Wingu Jeusi la kuvunjika Amani

Wingu Jeusi la kuvunjika Amani

Ningetegemea watanzania tuwe na akili zenye maarifa nyakati hizi, hawa watu hatuwajui vema itupasavyo na ndio maana wanatulaghai tena na tena kwa siasa zao za uongo . Lakini nyakati na matukio yanayotupa nafasi kuwafahamu vizuri bado tunajifanya vipofu tusioelewa! Sasa ndio muda pekee wa kujua kuwa hao ni wauaji na sio wauaji tu waoweza kumuua babaye na "vicent" bali mtu yeyote atakaekuwa kikwazo kwa uovu wao.
Wanaweza hata kuangamiza taifa zima kama itafikia siku wao wapo madarakani na taifa likaamka kuwa kikwazo cha uovu wao, haitatokea kwa bahati mbaya, bali watafanya kwa makusudi mazima . Watanzania tunapaswa kugundua kuwa Mwenyezi MUNGU ametupa neema ya kupata uamsho wa ghafula wakati hao jamaa hawajatarajia ndio maana hawanavurugu wanaweza kuanzisha kwa sasa ila kufanya ugumu wa chinichini; hii ni neema tu ya MUNGU anaelitakia amani taifa letu lakini mwamko huu wa mabadiliko unaotishia maslahi ya waovu wakuu namna hiyo ungekwenda taratibu nna hakika wasingeuruhusu na wangeweza kufanya matata makuu hapa Tanzania.
Waliouawa , walioteswa , wanaoteseka na wote tunaonyimwa haki na kugandamizwa ni nani ana haki zaidi ya mwenzake? Kama wamewafanya hivyo wenzetu, sie je , hawatathubutu? Tunajisahau kwa kuwa tu hayajatufika , na wao wanaufurahia ufinyu huo wa fikira zetu!
WITO WANGU NI KUWA , MABADILIKO YA GHAFULA NAMNA HII NI HEKIMA TU YA AJABU YA MUNGU KUTULINDIA AMANI YETU, AMEONA NI LAZIMA MASHETANI WASHTUKIZWE ILI WASIFANYE UOVU WA LIBYA NA IRAQ KAMA WALIVYODAI WENYEWE, SASA BASI TUTUMIE NAFASI HII VEMA KUMNG'OA ADUI HARAKA NA KWA AMANI AKIWA ANAONA HAYA HATA KUFYATUA RISASI MOJA KWETU VINGINEVYO TUTAJUTIA MILELE NAFASI HII NA TUSIJEKUMLAUMU MUNGU TENA!
Cc Mbatia, Mbowe, Mnyika,Mdee, Sumaye, Kingunge na makamanda wote hili liwe neno lenu la maonyo ya mwisho kwa watanzania tarehe hizi kabla ya uchaguzi.
 
UKAWA mtegemeeni Mungu tu. Akiwa upande wenu hakuna kitakachokuwa juu yenu. Tanzania siyo mali ya familia ya mwenyekiti wa ccm. Hatutamwaga damu maadamu tusichague viongozi kwa kutishwa.

Demokrasia ni zaidi ya unafiki.
 
Serikali imewekeza pesa ktk kununua vitendea kazi ili kulinda amani ya nchi au imewekeza kuelekea kujipanga kuelekea kuvunja haki za binadamu (An investment for human rights violation)?

Kwangu mimi serikali imewekeza ili kulinda amani ya nchi, kuwalinda wananchi na mali zao. Pia, naomba tukubali kuwa magari haya na mafunzo yanyofanyika hayana impacts kwenye kipindi cha uchaguzi tu, bali vyombo hivi vya moto vitatumika baada ya uchaguzi iwe ni serikali ya Dr. John Magufuli au Ndugu Edward Lowassa.

Vyombo hivi vitaelekea kuvunja haki za binadamu au kuchochea machafuko endapo hekima na busara za kibinadamu kati ya watawala, askari na wananchi hazitatumika kwa kufuata sheria za nchi na maadili ya kazi.

Hivyo basi ni rai yangu kwa watanzania wenzangu kuwaombeni kudumisha amani, watawala tafadhalini sana tena sana- ni wazi kuwa mngependa kuona chama chenu kinashinda labda kwa mapenzi mema au masalahi binafsi, hivyo acheni haki itendeke na uhuru uwepo, waacheni wananchi waamue. Askari wetu na vijana wetu naombeni kutenda kwa haki ingawa mwatenda kazi kwa amri.
 
Wananchi watapiga kura kwa lowassa na hao makitu majeshi ccm yaje yakutane na nguvu ya umma.


swissme
 
Inatisha.
Ni dhahiri vitendea kazi hivi vimeletwa ili mosi kulinda maslai ya chama na pili kutishia wapiga kura.
Walikuwa wapi kuagiza haya magari ili kuipa polisi nguvu kukabiliana na vitendo vya uhalifu vinavyotokea kila kona ya nchi hii?
Ikitokea Chama tawala kinaanguka haya ndo magari yatakayotumika kufanya Ukurunziza.
 
Kwani hayo magari yatakufuata nyumbani yakushambulie??!!
Hutaki Polisi wawe na vitendea kazi??!!!

Wangejaribu kusahihisha huu uchafu waliotufanyia
1. Wanawake kujifungulia Sakafuni

2. Watoto kusomea chini ya Miti

3. Watumishi kulipwa mishahara ya Hadaa

4. Twiga kupandishwa kwenye Ndege

5. wizi wa ESCROW

6. Ufisadi wa EPA

7. Ufisadi wa RICHMOND

8. Ujangili Uliokithiri

9. Mikataba Mobovu ya Dhahabu

10. Mikataba mibovu kwenye Tanzanite

11. Mikataba mibovu kwenye Almasi

12. Ubinafsishaji wa Bandari, ATC, Mashamba yaNAFCO, VIWANDA, NBC nk

13. Huduma duni za Afya

14. Huduma Mbovu za Elimu

15. Ukosefu wa Maji

16. Ukosefu wa Umeme wa Uhakika

17. Gharama kubwa za Umeme

18. Kupanda kwa Bei ya Mafuta ilhali inashuka kwenye soka la Dunia

19. Gharama kubwa za vifurushi vya simu za mkononi

20. Wawekezaji kutokulipa kodi

21. Rais kusaini cheque kwa dhehebu moja

22. Pengo la kukataa Rasimu ya Katiba mpya

23. Ubovu wa barabara

24. Kugawana Nyumba za Serikali

25. Mauaji ya Daudi Mwangosi

31. Mkaahapa kujimilikisha mgodi wa Kiwira

32. Yusuf Marope kutumia Bilioni 5 uchaguzimdogo wa Tarime

33. Ufisadi wa Deep Green
34. Ufisadi wa Meremeta

35. Mabomu ya Arusha

36. Uvamizi wa vituo vya Police

37. Ununuzi wa Mv Dar es Salaam kifisadi

38. Mabehewa Feki ya Treni –

39. Ununuzi wa Ndege ya Rais

40. Mikataba 17 ya kichina

41. Kushamiri kwa biashara ya Sembe (madawa ya kulevya)

42. Usafirishaji wa Meno ya Tembo

ningewasifu sana lakini sio kuleta magari ya washa washa, sasa waje wawapige hao watu tunajua wanapokaa, yani hapa chuki za polisi na raia zitakuwa ni nyingi sana
 
Serikali imewekeza pesa ktk kununua vitendea kazi ili kulinda amani ya nchi au imewekeza kuelekea kujipanga kuelekea kuvunja haki za binadamu (An investment for human rights violation)?

Kwangu mimi serikali imewekeza ili kulinda amani ya nchi, kuwalinda wananchi na mali zao. Pia, naomba tukubali kuwa magari haya na mafunzo yanyofanyika hayana impacts kwenye kipindi cha uchaguzi tu, bali vyombo hivi vya moto vitatumika baada ya uchaguzi iwe ni serikali ya Dr. John Magufuli au Ndugu Edward Lowassa.

Vyombo hivi vitaelekea kuvunja haki za binadamu au kuchochea machafuko endapo hekima na busara za kibinadamu kati ya watawala, askari na wananchi hazitatumika kwa kufuata sheria za nchi na maadili ya kazi.

Hivyo basi ni rai yangu kwa watanzania wenzangu kuwaombeni kudumisha amani, watawala tafadhalini sana tena sana- ni wazi kuwa mngependa kuona chama chenu kinashinda labda kwa mapenzi mema au masalahi binafsi, hivyo acheni haki itendeke na uhuru uwepo, waacheni wananchi waamue. Askari wetu na vijana wetu naombeni kutenda kwa haki ingawa mwatenda kazi kwa amri.

Mzaramo ana msemo wake unaosema kusoma hujui hata picha huoni, fikiria marehemu mwangosi ni kipi alichofanya mpaka wakawanya mwili wake namna ile, kuna mambo mengi ya kufanya kutupa motisha watz lakini sio kuleta magari haya ya washa washa, wanatutia hasira wananchi tu, juzi nilienda hospital kumuangalia rafiki yangu ambae alipata ajali niliyoyakuta huko nilishangaa nikasema haya mambo nayaona kwa mtandao kumbe ni kweli,
 
Porojo ndeeeeefu, haina kichwa wala miguu.

Ulitaka wingu za mvua ya kununuwa Thailand?
Dada FF najua mahaba yako na ccm pia najua unatokwa povu tu hapa lakini yaliyo elezwa yanagusa mtima wako.... ni mjinga pekee atakae puuzia uzi huu kwamba hamna hoja... lakini wewe najua unaatetea mkate wako.... watawala hukosa busara na hekima, humweka Mungu pembeni japo wanasali na vibaraka wao kama wewe huwapigia makofi... ila wakati ukifika utakuwa umeisha umiza wengi ila uhuru kamili utapatikana... pole dada angu.
 
Bado kuna watu wamezibwa masiko watu wanajifungulia chini hakuna vitanda lakini pesa za magari zimepatikana...na baada ya miaka 5 hayo magari yako hoi kwa kukosa service..
Unafakiri pakichafuka hapa utaweza kumpa mimba mkeo? Usalama kwanza kujifungulia kitandani baadaye!
 
Suala la amani na usalama wa nchi halina mjadala.hata wanunue gari 3000 lakini kama ni kwa kulinda usalama wetu poa tu.ni mhalifu tu ndie atakaeogopa polisi kupata vifaa vya kisasa
 
Suala la amani na usalama wa nchi halina mjadala.hata wanunue gari 3000 lakini kama ni kwa kulinda usalama wetu poa tu.ni mhalifu tu ndie atakaeogopa polisi kupata vifaa vya kisasa

Amani ipi wakati watu wanashida kibao
 
Mkuu nimeipenda sana mada yako.... iko level tofauti.... najua hata magamba watajifanya mioyo yao migumu tu lakini ukweli wanauona maana wanasali ... imejibu kwa nn watu walinde kura mita 200 na tutasogea karibu kadri muda unavo enda... Martin Luther King alisema. "Utekelezaji mzuri wa sheria mbaya ni kuzivunja"... tutafanya hivo mwaka huu na tuone kama wana uwezo wa kudeal nasi malofa wote.... tutalinda kura, tutavunja amri ya kuto kaa mita 200 maana ni katika amri mbovu.... hatutaki tupendelewe bali tupewe haki.... aliye shinda atangazwe mshindi hata kama wote wametoka ccm.... ila mshindi wa haki.... analysis yako ni level ya PhD ahsante mkuu.....
 
Sugu aliomba magari mia tano wayap
eleke mbeya hope yataenda
 
kama polisi wanajua kulinda amani, usalama na mali za taifa kwa nini wasingeanza na kumkamata magufuri na kumwajibisha ipasavyo, kuna ubadhilifu mkubwa sana wa mabilioni ya fedha kwenye wizara yake kwenye malipo wa wakandarasi
 
Porojo ndeeeeefu, haina kichwa wala miguu.

Ulitaka wingu za mvua ya kununuwa Thailand?

msukule wa ccm at work,
poor you,
wana kura yako moja tu humu,
ccm ni ileile men!!
hambadiliki!!; keh!!!!
 
Back
Top Bottom