Wingu Jeusi la kuvunjika Amani

Wingu Jeusi la kuvunjika Amani

Very analytical, extremely readable. Watanzania wamebanwa kote kote hawana pa kupumulia. Lakini hata Shah aliyekuwa na majeshi maradufu, hatimaye aling'olewa. Siku walio wengi watakapochoshwa na hali iliyopo, hapo chochote kinaweza kutokea.

umenikumbusha uyu mfalme wa irani alotawala kwa mkono wa chuma miongo kadhaa lakini kuna wakati wananchi walisema basi
 
Jamani mbona tuna wasiwasi hivyo? Hamkumbuki uzinduzi wa bomba la gesi juzijuzi na sasa Dar makali ya Mgao wa Umemenyamepungua sana??? (Sijui mikoa mingine), hamkumbuki malipo ya madeni ya walimu, maboresho ya vyombo vya ulinzi na usalama, n.k. Inawezekana kwenye hizi siku chache kuna mambo mengine yanakuja kabla ya tarehe 25 october kwani jinsi kasi ya maendeleo inavyotokea ndani ya wiki mbili hizi ni kubwa sana......tuendelee kufunga na kuomba!

Waamini hiyo ni kasi ya maendeleo!? Mie naona ni nguvu ya soda tu na hongo,

Kwani hayo madeni ni ya mwezi huu?!

Huku mikoani hatuna umeme mwezi takribani watatu sasa...

Unasema nini wewe?!
 
Dada FF najua mahaba yako na ccm pia najua unatokwa povu tu hapa lakini yaliyo elezwa yanagusa mtima wako.... ni mjinga pekee atakae puuzia uzi huu kwamba hamna hoja... lakini wewe najua unaatetea mkate wako.... watawala hukosa busara na hekima, humweka Mungu pembeni japo wanasali na vibaraka wao kama wewe huwapigia makofi... ila wakati ukifika utakuwa umeisha umiza wengi ila uhuru kamili utapatikana... pole dada angu.

Ana mahaba na JK sio CCM
 
"taarifa ambazo polisi imezipata ni kwamba kuna watu wamepanga mbinu za kuvuruga uchaguzi katika mji wa Bukoba na maeneo ya jirani. Wamepanga kuwatisha na kuwashambulia watakaojitokeza kupiga kura na wana mpango wa kukaa vichochoroni wakiwa na mapanga, nondo na siraha nyingine ili kuhakikisha wanatimiza lengo hilo. Polisi imejipanga na imewaonya watu hao kuwa wasithubutu kutekeleza mpango huo" Reporter (Somebody) Mtiganzi wa Radio One.

Nimeiskia habari hii katika kipindi cha Nipashe asubuhi ya leo, sio kuwa niliona uchungu tu lakini aibu ya kuwa na jeshi la polisi linaloweza kutoa taarifa ya 'kijima' kiasi hiki. Sikutegemea kabisa! Hivi polisi kweli wanaweza kujua habari nyeti kama hizi na kuitisha press kuwaonya wanaoplan wasifanye!!??
Kinachoonekana wazi hapa ni kwamba watu wengi wamezaliwa wakakuta amani na kwa sababu mfumo wetu wa elimu ni mbovu unapelekea hata 'wanaosoma' na kupata ajira kama polisi hawawezi kuelewa ni jinsi gani amani inaweza kutokea penye vita au vita inaweza kutokea penye amani.
Serikali inachotaka kufanya ni kuzuia mabadiliko mwaka 2015 kwa kutumia mbinu za mwaka 1975. Huenda wakaona matokeo tofauti. Kikubwa na kinachoonekana tunaweza kupata wateja wa ICC kutoka Tanzania kwa maana watu wengi wanaotaka mabadiliko wanamaanisha mabadiliko na hatujui kiwango chao cha woga ni kiasi gani katika kushindana na vitisho hivi!
 
Acha hofu mkuu, rais JK ni mtu wa demokrasia sana sema kuna majitu yanayomzunguka ndiyo yanamuharibia na kumpa presha; rejea issue ya Katiba mpya. Jana kaongea kauli ya kidemokrasia, kwamba yuko tayari kukabidhi nchi kwa rais yeyote yule atakayeshinda. Penye kusifia tusifie, penye kukosoa tukosoe.

Kumbuka ni huyu JK aliwaambia CCM wenzake kule Dodoma kuwa, "Wajiandae kisaikolojia kwani wanaweza kung'oka." Kwa hiyo yeye amekwisha jiandaa kisaikolojia tyr, wito wangu ni kwa ccm wengine waige mfano wa rais wetu.

Binafsi, naamini JK hatatuangusha kwa kukataa kuruhusu upinzani kuingia ikulu. Hiki ni kipimo chake cha mwisho kidemokrasia ili atwae tuzo ya Mo. Ibrahim.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Ukawa.
 
Natatizwa sana kuona Serikali ya KIkwete ikijiimarisha "kiulinzi" kupitia Jeshi, Polisi na hata Usalama wa Taifa eti kudhibiti na kuzuia machafuko wakati wa uchaguzi mkuu.

Serikali imeweka majesho yote kwenye Red alert, polisi wamekabidhiwa magari mmapya zaidi ya 700 leo na yanasambazwa nchi nzima.

Najiuliza, hatua hizi za kuonyesha ukakamavu na uimara wa ulinzi leo hii ambapo tunakaribia kutimiza haki yetu ya kidemokrasia na kikatiba inatokana na nini?

Iweje ghafla kuwe na umuhimu wa kuhakikisha ulinzi na usalama uko imara zaidi kwa tendo la kuaminiana na linalohitaji amani, busara na hekima kuhakikisha katiba yetu na demkorasia tunayo ihubiri na kujisifia kuwa na amani, utulivu na mshikamano ni kitu cha kweli na si ulaghai na kiini macho?

Ni kitu gani hasa ambacho si sahihi na kina walakini kufikia hatua wananchi wanaweza kukosa imani na utiifu kuanzisha fujo na Serikali kuonelea ulazima wa kutunisha misuli "kudhibiti" amani?

Najiuliza ni wapi tumekosea kwamba Serikali na hasa Chama Tawala kukosa kuaminika kwa wale ambao si wafuasi wa Chama Tawala?

Je ni nchi ya namna gani tunaijenga inapofikia Serikali iliyoko madarakani inaonekana imejenga mazingira yasiyo ya haki, demokrasia na utu kwa manufaa ya Taifa na kuwa na upendeleo au kulazimisha Chama kilichoko madarakani kitumie dola kujihakikishia muendelezo wa utawala wake?

Hisia za hujuma zilizoonyeshwa katika chaguzi zilizopita zimepuuziwa. Mazingira ya rushwa yameendela. Vitisho vya kidola na nguvu za dola na hata kauli kuashiria mwananchi akitumia haki yake kikatiba na kuchagua anachokipenda kwa utashi wake, kuna hatari ya nchi kuingia machafuko na hata kumwaga damu.

Hii imetokea hata wagombea wa urasi, Ubunge na Udiwani kutoa kauli za vitisho kwa wananchi kuwa wakiacha kupigia chama fulani (hasa chama Tawala), nchi itaingiwa matatizo au hata wananchi kutishiwa kunyimwa kusikilizwa au huduma za maendeleo.

Mwaka huu pekee, Mgombea wa Chama Tawala John Magufuli na mgombea mwenza Salma Suluhu wametoa kauli za kuonyesha kuwa wananchi wakiamua kupigia vyama vingine ambavyo si CCM, basi nchi itageuka na kuwa na taswira ya nchi zilioingia vita (libya, Misri) na kuwa chama tawala-CCM kikishinda, basi waliopigia kura upinzani wawakilishi wao hawatasikilizwa wala kukaribishwa ikulu.

Hali hii ilifanyika pia wakati wa Urais wa Mkapa wakati aliyekuwa Waziri Mkuu Sumaye, alipotoa kauli mkoani Kilimanjaro kuwa wakichagua upinzani, watapoteza huduma za maendeleo na mgawanyo wa fungu la fedha kutoka Serikali kuu.

Hata Waziri Mkuu anayeondoka Mizengo Pinda alipotoa kauli yake kuwa "Wapinzani Wapigwe tuu" au Spika wa Bunge (Makinda na Ndungai) kutumia wingi wa kura za Kibunge kuzima hoja, tulikuwa tunajengewa demokrasia ya namna gani?

Je ni kwa nini ulazima huu wa kutumia vitisho kuhakikisha Chama Tawala na Ssrikali zake zinaendela kuwa madarakani?

Ukitafakari hata sheria ya Mtandao (Cyber Crime) au ya Takwimu (Statistics), zimelenga kuleta udhibiti wa nini Serikali inakitaka na kuonelea ni sawa na si uhakiki wa mambo yanayosemwa au usimamizi wa sheria na kanuni.

Leo hii, Serikali imeipa jeshi la Polisi magari zaidi ya 700 kufanya doria na ulinzi wakati wa uchaguzi, kwa nini hatushituki na kuhoji kulikoni?

Serikali hii ambayo imeendelea kusema haina fedha, imetaka kukopa benk za biashara, imeangusha shilingi kwa kukosa thamani, haina fedha za kuzalisha umeme na kupoteza mapato ya uzalishaji kutokana na umeme haba, ilipata wapi fedha kujitutumua kuhakikisha Jeshi liko tayari na Polisi?

Je kulikuwa na ulazima wa kujiimarisha kijeshi kuhakikisha demokrasia na haki ya kikatiba ya kupiga kura inafanyika kwa usalama?

Je "usalama" huu ni kulinda maslahi wa Taifa au kulinda maslahi na ustawi wa mamlaka ya Chama Tawala?

Mwaka 2000-2001 tuliona vurugu za hali ya juu Zanzibar mpaka watu walitolewa kafara walipokuwa anapigania haki yao na kuhoji kudhulumiwa haki hii.

Tumeona kwa miaka 20 sasa, CCM ikituhumiwa kutima dola na kutoa mifano ya nchi zilioingia mifarakano na umwagaji damu kuhakikisha kinaendelea kuhodhi madaraka na dhamana ya kutawala nchi (si kuongoza, bali ni kutawala na hivyo kujiita Chama Tawala)!

Tumeshuhudia malalamiko ya ukiukwaji wa haki na kukosekana na mfumo usio na upendeleo kuendesha siasa na chaguzi zetu: Tume ya uchaguzi, msajili wa vyama, mahakama, polisi, sheria za uchaguzi, serikali za mitaa, usalama wa taifa na hata katiba, vikiegemea kuipa CCM upendeleo na kuihakikishia ushindi.

Je kuna maana gani basi kuwa na uchaguzi mkuu na kuhubiri demokrasia ikiwa mfumo mzima wa uendeshaji siasa, vyama na uchaguzi unategemea ridhaa ya CCM kama chama tawala?

Leo hii Wafadhili na waangalizi wa Uchaguzi wanakuja kufanya nini cha unafiki? kuhakikisha haki inatendeka au kuhakikisha usalama wa maslahi yao unatunzwa?

Leo watendaji wa CCM wanapotoa kauli na kufanya vitendo vya kusema hata kwa goli la mkono ikiwa ni kuashiria hata kwa dhuluma na si uhalali lazima CCM ishinde kunatupa Watanzania hisia gani?

Najiuliza, je kama katiba yetu ingekuwa thabiti na isiyo ya upendeleo, kama tume yta uchaguzi ingekuwa huru, kama Polisi, Mahakama, Usalama wa Taifa na Jeshi vingekuwa vyombo huru na si vijakazi wa Chama Tawala (urithi wa mfumo wa chama kimoja), leo tungekuwa na kutokuaminiana na hata kuwa na haja ya kutenga fungu la fedha kudumisha dola ya CCM na si kuzitumia fedha hizi kwa shughuli za maendeleo na kutatua kero za wananchi kama maji safi, zahanati na elimu?

Je magari haya 700 ya polisi yangeweza kujenga visima vingapi katika vijiji vyetu vyote?

Je magari haya 700 na ushee ya polisi kutishia watu yangeweza kutupatia magari mangapi ya kubebea wagonjwa au zimamoto?

Je magari haya 700 gharama yake ingeweza kutujengea vituo vingapi vya afya vidogo vidogo pamoja na zana kutoa huduma za msingi na kwanza za kiafya kuhakikisha kinga na si tiba?

Najiuliza zawadi hii kwa polisi kama ni takrima ya shukrani na kuwakumbusha Polisi kuwa CCM ni baba na mama yao na wajibu wao wa utiifu ni kwa CCM na si katiba ya nchi?

Jeshi letu lilipozawadiwa vifaa vipya vya kijeshi na hata leo kuzinduliwa ujenzi wa kuboresha kituo cha kijeshi Ngerengere ni kurubuni utii wa Jeshi kwa chama Tawala?

Je Katiba yetu, ingekuwa ni yenye demokrasia ya kweli kama wananchi walivyopendekeza (Rasimu ya Katiba ya Warioba), tume ya uchaguzi ingekuwa huru na mchakato mzima wa uchaguzi ungefanyika kwa umakini na haki, kungekuwa na ulazima wa wananchi kuambiwa wahakikishe wanalinda kura na kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura kulinda haki zao?

Je tume ya uchaguzi ingejiendesha bila utata wa Daftari la kupiga kura, uandikishaji wa upiga kura, uhgakiki, usalama na usimamizi wa kupiga kura, haki na usawa wa kutangaza matokeo ya kupiga kura je tungekuwa tunaitilia mashaka ya kuweka kambi ya mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura?

je leo hii tunapoona wagombea wa Chama Tawala wakitoa kauli chafu bila kukemewa lakini vyama vya upinzani wakikemewa na tume ya uchaguzi kwa kauli, aina ya kampeni au vipeperushi tunajiuliza upendeleo huu ni wa nini?

Tulipoona Red brigade ya Chadema au Vikosi vya ulinzi CUF, wakijijenga ilikuwa ni kwa ajili ya nini? ikiwa wao wanashurtishwa kufuta "vikosi" lakini Green Guard wa CCM wana nguvu kuliko hata polisi na wakuu wa Wilaya, hatuoni kuwa tuna tatizo la msingi?

Leo kauli za uchochezi mpaka kufikia Jeshi kuwa mguu sawa na batalioni kusambazwa kila kona ya nchi, je tunajilidna dhidi ya adui gani? Adui demokrasia?

Leo halaiki za ukakamavu na ubora wa vyombo vya ulinzi na usalama ni kuhitimisha na kukamilisha mbegu chafu iliyopandwa kwenye vichwa vya Watanzania kuwa wakichagua Upinzani badala ya Chama Tawala CCM nchi itachafuka?

Leo wagombea wa CCM waliokuwa na madaraka ya Kiserikali wanapotumia madaraka hayo kuabudiwa majimboni mpaka kuitwa Nkurunzinza (Mwakyembe Kyela, na wenginewe), kunatupa picha gani?

Ni taswira gani tunaipanda kwenye vichwa na mawazo ya watoto na vijana wetu watakaopiga kura siku za baadae? Tunajenga taifa la namna gani lenye kujaa vitisho na kuhalalisha utawala wa mabavu?

Je ni kwa miaka na chaguzi ngapi vyama vya upinzani viendelee kuishi kwa woga au kujilinda kishari na kueneza imani ya kutoiamini Serikali na Chama Tawala CCM?

Je ni gharama gani tumetumia mpaka sasa kulihujumu Taifa na Watanzania haki yao ya kidemokrasia kudumisha mfumo dume na dola wa Chama tawala CCM?

Je ni gharama gani za kibajeti na kifedha Serikali imeingina na itaingia na kuminya kodi zetu kujihakikishia ushindi na utawala wa kudumu badala ya kuunda mazingira safi na mfumo bora wa kusimamia haki ya kidemokrasia kwa mujibu wa katiba?

Ni damu nyingi kiasi gani na roho ngapi zipotee kutetea haki hii ya kuzaliwa?

MASHABIKI WA LOW.... tumechoka kusikia kulia lia kwenu. rais wa nchi akiimarisha ulinzi wa nchi anavuja mali za uma. akiacha kufanya hivyo jeshi letu liko hoi yani kilakinachofanywa na serikali hakuna kilichofanyika kwa miaka 50 tumechoka na malalamishi yenu yaani kila kitu kinachofanyika ni tabu tupu...

Aaahh...!!!
 
CCM ni ya KISHETANI na tumeongozwa na mashetani kwa muda mrefu leo hii polisi haijitambui kama vilevile CCM isivyojitambua tarehe 25 ni siku ya ukombozi kwa watanzania.
 
Acha hofu mkuu, rais JK ni mtu wa demokrasia sana sema kuna majitu yanayomzunguka ndiyo yanamuharibia na kumpa presha; rejea issue ya Katiba mpya. Jana kaongea kauli ya kidemokrasia, kwamba yuko tayari kukabidhi nchi kwa rais yeyote yule atakayeshinda. Penye kusifia tusifie, penye kukosoa tukosoe.

Kumbuka ni huyu JK aliwaambia CCM wenzake kule Dodoma kuwa, "Wajiandae kisaikolojia kwani wanaweza kung'oka." Kwa hiyo yeye amekwisha jiandaa kisaikolojia tyr, wito wangu ni kwa ccm wengine waige mfano wa rais wetu.

Binafsi, naamini JK hatatuangusha kwa kukataa kuruhusu upinzani kuingia ikulu. Hiki ni kipimo chake cha mwisho kidemokrasia ili atwae tuzo ya Mo. Ibrahim.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Ukawa.

Heri ya wewe kuna UKAWA wengine wana akili.
 
Natatizwa sana kuona Serikali ya KIkwete ikijiimarisha "kiulinzi" kupitia Jeshi, Polisi na hata Usalama wa Taifa eti kudhibiti na kuzuia machafuko wakati wa uchaguzi mkuu.

Serikali imeweka majesho yote kwenye Red alert, polisi wamekabidhiwa magari mmapya zaidi ya 700 leo na yanasambazwa nchi nzima.

Najiuliza, hatua hizi za kuonyesha ukakamavu na uimara wa ulinzi leo hii ambapo tunakaribia kutimiza haki yetu ya kidemokrasia na kikatiba inatokana na nini?

Iweje ghafla kuwe na umuhimu wa kuhakikisha ulinzi na usalama uko imara zaidi kwa tendo la kuaminiana na linalohitaji amani, busara na hekima kuhakikisha katiba yetu na demkorasia tunayo ihubiri na kujisifia kuwa na amani, utulivu na mshikamano ni kitu cha kweli na si ulaghai na kiini macho?

Ni kitu gani hasa ambacho si sahihi na kina walakini kufikia hatua wananchi wanaweza kukosa imani na utiifu kuanzisha fujo na Serikali kuonelea ulazima wa kutunisha misuli "kudhibiti" amani?

Najiuliza ni wapi tumekosea kwamba Serikali na hasa Chama Tawala kukosa kuaminika kwa wale ambao si wafuasi wa Chama Tawala?

Je ni nchi ya namna gani tunaijenga inapofikia Serikali iliyoko madarakani inaonekana imejenga mazingira yasiyo ya haki, demokrasia na utu kwa manufaa ya Taifa na kuwa na upendeleo au kulazimisha Chama kilichoko madarakani kitumie dola kujihakikishia muendelezo wa utawala wake?

Hisia za hujuma zilizoonyeshwa katika chaguzi zilizopita zimepuuziwa. Mazingira ya rushwa yameendela. Vitisho vya kidola na nguvu za dola na hata kauli kuashiria mwananchi akitumia haki yake kikatiba na kuchagua anachokipenda kwa utashi wake, kuna hatari ya nchi kuingia machafuko na hata kumwaga damu.

Hii imetokea hata wagombea wa urasi, Ubunge na Udiwani kutoa kauli za vitisho kwa wananchi kuwa wakiacha kupigia chama fulani (hasa chama Tawala), nchi itaingiwa matatizo au hata wananchi kutishiwa kunyimwa kusikilizwa au huduma za maendeleo.

Mwaka huu pekee, Mgombea wa Chama Tawala John Magufuli na mgombea mwenza Salma Suluhu wametoa kauli za kuonyesha kuwa wananchi wakiamua kupigia vyama vingine ambavyo si CCM, basi nchi itageuka na kuwa na taswira ya nchi zilioingia vita (libya, Misri) na kuwa chama tawala-CCM kikishinda, basi waliopigia kura upinzani wawakilishi wao hawatasikilizwa wala kukaribishwa ikulu.

Hali hii ilifanyika pia wakati wa Urais wa Mkapa wakati aliyekuwa Waziri Mkuu Sumaye, alipotoa kauli mkoani Kilimanjaro kuwa wakichagua upinzani, watapoteza huduma za maendeleo na mgawanyo wa fungu la fedha kutoka Serikali kuu.

Hata Waziri Mkuu anayeondoka Mizengo Pinda alipotoa kauli yake kuwa "Wapinzani Wapigwe tuu" au Spika wa Bunge (Makinda na Ndungai) kutumia wingi wa kura za Kibunge kuzima hoja, tulikuwa tunajengewa demokrasia ya namna gani?

Je ni kwa nini ulazima huu wa kutumia vitisho kuhakikisha Chama Tawala na Ssrikali zake zinaendela kuwa madarakani?

Ukitafakari hata sheria ya Mtandao (Cyber Crime) au ya Takwimu (Statistics), zimelenga kuleta udhibiti wa nini Serikali inakitaka na kuonelea ni sawa na si uhakiki wa mambo yanayosemwa au usimamizi wa sheria na kanuni.

Leo hii, Serikali imeipa jeshi la Polisi magari zaidi ya 700 kufanya doria na ulinzi wakati wa uchaguzi, kwa nini hatushituki na kuhoji kulikoni?

Serikali hii ambayo imeendelea kusema haina fedha, imetaka kukopa benk za biashara, imeangusha shilingi kwa kukosa thamani, haina fedha za kuzalisha umeme na kupoteza mapato ya uzalishaji kutokana na umeme haba, ilipata wapi fedha kujitutumua kuhakikisha Jeshi liko tayari na Polisi?

Je kulikuwa na ulazima wa kujiimarisha kijeshi kuhakikisha demokrasia na haki ya kikatiba ya kupiga kura inafanyika kwa usalama?

Je "usalama" huu ni kulinda maslahi wa Taifa au kulinda maslahi na ustawi wa mamlaka ya Chama Tawala?

Mwaka 2000-2001 tuliona vurugu za hali ya juu Zanzibar mpaka watu walitolewa kafara walipokuwa anapigania haki yao na kuhoji kudhulumiwa haki hii.

Tumeona kwa miaka 20 sasa, CCM ikituhumiwa kutima dola na kutoa mifano ya nchi zilioingia mifarakano na umwagaji damu kuhakikisha kinaendelea kuhodhi madaraka na dhamana ya kutawala nchi (si kuongoza, bali ni kutawala na hivyo kujiita Chama Tawala)!

Tumeshuhudia malalamiko ya ukiukwaji wa haki na kukosekana na mfumo usio na upendeleo kuendesha siasa na chaguzi zetu: Tume ya uchaguzi, msajili wa vyama, mahakama, polisi, sheria za uchaguzi, serikali za mitaa, usalama wa taifa na hata katiba, vikiegemea kuipa CCM upendeleo na kuihakikishia ushindi.

Je kuna maana gani basi kuwa na uchaguzi mkuu na kuhubiri demokrasia ikiwa mfumo mzima wa uendeshaji siasa, vyama na uchaguzi unategemea ridhaa ya CCM kama chama tawala?

Leo hii Wafadhili na waangalizi wa Uchaguzi wanakuja kufanya nini cha unafiki? kuhakikisha haki inatendeka au kuhakikisha usalama wa maslahi yao unatunzwa?

Leo watendaji wa CCM wanapotoa kauli na kufanya vitendo vya kusema hata kwa goli la mkono ikiwa ni kuashiria hata kwa dhuluma na si uhalali lazima CCM ishinde kunatupa Watanzania hisia gani?

Najiuliza, je kama katiba yetu ingekuwa thabiti na isiyo ya upendeleo, kama tume yta uchaguzi ingekuwa huru, kama Polisi, Mahakama, Usalama wa Taifa na Jeshi vingekuwa vyombo huru na si vijakazi wa Chama Tawala (urithi wa mfumo wa chama kimoja), leo tungekuwa na kutokuaminiana na hata kuwa na haja ya kutenga fungu la fedha kudumisha dola ya CCM na si kuzitumia fedha hizi kwa shughuli za maendeleo na kutatua kero za wananchi kama maji safi, zahanati na elimu?

Je magari haya 700 ya polisi yangeweza kujenga visima vingapi katika vijiji vyetu vyote?

Je magari haya 700 na ushee ya polisi kutishia watu yangeweza kutupatia magari mangapi ya kubebea wagonjwa au zimamoto?

Je magari haya 700 gharama yake ingeweza kutujengea vituo vingapi vya afya vidogo vidogo pamoja na zana kutoa huduma za msingi na kwanza za kiafya kuhakikisha kinga na si tiba?

Najiuliza zawadi hii kwa polisi kama ni takrima ya shukrani na kuwakumbusha Polisi kuwa CCM ni baba na mama yao na wajibu wao wa utiifu ni kwa CCM na si katiba ya nchi?

Jeshi letu lilipozawadiwa vifaa vipya vya kijeshi na hata leo kuzinduliwa ujenzi wa kuboresha kituo cha kijeshi Ngerengere ni kurubuni utii wa Jeshi kwa chama Tawala?

Je Katiba yetu, ingekuwa ni yenye demokrasia ya kweli kama wananchi walivyopendekeza (Rasimu ya Katiba ya Warioba), tume ya uchaguzi ingekuwa huru na mchakato mzima wa uchaguzi ungefanyika kwa umakini na haki, kungekuwa na ulazima wa wananchi kuambiwa wahakikishe wanalinda kura na kukaa mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura kulinda haki zao?

Je tume ya uchaguzi ingejiendesha bila utata wa Daftari la kupiga kura, uandikishaji wa upiga kura, uhgakiki, usalama na usimamizi wa kupiga kura, haki na usawa wa kutangaza matokeo ya kupiga kura je tungekuwa tunaitilia mashaka ya kuweka kambi ya mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura?

je leo hii tunapoona wagombea wa Chama Tawala wakitoa kauli chafu bila kukemewa lakini vyama vya upinzani wakikemewa na tume ya uchaguzi kwa kauli, aina ya kampeni au vipeperushi tunajiuliza upendeleo huu ni wa nini?

Tulipoona Red brigade ya Chadema au Vikosi vya ulinzi CUF, wakijijenga ilikuwa ni kwa ajili ya nini? ikiwa wao wanashurtishwa kufuta "vikosi" lakini Green Guard wa CCM wana nguvu kuliko hata polisi na wakuu wa Wilaya, hatuoni kuwa tuna tatizo la msingi?

Leo kauli za uchochezi mpaka kufikia Jeshi kuwa mguu sawa na batalioni kusambazwa kila kona ya nchi, je tunajilidna dhidi ya adui gani? Adui demokrasia?

Leo halaiki za ukakamavu na ubora wa vyombo vya ulinzi na usalama ni kuhitimisha na kukamilisha mbegu chafu iliyopandwa kwenye vichwa vya Watanzania kuwa wakichagua Upinzani badala ya Chama Tawala CCM nchi itachafuka?

Leo wagombea wa CCM waliokuwa na madaraka ya Kiserikali wanapotumia madaraka hayo kuabudiwa majimboni mpaka kuitwa Nkurunzinza (Mwakyembe Kyela, na wenginewe), kunatupa picha gani?

Ni taswira gani tunaipanda kwenye vichwa na mawazo ya watoto na vijana wetu watakaopiga kura siku za baadae? Tunajenga taifa la namna gani lenye kujaa vitisho na kuhalalisha utawala wa mabavu?

Je ni kwa miaka na chaguzi ngapi vyama vya upinzani viendelee kuishi kwa woga au kujilinda kishari na kueneza imani ya kutoiamini Serikali na Chama Tawala CCM?

Je ni gharama gani tumetumia mpaka sasa kulihujumu Taifa na Watanzania haki yao ya kidemokrasia kudumisha mfumo dume na dola wa Chama tawala CCM?

Je ni gharama gani za kibajeti na kifedha Serikali imeingina na itaingia na kuminya kodi zetu kujihakikishia ushindi na utawala wa kudumu badala ya kuunda mazingira safi na mfumo bora wa kusimamia haki ya kidemokrasia kwa mujibu wa katiba?

Ni damu nyingi kiasi gani na roho ngapi zipotee kutetea haki hii ya kuzaliwa?

Umeandika mambo mengi lkn nakujibu kwamba ukiwa raia mwema hakuna mahali ambapo utakumbana na Jeshi letu, haya yote Serikali yetu inayoyafanya ni kutulinda raia wema dhidi ya watu wabaya kama fisadi Lowasa, Mbowe Tundu Lisu & Co.!
 
CCM ni ya KISHETANI na tumeongozwa na mashetani kwa muda mrefu leo hii polisi haijitambui kama vilevile CCM isivyojitambua tarehe 25 ni siku ya ukombozi kwa watanzania.

Hapo umeongea Mkuu, Tarehe 25 tunamuingiza Raisi wetu mpya Dr.Pombe Magufuli, Ubarikiwe sana kwa kuliona hilo!
 
Huwa naheshimu sana mawazo yako hapa JF, lakini naona leo umekwenda nje ya msitari. Vipaumbele vya nchii hii pendwa ni vipi? Leo tunadhindwa kudhibiti kipindupindu Dar, still pesa tunaongeza magari ya maji ya kuwasha! Mwananyamala na Amana hospitalini akina mama hawana hata gloves za kuwasaidia kujifungua, tuonaongeza landruiser za kubebea FFU na mabomu. Serious? Polisi wenyewe hawana nyumba za kutosha, hata hizi wanazoishi (hasa UKONGA) zimechakaa ile mbaya. Kwa nini hizo pesa zisingeboresha nyumba zao kwanza?
Tukiachilia mbali ushabiki wa kisiasa, hebu turudi kwenye basics, kweli polisi wana upungufu wa magari?

1. Nakuheshimu pia mkuu saana tu. . . .Labda nimesema usichokipenda. . . .Inatosha kuondoa heshima??!!!
2. Vipaumbele leo siku tatu zimebaki??!! Miaka tisa hatujaulizana haya mkuu?!!! Lini vilikuridhisha tangu Uhuru??!!
3. Tukiacha siasa tuanze na facts. . . .Mahitaji ya gari kwa polisi yakoje??!! Wanahitaji ngapi za aina gani na wanazo ngapi??!!

Tuanzie hapo
 
tatizo mna extramize mambo kw propagand uchwar,polis wakishindw timiz majukum yao sbb y vitendea kaz dun lawam kw serkl leo wamepew vitendea kaz lawam kw serkl sas nyie watu mko upand gan,si kwel kwmb watatawal milele chin y jua ila wakat w kuiach madarak ukifk hawatawez kupngn na ukwel
 
Wanasema usilolijua ni sawa na usiku wa gizaa. Watanzania laleni amkeni nendeni kwenye shughuli zenu lakin hamjui wapo watu hawalali wanakesha kuhakikisha ulinzi wa taifa hili. Kuna watu hawana muda wakuka na wake za na waume zao na familia zao yote ni kuhakikisha amani ya nchi hii. Kiweni na huruma watanzania laiti mngetaka kila linalojiri tz litangazwe basi ndo mngejua tz ni nchi isiyokuwa na amani. Matukio mengi yamezuia yasitoke na vyombo vya ulinzi na usalama kimya kimya. Jamani hali ni tete upande wa pili hao ukawa wana mikakati ambayo ukiijua leo unaweza kimbia nchi. Lakin vyombo hivi vimekesha kuzuia mikakati hiyo. Narudia usilolijua ni sawa na ucku wa giza. Acheni serikali ijiandae kulinda amani ya watz kutoka kwa wale wanaotaka kuichafua. Watz kuweni na hata shukurani chembe kwa vyombo vya ulinzi na usalama

Elimu ni muhimu sana nchi hii ,unataka tuwapingeze watu wanaowajibika katika shughuli zao na wanalipwa kwa kodi zetu wananchi ?.

Halafu hiyo 'AMANI'inalindwa kwa mitutu ya bunduki au kwa silaha za kivita?.Kama ni hivyo Iraq
/Afghanistan/Libya/Syria/Palestina/Israel pangekuwa na amani kweli kweli ....

Jinga were.
 
Kwani hayo magari yatakufuata nyumbani yakushambulie??!!
Hutaki Polisi wawe na vitendea kazi??!!!


Bado kuna watu wamezibwa masiko watu wanajifungulia chini hakuna vitanda lakini pesa za magari zimepatikana...na baada ya miaka 5 hayo magari yako hoi kwa kukosa service..

Mkuu jamii01


Kwa akili za Kushikiwa mtu hawezi liona hili. OLESAIDIMU Akili yake Kashikiwa na Watu
Hawezi kuliona hili
 
Last edited by a moderator:
tatizo mna extramize mambo kw propagand uchwar,polis wakishindw timiz majukum yao sbb y vitendea kaz dun lawam kw serkl leo wamepew vitendea kaz lawam kw serkl sas nyie watu mko upand gan,si kwel kwmb watatawal milele chin y jua ila wakat w kuiach madarak ukifk hawatawez kupngn na ukwel
 
Swali la kipimajoto
Je ccm inaponunua gari za polisi 777 bila kununua ambulance hata moja au kuboresha huduma za afya kwa namna yoyoye, je ni ishara kwamba nchi ina wakorofi wengi kuliko wagonjwa?

Jibu Ndio
Hapana
Sijui



Tunatakiwa kufahamu kwamba kila jambo lina umuhimu wake, mimi sioni tatizo la serikali kununua magari ya polisi. Wanaochukia hilo ni wale waarifu na wafanya fujo tu, kama ww ni raia mwema utapenda hata kuliona gari la polisi kwa sababu ya uhakika kuwa upo mahala salama.

Pia, Tanzania ina polisi chini ya 40000 na vituo vya kupiga kura vipo zaidi ya 70000 kwa maana hiyo tuna uhaba hata wa hao polisi, mimi simaanishi afya isipewe kipaumbele bali usalama kwanza maana amani ikitibuka ni vita, mkiangalia hata mataifa ya jirani kuna vurugu kutokana na uchaguz tu. Tumejua kwamba Kenya, Rwanda, Burundi, nk kuna ukabila kutokana na uchaguzi tu na si vinginevyo, usalama wetu ni muhimu na afya ni muhimu.

Zile machine za voters' ID ziligharimu 85mn dollars, equivalent to 185.47595bn za kitanzania, mbona hawakusema Serikali imepoteza hela? Si tunahitaji hyo huduma. UKAWA waambieni waache upumbavu.

Huyu anayeandika hii kusema CCM imenunua gari la polisi na sio gari la kubeba wagonjwa ni mchochez wa vurugu tu, na kama ningekuwa askari ningemkamata upesi. Tuache siasa za kuharibu amani ya nchi. Ina maana waliotoa hilo agizo ni wajinga? kila kitu kina muda wake na wala serikali haijakosea kufanya hvyo.


#CCM haijanunua ni Serikali ndo imenunua


..............................MCHAGUE MAGUFULI KWA MAENDELEO YAKO BINAFSI NA TANZANIA KWA UJUMLA.................................................
 
Sijui...............................................................................................
 
Back
Top Bottom