Wimbo wa Sauti Sol Nerea

Wimbo wa Sauti Sol Nerea

nchelegwanzingi

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2013
Posts
468
Reaction score
277
Licha ya kuwa ni wimbo mzuri wenye mpangilio wasauti na waimbaji,pia una ujumbe muhimu sana kwenye jamii yetu,
Hivi tumekwisha kaa tukawaza kuwa kutoa mimba pia ni kosa na ni dhambi kubwa sana,
Kwanini tuwauwe watoto wetu wakiwa tumboni? Hatujui watakuja kuwa kina nani hapa duniani, wengi wetu tunadhani mtoto akiwa tumboni hahisi maumivu yoyote, laaa anahisi maumivu sana tu lakini uwezo wa kusema ndio hana,

Dada zangu, kaka zangu, ndugu zangu kwa pamoja tupinge kabisa suala hili la kutoa mimba,
 
Hupo sahihi kiongozi,mtoto anatambulika tumboni tangia wiki nane
 
Licha ya kuwa ni wimbo mzuri wenye mpangilio wasauti na waimbaji,pia una ujumbe muhimu sana kwenye jamii yetu,
Hivi tumekwisha kaa tukawaza kuwa kutoa mimba pia ni kosa na ni dhambi kubwa sana,
Kwanini tuwauwe watoto wetu wakiwa tumboni? Hatujui watakuja kuwa kina nani hapa duniani, wengi wetu tunadhani mtoto akiwa tumboni hahisi maumivu yoyote, laaa anahisi maumivu sana tu lakini uwezo wa kusema ndio hana,

Dada zangu, kaka zangu, ndugu zangu kwa pamoja tupinge kabisa suala hili la kutoa mimba,
Mleta thread ame-assume kwamba wasomaji wana ufahamu juu ya huo wimbo ie mwimbaji na maudhui nk.Assumption hiyo inaharibu kabisa uzito wa thread. Mleta thread hajanitendea mimi msomaji haki.
 
kuna situation ambazo ni bora kutoa kuliko kuzaa!
 
Mods kwanini mmebadili heading yangu bila kunipa maelezo ya kubadili? Mnafahamu nilichokuwa nimekusudia watu kiwafikie cc Invisible Paw
 
Last edited by a moderator:
kuna situation ambazo ni bora kutoa kuliko kuzaa!

Hakuna ubora wenye kuhalalisha kuuwa ndugu yangu, Hivi hizo situation zingewafikia wazazi wako Leo ungekuwa wapi? Au ni bora kwa sababu unapumua?
 
Mleta thread ame-assume kwamba wasomaji wana ufahamu juu ya huo wimbo ie mwimbaji na maudhui nk.Assumption hiyo inaharibu kabisa uzito wa thread. Mleta thread hajanitendea mimi msomaji haki.

Unaweza kunielewesha sijakuelewa ndugu yangu, haki ipi sijakutendea?
 
Vifaa vya kutolea mimba vipo mahospitalini ili ikitokea mtoto atazaliwa na complication basi atolewe
 
weka huo wimbo,wengine hatuufahamu so tunakosa cha kuchangia kupitia maudhui ya wimbo huo
 
Kuna mauaji ambayo watu wanayafanya bila hata kufikiri kuwa wanafanya mauaji na wanadhambi ya kuuwa. Mfano mwengine watu wenye kuwapiga wezi hadi kuuwa,sidhani kama wanapofanya vile mtu anakumbuka kuwa mie nimeua.
 
Vifaa vya kutolea mimba vipo mahospitalini ili ikitokea mtoto atazaliwa na complication basi atolewe

Mkuu inapotokea jambo kama hilo hakuna hila, lakini mimba za kwetu huku uswahilini na huko uzunguni sio kama hizo unasema
 
Hakuna ubora wenye kuhalalisha kuuwa ndugu yangu, Hivi hizo situation zingewafikia wazazi wako Leo ungekuwa wapi? Au ni bora kwa sababu unapumua?

Nisingekuwapo, wala isingeniuma kwa sababu nisingejua hata kama kuna kuexist kwa sababu nisingekuwa naexist! Kwa nini hauwazii hizo sperm unazozimwaga kila siku, hujuwi ni billions minute beings unaziuwa? Naunga mkono haki ya wanawake kukataa kuzaa, hasa katika siku chache za mwanzo za ujauzito! Ni haki yao hasa inapothibitika kwamba hawataweza kulea hiko kijacho, kuliko kikaishi mazingira ya tabu na mateso ni bora kisizaliwe kabsaa.
 
Kuna mauaji ambayo watu wanayafanya bila hata kufikiri kuwa wanafanya mauaji na wanadhambi ya kuuwa. Mfano mwengine watu wenye kuwapiga wezi hadi kuuwa,sidhani kama wanapofanya vile mtu anakumbuka kuwa mie nimeua.

Maneno yako ni sawa kabisa ndugu yangu,

Nina rafiki yangu aliwahi kuowa miaka ya nyuma akapata watoto 2 wa kiume, baada ya hapo aliachana na wife wake, kipindi yuko single alimpa mimba dada fulani, mwisho waliafikiana yule bint atoe mimba jamaa alimpa pesa kabisa, baadae yule bint akabadili mawazo akasema sitoi, jamaa hakukasirika wala nini alimwambia tu nitakusaidia malezi na mengine, kweli akajifungua mtoto wa kike, baadae yule bint aliolewa na jamaa mwingine, na jamaa aliowa mke mwingine lakini alimweleza mkewe kuhusu yule mtoto wake wa nje,
Jamaa kwa mkewe kapata watoto 2 wengine wote wa kiume, sasa aliwahi kuniambia kila akikumbuka kuhusu kutoa ile pesa ili yule bint atoe mimba basi huwa analia sana, maana hawa watoto wake wa kiume wote wanampenda sana yule dada yao wa pekee, kweli huwezi kujua unaemtoa atakuja kuwa nani
 
Unaweza kunielewesha sijakuelewa ndugu yangu, haki ipi sijakutendea?
nchelegwanzingi,hujanitendea haki mimi kama msomaji wa thread yako kwa sababu umeanza thread yako kwa maneno niliyobold.Hayo maneno yanafaa kutumiwa kwa mtu anayeufahamu huo wimbo.Kwa kuwa mimi siufahamu thread yako haina maana yoyote kwangu, ndo maana nikasema hujanitendea haki mimi kama msomaji wa thread.Ningekuwa mimi ndo wewe, ningeanza na maneno ya wimbo huo kwenye ubeti unaohusika.Bila shaka sasa umenielewa ndugu au?

Licha ya kuwa ni wimbo mzuri wenye mpangilio wasauti na waimbaji,pia una ujumbe muhimu sana kwenye jamii yetu,
Hivi tumekwisha kaa tukawaza kuwa kutoa mimba pia ni kosa na ni dhambi kubwa sana,
Kwanini tuwauwe watoto wetu wakiwa tumboni? Hatujui watakuja kuwa kina nani hapa duniani, wengi wetu tunadhani mtoto akiwa tumboni hahisi maumivu yoyote, laaa anahisi maumivu sana tu lakini uwezo wa kusema ndio hana,

Dada zangu, kaka zangu, ndugu zangu kwa pamoja tupinge kabisa suala hili la kutoa mimba,
 
Last edited by a moderator:
Naupenda sana huu wimbo I wish ifike stage wanaume wasikatae mimba zao na wadada pia wakubali matokeo pindi wapatapo mimba na si kukimbilia kutoa
 
Unaweza kunielewesha sijakuelewa ndugu yangu, haki ipi sijakutendea?
nchelegwanzingi,hujanitendea haki mimi kama msomaji wa thread yako kwa sababu umeanza thread yako kwa maneno niliyobold.Hayo maneno yanafaa kutumiwa kwa mtu anayeufahamu huo wimbo.Kwa kuwa mimi siufahamu thread yako haina maana yoyote kwangu, ndo maana nikasema hujanitendea haki mimi kama msomaji wa thread.Ningekuwa mimi ndo wewe, ningeanza na maneno ya wimbo huo kwenye ubeti unaohusika.Bila shaka sasa umenielewa ndugu au?

Licha ya kuwa ni wimbo mzuri wenye mpangilio wasauti na waimbaji,pia una ujumbe muhimu sana kwenye jamii yetu,
Hivi tumekwisha kaa tukawaza kuwa kutoa mimba pia ni kosa na ni dhambi kubwa sana,
Kwanini tuwauwe watoto wetu wakiwa tumboni? Hatujui watakuja kuwa kina nani hapa duniani, wengi wetu tunadhani mtoto akiwa tumboni hahisi maumivu yoyote, laaa anahisi maumivu sana tu lakini uwezo wa kusema ndio hana,

Dada zangu, kaka zangu, ndugu zangu kwa pamoja tupinge kabisa suala hili la kutoa mimba,
 
Last edited by a moderator:
Ni wimbo mzuri,ila naona historia ya Afrika imepotoshwa pale wimbo unaposema "Mandela ni mkombozi wa Afrika". Inajulikana wazi kabisa wakombozi wa Afrika ni kina Kwame Nkurumah, Mwalimu Nyerere, na Mandela ni uzao wa harakati za hawa watu.
 
nchelegwanzingi,hujanitendea haki mimi kama msomaji wa thread yako kwa sababu umeanza thread yako kwa maneno niliyobold.Hayo maneno yanafaa kutumiwa kwa mtu anayeufahamu huo wimbo.Kwa kuwa mimi siufahamu thread yako haina maana yoyote kwangu, ndo maana nikasema hujanitendea haki mimi kama msomaji wa thread.Ningekuwa mimi ndo wewe, ningeanza na maneno ya wimbo huo kwenye ubeti unaohusika.Bila shaka sasa umenielewa ndugu au?

Nimekupata vizuri ndugu yangu Tuko pamoja SHIEKA
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom