Izzi
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 553
- 1,107
Habari wanajukwaa,
Ikiwa ni mara ya kwanza kwa WUTz kufanyika Njombe, na nikiwa ni mmoja wa waratibu wa jukwaa hili la WUTz Kanda ya Njombe nimeona ni vyema nikilileta suala hili hapa JF. Kwanza ni kwasababu ninaamini kuna wadau wengi wenye uzoefu na fikra tunduizi za kutosha zinazoweza kutusaidia kulifanya jukwaa la WUTz2022 Kanda ya Njombe lilete tija. Pili ni namna mojawapo ya kualika wadau, hususani wabunifu kushiriki WUTz2022 - Kanda ya Njombe. Naomba nitoe dondoo kidogo kwa kifupi;
NB: Popote linapotumika neno "Ubunifu" ni kwa maana ya "Innovation". Wataalamu wa Kiswahili watatusaidia tafsiri mahsusi ya haya maneno matatu: 'Innovation', 'Invention' na 'Creativity'
WIKI YA UBUNIFU NI NINI?
Sio tukio, ni jukwaa ambalo lilianza mwaka 2015 chini ya Mfuko wa HDIF (Human Development Innovation Fund) wa UKAid, likiratibiwa na UNDP kwa kushirikiana na COSTECH. Jukwaa hili huwa lipo kila mwaka na hufanyika kwa wiki moja kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ambapo wabunifu hupata nafasi ya kuonekana, wadau hupata nafasi ya kufahamiana na kutengeneza ushirikiano, maarifa ya kutosha hushirikishwa, mambo mbalimbali ya kibunifu huoneshwa na masuala nyeti ya kisera hujadiliwa. Lengo kuu ni kuujenga mfumo wa ikolojia ya ubunifu Tanzania.
MWAKA HUU ITAFANYIKA WAPI?
Kwa mwaka huu 2022, kilele cha WUTz2022 kitakuwa Jijini Dodoma katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, kuanzia Tarehe 15 Mei mpaka Tarehe 20 Mei.
KWANINI INAITWA "KILELE"?
Kwasababu kabla ya Tarehe 15 Mei, kutakuwa na matukio mbalimbali katika mikoa 16, yatakayokuwa yanafanyika kwa nyakati tofauti tofauti kuanzia Aprili 23 Mpaka Mei 14 yote ni katika kuadhimisha WUTz katika ngazi za mikoa/kanda.
KUNA KAULI MBIU?
Ndio, WUTz2022 ina kauli mbiu (Main theme) ifuatayo: "UBUNIFU KWA MAENDELEO ENDELEVU" (Innovation for sustainable Development).
Lakini kuna 'sub-themes' 5, ambazo ni: (*Samahani nitatumia lugha ya kukopa);
WUTz2022 kanda ya Njombe itafanyika kuanzia Tarehe 8 Mei mpaka Tarehe 14 Mei, 2022 katika maeneo tofauti tofauti, kwa Halmashauri zote zilizopo katika Mkoa wa Njombe.
OK, KWAHIYO?
Nitumie fursa hii kukaribisha mawazo, ushauri, maoni kuhusu namna bora ya kulifanya jukwaa lilete tija zaidi. Ikumbukwe, jukwaa hili kwa mikoa mingi linawalenga zaidi wanafunzi wa vyuo vikuu. Kwa Mkoa wa Njombe hali ni tofauti, hatuna vyuo vikuu zaidi ya OUT - kwa sehemu kubwa walengwa wengi ni vijana na wananchi walioishia kidato cha nne, cha sita, na vyuo vya ufundi. Hivyo, tunafahamu tunahitaji kutumia mbinu tofauti za kulifanya jukwaa hili liendane na mazingira yaliyopo. Kwa mwenye mawazo, karibu sana. Lakini pia inawezekana yapo maswali, ruksa kuniswalika pia.
Pia, nitumie fursa hii kumkaribisha yeyote anayeona anaweza kufanya chochote katika WUTz2022 kanda ya Njombe; Iwe ni mbunifu, au ni muwezeshaji, au ni mdau wa namna yoyote, tunaendelea kupokea wadau ambao tutashirikiana nao ili kufanikisha tukio. Nitumie ujumbe DM au acha maoni yako hapa na mimi nitakuwa nikipita kusoma na kujibu.
NB: Tunaandaa matukio yatakayofanyika "Physically" na "Online".
Kwa sasa naomba niishie hapa, nitaendelea kuleta masasisho (updates) kadiri itakavyoonekana inafaa. Na baadae nitakuwa nikileta masasisho kuhusu WUTz2022 kwa ujumla.
Mimi... ninashukuru.
PS: Nimeambatanisha kijarida chenye taarifa kuhusu WUTz2022 kwa ujumla.
MASASISHO: Aprili 07, 2022
View attachment IWTz 2022 Open Call-01.png
View attachment IWTz 2022 Open Call II-01.png
MASASISHO: MEI 4, 2022
Ifuatayo ni mikoa inayoandaa "events" kuelekea wiki ya Ubunifu kitaifa, sambamba na Taasisi zinazohusika katika mikoa tajwa;
1. ARUSHA: Westerwelle Foundation Tanzania - Tarehe 9 - 13 Mei, 2022.
2. DODOMA: Capital Space Limited - Tarehe 15 - 20 Mei, 2022.
3. IRINGA: R-Labs - Tarehe 12 - 14 Mei, 2022.
4. MBEYA: MUST - Tarehe 9 - 13 Mei, 2022.
5. ZANZIBAR: Cube Zanzibar - Tarehe 10 - 14 Mei, 2022.
6. MTWARA: SIDO - Tarehe 13 Mei, 2022.
7. MWANZA: SIDO - Tarehe 25 - 29 Aprili, 2022
8. TANGA: Projekt Inspire Ltd - Tarehe 6 Mei, 2022.
9. MOROGORO: The Arena of Taking Charge (TAOTIC) - Tarehe 6 - 13 Mei, 2022.
10. NJOMBE: Valiant Hands of Care (VAHACA) Foundation - Tarehe 11 - 13 Mei, 2022.
11. KILIMANJARO: Kilistart - Tarehe 6 - 7 Mei, 2022.
12. KAGERA: KADETFU - Tarehe 27 - 30 Aprili 2022.
13. KIGOMA: SIDO - Tarehe 9 Mei, 2022.
14. MARA: Buhare CDTI - Tarehe 9 Mei, 2022.
15. RUVUMA: Mlale Digital Innovation Centre - Tarehe 6 Mei, 2022.
16. DAR ES SALAAM: TAI Volunteers - Tarehe 9 - 12 Mei, 2022.
Ikiwa ni mara ya kwanza kwa WUTz kufanyika Njombe, na nikiwa ni mmoja wa waratibu wa jukwaa hili la WUTz Kanda ya Njombe nimeona ni vyema nikilileta suala hili hapa JF. Kwanza ni kwasababu ninaamini kuna wadau wengi wenye uzoefu na fikra tunduizi za kutosha zinazoweza kutusaidia kulifanya jukwaa la WUTz2022 Kanda ya Njombe lilete tija. Pili ni namna mojawapo ya kualika wadau, hususani wabunifu kushiriki WUTz2022 - Kanda ya Njombe. Naomba nitoe dondoo kidogo kwa kifupi;
NB: Popote linapotumika neno "Ubunifu" ni kwa maana ya "Innovation". Wataalamu wa Kiswahili watatusaidia tafsiri mahsusi ya haya maneno matatu: 'Innovation', 'Invention' na 'Creativity'
WIKI YA UBUNIFU NI NINI?
Sio tukio, ni jukwaa ambalo lilianza mwaka 2015 chini ya Mfuko wa HDIF (Human Development Innovation Fund) wa UKAid, likiratibiwa na UNDP kwa kushirikiana na COSTECH. Jukwaa hili huwa lipo kila mwaka na hufanyika kwa wiki moja kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ambapo wabunifu hupata nafasi ya kuonekana, wadau hupata nafasi ya kufahamiana na kutengeneza ushirikiano, maarifa ya kutosha hushirikishwa, mambo mbalimbali ya kibunifu huoneshwa na masuala nyeti ya kisera hujadiliwa. Lengo kuu ni kuujenga mfumo wa ikolojia ya ubunifu Tanzania.
MWAKA HUU ITAFANYIKA WAPI?
Kwa mwaka huu 2022, kilele cha WUTz2022 kitakuwa Jijini Dodoma katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, kuanzia Tarehe 15 Mei mpaka Tarehe 20 Mei.
KWANINI INAITWA "KILELE"?
Kwasababu kabla ya Tarehe 15 Mei, kutakuwa na matukio mbalimbali katika mikoa 16, yatakayokuwa yanafanyika kwa nyakati tofauti tofauti kuanzia Aprili 23 Mpaka Mei 14 yote ni katika kuadhimisha WUTz katika ngazi za mikoa/kanda.
KUNA KAULI MBIU?
Ndio, WUTz2022 ina kauli mbiu (Main theme) ifuatayo: "UBUNIFU KWA MAENDELEO ENDELEVU" (Innovation for sustainable Development).
Lakini kuna 'sub-themes' 5, ambazo ni: (*Samahani nitatumia lugha ya kukopa);
- Green and blue innovations for a hunger-free future.
- Policy and institutional frameworks for a vibrant innovation ecosystem.
- Innovation financing for job creation.
- Inclusive digital connectivity - Leaving no one behind.
- Innovation for a future-proof education system.
WUTz2022 kanda ya Njombe itafanyika kuanzia Tarehe 8 Mei mpaka Tarehe 14 Mei, 2022 katika maeneo tofauti tofauti, kwa Halmashauri zote zilizopo katika Mkoa wa Njombe.
OK, KWAHIYO?
Nitumie fursa hii kukaribisha mawazo, ushauri, maoni kuhusu namna bora ya kulifanya jukwaa lilete tija zaidi. Ikumbukwe, jukwaa hili kwa mikoa mingi linawalenga zaidi wanafunzi wa vyuo vikuu. Kwa Mkoa wa Njombe hali ni tofauti, hatuna vyuo vikuu zaidi ya OUT - kwa sehemu kubwa walengwa wengi ni vijana na wananchi walioishia kidato cha nne, cha sita, na vyuo vya ufundi. Hivyo, tunafahamu tunahitaji kutumia mbinu tofauti za kulifanya jukwaa hili liendane na mazingira yaliyopo. Kwa mwenye mawazo, karibu sana. Lakini pia inawezekana yapo maswali, ruksa kuniswalika pia.
Pia, nitumie fursa hii kumkaribisha yeyote anayeona anaweza kufanya chochote katika WUTz2022 kanda ya Njombe; Iwe ni mbunifu, au ni muwezeshaji, au ni mdau wa namna yoyote, tunaendelea kupokea wadau ambao tutashirikiana nao ili kufanikisha tukio. Nitumie ujumbe DM au acha maoni yako hapa na mimi nitakuwa nikipita kusoma na kujibu.
NB: Tunaandaa matukio yatakayofanyika "Physically" na "Online".
Kwa sasa naomba niishie hapa, nitaendelea kuleta masasisho (updates) kadiri itakavyoonekana inafaa. Na baadae nitakuwa nikileta masasisho kuhusu WUTz2022 kwa ujumla.
Mimi... ninashukuru.
PS: Nimeambatanisha kijarida chenye taarifa kuhusu WUTz2022 kwa ujumla.
MASASISHO: Aprili 07, 2022
View attachment IWTz 2022 Open Call-01.png
View attachment IWTz 2022 Open Call II-01.png
MASASISHO: MEI 4, 2022
Ifuatayo ni mikoa inayoandaa "events" kuelekea wiki ya Ubunifu kitaifa, sambamba na Taasisi zinazohusika katika mikoa tajwa;
1. ARUSHA: Westerwelle Foundation Tanzania - Tarehe 9 - 13 Mei, 2022.
2. DODOMA: Capital Space Limited - Tarehe 15 - 20 Mei, 2022.
3. IRINGA: R-Labs - Tarehe 12 - 14 Mei, 2022.
4. MBEYA: MUST - Tarehe 9 - 13 Mei, 2022.
5. ZANZIBAR: Cube Zanzibar - Tarehe 10 - 14 Mei, 2022.
6. MTWARA: SIDO - Tarehe 13 Mei, 2022.
7. MWANZA: SIDO - Tarehe 25 - 29 Aprili, 2022
8. TANGA: Projekt Inspire Ltd - Tarehe 6 Mei, 2022.
9. MOROGORO: The Arena of Taking Charge (TAOTIC) - Tarehe 6 - 13 Mei, 2022.
10. NJOMBE: Valiant Hands of Care (VAHACA) Foundation - Tarehe 11 - 13 Mei, 2022.
11. KILIMANJARO: Kilistart - Tarehe 6 - 7 Mei, 2022.
12. KAGERA: KADETFU - Tarehe 27 - 30 Aprili 2022.
13. KIGOMA: SIDO - Tarehe 9 Mei, 2022.
14. MARA: Buhare CDTI - Tarehe 9 Mei, 2022.
15. RUVUMA: Mlale Digital Innovation Centre - Tarehe 6 Mei, 2022.
16. DAR ES SALAAM: TAI Volunteers - Tarehe 9 - 12 Mei, 2022.