Wife material

Wife material

Wewe unafikiri anatakiwa awe na zipi???
Awe na hofu ya Mungu.
Awe na mtazamo chanya katika maisha
Awe na uwezo wa kupambanua mambo kwa upana zaidi
Awe na heshima na uvumilivu
Ayabebe mapungufu yako Kama yake(ila sio usaliti)
Awe na upendo kwa jamii inayomzunguka (kuanzia vizazi vyenu Hadi kwa ndugu na wengine)
Asiwe muongeaji sana awe msikilizaji itapendeza zaidi
Mwisho ajue alama za nyakati hasa katika suala la uchumi
 
Kwangu mie wife material ni mwanamke mwenye vision alie na tabia za mke au mama, anaeweza kuishi ndani ya uwezo wa kidume bila kumsumbua, asiye wakwa na tamaa wala makuu yani anaeweza kumpenda mtu kama alivyo. Mara nyingi huwaga naspot ni wale wanawake wanaoonekana washamba flani hivi mbele ya wenzao ila wapo real na life. Wife material anaweza ishi maisha yoyote yale yanayowajia na atastick na wewe na kukupa mawazo ya kukujenga na atakutia moyo ilimradi mtoboe kimaisha hata kama mna hali ya chini sana.

Anauwezo wa kukufanya ujisikie bhakressa ijapokuwa wewe ni kapuku tu na ikitokea ana uwezo kiuchumi zaidi yako atakulindia heshima yako kama mume always na kujitahidi kuficha mapungufu yako mbele ya jamii. She will never reduce you or make you feel inferior because she's a ride or die kind of woman.

Uzuri ni variable tu anaweza kuwa mzuri sana ama kiasi alimradi akonge nafsi yako tu ila mara nyingi naonaga mvuto wa wife materials wengi huwaga ni wastani compared na wanawake wenye mvuto sana ambao wengi ndio waigizaji maisha ama slay queens.
 
Kweli kabisa ila kuna ambao ukiupata havumilii anajiangalia alivyo na anavyotongozwa anatafuta sababu ya kusepa
Wife material hakimbii ukiwa kapuku au ukiyumba kiuchumi. Anakomaa nawewe na kuchekecha akili huku na kule kuangalia fursa gani itawarudisha kwenye raiti traki kisha anakusanua huku yeye akifanya harakati yeyote ile mradi msavaivu hata kuanzisha banda la mama ntilie fasta kama emergency plan. Anaweza hata kuongea na jamaa kadhaa akakuulizia michongo sehemu nyingine na kipindi chote hiki atakutia moyo sio kukusimanga kwamba huna lolote. She understands unaumia na hali halisi kama mume.

Hapo slay queen ama mwanamke mbinafsi kama kangedere, atahamia tawi lenye matunda ili aendelee kula kwa ubua maana ushafulia huwezi kumpeleka samaki samaki, shopping wala saluni kila weekend kubandika kucha na mawigi mapya, life lime change ghafla na anaona escape plan ndio right choice ili aendelee kula maisha maana umaskini kwake mwiko na hio ni baada ya masimango ya kutosha yani, utaskia we mwanaume gani bana hapo kashasahau kwamba ulimpa maisha kinoma. Bila kujali maumivu yako utaachwa tu na wale watu waliokuwa wanamtolea macho viwanja ndio wataanza kumdokoa. Imagine mtu anaoa mke kama Tunda official kale ka bitch kanakoonekana mitandaoni kakila bata tu halafu hela zikate ghafla 🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Wacha sie tuoe wanawake halisi tu, hao ndizi kisukari tunawaachia nyie wenye uhakika na hela mpaka kifo. Tunaojua maisha ni milima na mabonde wacha tujihami kwa wife materials tu.
 
Back
Top Bottom