na tutabaki kupiga mark time hapa hapa tulipo!
 
Ndiyo maana tunajitahidi kuwafungua wananchi macho kwa kuwaeleza ukweli kwamba CHADEMA ni chama cha kilaghai.

Ulaghai kwa kuwahadaa viongozi waoga kama Mwigamba, sisi hatulei mamruki na wasio kuwa na sifa tuna scan kisha tuna delete na kufuta kabisa.
 
Duuuh kazi kweli kweli jamani angalieni na kazi inayofanyika...hata panya anakula kwa kukupa raha
 
Tatizo la chadema ni kutokupenda kukosolewa. Hapa mwigamba ana haki ya kusema aliyoyasema. Chama kinapaswa kuyafanyia kazi badala ya kutokwa na povu
 
Watanzania/wanachadema yatupasa kuwa makini sana katika wakati huu wa mpito ambapo vyama tunavyoweza kudhania vinakuja kutusaidia vikaja kutugeuka. Lkn pia katika vyama tuwe makini katika wakati huu ambapo ndani ya vyama kuna wafuasi wa ndugu yetu ibilisi ambaye kazi yake ni kuvunja na kuharibu. Sasa cha muhimu hapa ni kujiuliza yafuatayo;1. Je mtoa mada akiwa kati ya viongozi ndani ya chama amekosa kabisa sehemu ambapo angewakilisha hizi ajenda zake na akaeleweka kuliko kulalamika huku nje? na je huo ndo uongozi?2. Hakuna haja ya kuchukua ajenda zake na kuzikataa badala yake ni kukaa chini na kuangalia penye ukweli ili awa viongozi wajulikane kama kweli nao ni wale wale ambao huku nje inasemekana wanawapinga(mafisadi), narejea hali mbaya ya ofisi za mikoa na kanda
 
Chadema ni saccos ya wachache, kubali kataa, huo ndio ukweli
 
MOSI:
CHADEMA inabidi ipige hatua ya ziada, humu kwenye mitandao wako wengi wanaokichafua chama kutokana na post na comments zao,,,, wapo wanaCHADEMA kwa makusudi aidha kwa kutumwa au kwa kujituma wamekuwa wakimchafua Zitto huku wakidhani kumchafua kiongozi si kuchafua chama. Watu wa namna hii lazima nao washughulikiwe.

Halafu hii tabia ya kuchafua viongozi kwa kutumia mitandao imeshakuwa ndio tabia ya watu fulani humu kwenye mitandao, afadhali ya Mwigamba kafanya hivyo[kawachafua viongozi] kwa kujenga hoja, lakini wengine wanawachafua viongozi wengine bila hata hoja,,,husani wale wanamchafua Zitto sikuzote wanafanya hivyo bila hata hoja zaidi ya mtu akimua kuchafua hali ya hewa, basi anafanya hivyo. Nimesema Mwigamba kawachafua viongozi kwasababu amewakosoa viongozi nje ya utaratibu wa kichama, TABIA KAMA HII NA IKOME.

PILI:
Naunga mkono hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi ya Mwigamba, kwani kitendo cha Mwenyekiti wa chama mkoa kutumia mitandao kukosoa chama lazima kihesabike kuwa ni hujuma dhidi ya chama na njama za kukichafua chama hata kama hoja zake zitakuwa lulu kwa kiasi kikubwa. Hivyo, hatua hizi ziwe fundisho kwa viongozi wenye tabia kama zake.

TATU:
CHADEMA lazima iangalie mfumo wake wa kupokea mawazo mapya, maoni na utaratibu mzima wa vikao vya chama. Kwa vyovyote vile hizi hoja za Mwigamba hazijalishi mbaya au nzuri atakuwa amekosa jukwaa la kuzisemea ndani ya chama au chama kina mfumo usio rasmi wa kubeza mawazo mapya. Kama hali hii ndivyo ilivyo ndani ya chama chetu, kwa vyovyote watu watatafuta majukwaa ya kuibua mawazo mapya na kutoa maoni nje ya majukwaa rasmi ya CHADEMA, kwa kuzingatia wazo jipya huboresha au hupinga wazo la zamani hivyo basi mtoa wazo jipya au maoni ataonekana ni msaliti pamoja na nia yke nzuri kwa chama.

NNE:
Nimesoma hoja za Mwigamba, labda uwe mwendawazimu, au kibaraka wa mfumo ulikosolewa na hoja za Mwigamba ndio utaweza kuona kuwa MWIGAMBA hoja zake hazina mashiko, lakini kiukweli CHADEMA haitakiwi kuzijibu hoja za Mwigamba bali inatakiwa kuzifanyia kazi. Isishie kumchukulia hatua za kinidhamu tu bali pia izifanyie kazi hoja zake, kwani zinaeleweka na kwa vyovyote vile amezitoa kwa lengo la kujenga chama na si vinginevyo.

MUNGU IBARIKI CHADEMA.
 
dah mbowe ni nomaaaaa!!na kwnn asiachie hyo nafas wengne wakiendeleze chama,nadhan iko shida!!
 
Nimekusoma mpaka mwisho. Kuna hoja japo unatakiwa kuleta data ili ziwe kamili. Kila mtu ana haki ya kukosoa. Lakini je, haya mambo hayakuonekana mapema? Isije ikawa mpango wa kuiua CDM kuelekea 2015. Kaofisi ka Kinondoni hakafai hakana hadhi.
 
Back
Top Bottom