MTOTO KITAA
===>Mimi hapa ndio panaponishangaza,tangu jana suala hili la Mwigamba lilipoibuka watu wengi waliomba kuwa hata kama atafukuzwa je hoja alizotoa pia ni za uongo?
===>Suala la kutofanyika kwa uchaguzi pia ni la uongo?kwa kweli hata sisi mashabiki wa CDM tunaanza kushikwa na ka uoga kuhusiana na hali ya mambo ndani ya CDM,
===>Pamoja na yote haya naanza kuhisi kuwa CDM hasa viongozi hawasikilizi maoni ya wanachama wenzao,na pia inawezekana kabisa ukiongea kitu ambacho hakimfurahishi Mbowe au Dk Slaa basi wewe ni adui na ni muasi wa chama,kwa sababu kwa maelezo aliyotoa
Tumaini Makene jana kuwa Mwigamba alikisifia chama kwa kutekeleza ahadi za chama vizuri,na muda huo huo akaposti tamko lililosababisha akaondolewa hii inaonekana kuwa ukisema kitu tofauti na kile ambacho viongozi hawakifurahii basi unaondolewa madarakani
===>Taratiibu naanza kumuna Zitto kama kiongozi makini na mvumilivu sana ndani ya CDM,
===>Mbowe na Dk Slaa tunaamini mnahusika kwa namna moja ama nyingine kwenye mgogoro hasa kwa nyie kuendelea kukaa madarakani bila kufuata taratibu na sheria za chama,mkijifanya mnajua na kuanza kufukuza watu ambao wanahoji yale ambayo mmekuwa mnayakosea basi mkae mkijua CDM itawafia mikononi mwenu,si lazima kwa Mbowe au Dk Slaa kugombea urais mwaka 2015,au kuendelea kukaa madarakani maisha,waacheni wana CDM waamue wenyewe,kama wana CDM wanataka nyie muwe wagombea hilo halina ubishi mtakuwa tu,lakini taratibu zifuatwe ili kukinusuru chama.
===>
Kitila Mkumbo,Prof Safari na wengineo wasaidieni hawa viongozi wa CDM na huu ndio wakati wa kuwa pamoja kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2014,kama msiporekebisha haya itakula kwenu mapema sana.