Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 7,554
- 15,419
Vijana wa hii nchi sio tatizoShida ni malengo, Hii nchi wananchi wake hawana malengo. Mwaka jana sijui ilitoka budget ya 692B za anunani za makazi
Mpaka leo hii sijaskia au kuona watanzania wanaonufaika na huo mradi, trca walitoa API lkn hamna IT anae zitumia na ni bure
IT wa tanzania ndo hawa wanabisha kama watoto sijui framework gani ni bora kuliko nyingi, sijui language hii ina speed kuliko nyingine
Badala wakae watengeneze mifumo, software zenyewe zimewashinda kutengeneza, wapo huku wanatafuta wanafunzi wa kuwafundisha programming ambayo wenyewe wameshidwa kuitumia
Hata iyo satellite kutiirusha inatumiwa na Mamlaka ya hali ya hewa na mzee azam kurusha matangazo ya azamTV
Vijana wa hii nchi wamelala na kupoa
Tatizo ni mazingira waliyokulia, Bongo hata elimu yetu tu ni mbovu, inaishia kumkaririsha kijana mambo yasiyo na tija kwenye maisha yake na kumpotezea muda mwingi. Unategemea huyo kijana afanye kipi kikubwa ikiwa msingi aliowekewa kupitia elimu ni mbovu?
Takribani wiki mbili zilizopita Mbeya University of Science and Technology (M.U.S.T) walifanya maonesho ya kiteknolojia juu ya ubunifu wa vijana wa chuoni hapo kwenye mambo ya kiteknolojia. Ukienda M.U.S.T pale vijana ni wabunifu sana licha ya kupata elimu duni ya Tanzania lakini cha ajabu hata lecturer wao analalamikia suala la kukosa support kutoka kwa serikali. Inaonesha suala la maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia Tanzania yanategemea zaidi siasa kuliko ujuzi. Project kibao zilizofanywa na wanachuo wa M.U.S.T zinaishia kuoneshwa kwenye maonesho watu wanazifurahia then zinakufa kwa sababu serikali haina interest na hayo mambo. Ili kukuza teknolojia hela inahitajika na ndio maana wabunifu wanashindwa kuendeleza ubunifu wao kwa sababu wamekosa financial assistance kutoka kwa government.
M.U.S.T walipeleka ubunifu fulani (nimesahau kidogo) kwenye halmashauri ya mkoa ila walikesha wakisubiri mrejesho mpaka wakachoka wao, project ikafa juu kwa juu
Sasa hivi wanaendelea na utafiti wa kubadili mabaki ya mazao ya ngano na mpunga kuwa mbadala wa cement kwenye vitu kama kupiga plaster kwenye nyumba. Wamefanikiwa kwa asilimia kadhaa ila hata wakija kumaliza utafiti wao sidhani kama watafika popote ikiwa serikali yenyewe haina hata muda nao
Usiseme vijana wa Bongo wamepoa, sema taifa ndio limepoa.
Vijana wabunifu tunao ila taifa ndio linawakwamisha. Nenda Mbeya ukajionee mwenyewe