Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,242
- 113,619
Si muda mrefu uliopita mwanamuziki nyota wa Marekani wa miondoko ya R&B, Usher Raymond, alifunguliwa mashitaka ya kumuweka kwenye hali/ mazingira hatarishi ya kumwambukiza gonjwa la zinaa mwanadada mmoja hivi baada ya kukutana naye kimwili na kumficha kuwa yeye [Usher] ni mwathirika wa ugonjwa wa malengelenge ya neva ngozini kwenye kiungo cha uzazi [genital herpes].
Mwanadada huyo anadai fidia ya mamilioni ya dola za Kimarekani.
Mwaka 2012 Usher alimlipa mwanadada mwingine fidia ya dola za Kimarekani milioni moja na ushee nje ya mahakama kwa kumwambukiza hilo gonjwa!
Sasa wamejitokeza watu wengine watatu waliopanga kumfungulia mashitaka Usher kesho Jumatatu huko kwenye jimbo la California, nchini Marekani kuhusu kutokuwaambia yeye ni mwathirika kabla ya kukutana nao kimwili.
Wawili kati yao ni wanawake na mmoja ni mwanaume. Hapo kwa mwanaume kunaibua maswali kadhaa....
Ina maana Usher yuko kotekote? Yaani anapenda wanawake na wanaume pia?
Halafu, hivi mtu unathibitishaje kuwa kweli huyu ndiye aliyeniambukiza hili gonjwa na si mwingine?
Unathibitishaje kuwa kati ya wote uliolala nao huyu ndiye aliyeniambukiza?
Hahahaaa....pole zake huyo Usher maana naamini anapitia kipindi kigumu sasa hivi.
Mwanadada huyo anadai fidia ya mamilioni ya dola za Kimarekani.
Mwaka 2012 Usher alimlipa mwanadada mwingine fidia ya dola za Kimarekani milioni moja na ushee nje ya mahakama kwa kumwambukiza hilo gonjwa!
Sasa wamejitokeza watu wengine watatu waliopanga kumfungulia mashitaka Usher kesho Jumatatu huko kwenye jimbo la California, nchini Marekani kuhusu kutokuwaambia yeye ni mwathirika kabla ya kukutana nao kimwili.
Wawili kati yao ni wanawake na mmoja ni mwanaume. Hapo kwa mwanaume kunaibua maswali kadhaa....
Ina maana Usher yuko kotekote? Yaani anapenda wanawake na wanaume pia?
Halafu, hivi mtu unathibitishaje kuwa kweli huyu ndiye aliyeniambukiza hili gonjwa na si mwingine?
Unathibitishaje kuwa kati ya wote uliolala nao huyu ndiye aliyeniambukiza?
Hahahaaa....pole zake huyo Usher maana naamini anapitia kipindi kigumu sasa hivi.