Wiki Moja Sasa Bila Local Channels:Je TBC1 imekuvutia?

Wiki Moja Sasa Bila Local Channels:Je TBC1 imekuvutia?

Takribani wiki moja sasa local channel tunayopata ni TBC1, je wewe mpaka sasa kuna kipindi gani kimekuvutia?
Acha wamiliki wa kampuni nao wasome namba; akina Anthony Dialo walikuwa wanachapisha hadi habari za uongo kumhusu Mzee Lowasa ili chama kikongwe kibaki madarakani wakidhani watarudisha zama za uhuru za kina mzee Jakaya, wakatumia vyombo vyao na taaluma zao kukiweka chama dola madarakani,
Naamini wanakula hasara kwa kuwa hata matangazo ya biashara kwenye TV sasa hayana viewers wengi, MIE NILIKUWA NALIPIA KISIMBUZI ili nitazame taarifa na matukio kutoka ITV, ITV ameminywa kwenye kisimbuzi changu so sioni ulazima wa kuendelea kulipia katuni tu za watoto...!
TBC hata sifuatilii iwepo; isiwepo HAINIHUSU...
 
Naangalia Azam App matangazo yote hakuna nilikuwa naona matangazo ya Halotel na GSM Godoro ila sasa Kuna Tangazo la Juice za Azam tu(African Fruits).........
 
Sio kiushabiki lakini ni mwaka wa pili sasa sijawahi kwa hiyari yangu mwenyewe kuangalia taarifa ya Habari ya kituo chochote kile cha tv za Tanzania. Nimeelewa sasa ni kwa nini mtukanaji namba moja aliwahi kusema kwamba watanzania ni wavivu wa kufikiri!
 
Mimi nimeifutilia mbali nimeliondoa kabisa Li Tbc Lao kwenye king'amuzi changu star imes
 
kwani TBC1 ndo kitu ganii aina ya mnyama au??
 
Takribani wiki moja sasa local channel tunayopata ni TBC1, je wewe mpaka sasa kuna kipindi gani kimekuvutia?
Sijui kwanini mwanangu yupstandard iv (English medium) nikiweka TBC 1 Kwa bahati mbaya hulia sana na kama anakula huacha !!!
 
Mwambieni raisi John aje na Mbeya. Sio kila siku Mwanza tu. Tumechoka kubaguliwa wakati kodi zetu mnachukua.
Hivi mbeya kwa nn anakwepa, ili hali alikuja kuomba kura na hakupata 0 bali kuna kiasi cha kura alivuna. Kwa mfano iringa ndo maeneo aliyipata kura kiduchu lkn kafika, why not mbeya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom