What went wrong with Harmonize

"What went wrong with Harmonize" not 'to'.
Jamaa nilikiwa namkubali sana,sababu alikuwa mtu wa kujituma.Naona alikurupuka kutoka WCB,alikuwa bado hayupo tayari kusimama kama yeye.Wasafi wapo smart na ni label wenye watu makini sana ndo maana wametoa na bado wanaendelea kutoa wanamziki na nyimbo nzuri.Ukiangalia toka Diamond wa mbagala,ray van,mbosso,Harmonize wenyewe mpaka walipofika na Zucchu ni Transformation kubwa.Wasafi wanajua jinsi ya kunoa vipaji,wanawatafutia wasanii matamasha,wanawatangaza na wanajua biashara.Harmonize alifikir kipaji pekee inatosha,akasahau kuwa inabidi aji.'re introduce' kwa washabiki wake kitu ambacho hakufanya,ndo mpaka leo ukimuangalia bado ana u diamond kila anachofanya ma hii ina 'bore' sana.Kujiita tembo inaonyesha hana ubunifu,kuvaa micheni kibao,maguo mengi ya joto,mi tatoo mwili mzima,yaani ana fanya mambo kupitiliza mpaka inachefua.Ukisikiliza nyimbo zenyewe hamna kitu,mi naona anajiangaisha sana bila matunda,yaani mambo mengi anayofanya ni upuuzi tu hamna sanaa na havimpaishi kama mwanamziki.Cha kufanya Harmonize,kwanza aache obsession yake na diamond,huyu jamaa ndo kamtoa jalalani.Atafute timu ya watu watakaomsaidia kukuza na kutangaza kipaji chake,aache kiki za ivyo,aache vijembe na a focus kwenye mziki.Asitishe kusajili wanamziki wengine ajijenge yeye kwanza,yaani apunguze spidi na ajipange yeye kwanza.Akifanya ivi,labda anaweza kueleweka kama msanii huru.
 
Kama wa2 waliomzunguka ndio Hawa unategemea nini?
Screenshot_20201119-105352~2.jpg
 
Hivyo nilidhani hili nimeliona peke yangu, nilikuwa kwa safari juzi wakawa wana play nyimbo za Harmonize, za toka kipindi anaanza music dabliusibi,

Nyimbo ni nzuri na una feel that taste kabisa, zilipoanza nyimbo zake za hivi karibuni, hapo ndiyo nikaona tofauti kubwa sana ya Harmo wa sasa na wa zamani hata kwenye mashairi tu..!

I asked myself the same question, mshkaji anakwama wapi.?
Kijana inaonekana akli yake haijatulia , alipotoka WCB alikuwa hajawa confused Sana , baada ya mda inaonekana alipata washauri wengne possibly hata maswala ya ushirikina , (kuna mda aliimba kwamba wenzake wanamroga )amekuwa confused Sana mda mwingi anaimba kujihami, anachoimba kwa sasa ni yale anayowaza na kufikria most of the time .... Kuambiwa kuwa yeye ni level moja na Diamond kunamfanya afanye vitu ili kuuaminisha uma kwamba huenda ni kweli mwisho vinakuwa oversize na vinakuwa out of control.....
 
Leaving WBC was not a problem to me. He thought he was ready to be on his own and was feeling stifled and his progress was somehow limited. He started very well with his label and was actually doing good. At the moment I think he has lost focus. He needs to concentrate on his music and move forward. These sarcasm to the people where he came from are not helping his cause and they might even lead to his downfall.
 
Anaweza Kuwa ka post hivi kwa MAPENZI ya mziki ila Pia anatimiza wajibu wake na shughuli zake kama kawaida....

Kila mtu ana hobby yake, anayoyafanya kama burudani baada ya kazi, inawezekana anapenda mziki... ana haki ya ku comment!

Usiwe mjuaji sana, hategemei kitu kutoka kwa wasanii, a napenda burudani! Wewe unapata nini kushabikia Manchester?
SAFI SANA MKUU JAMAA UJUAJI MWINGI
 
Mkuu ishi maisha yako, wazazi probably wako wanakutegemea.

Wasanii hawana time na wewe, rafiki yao ni yule mwenye pesa na madaraka.

Kwa lugha rahisi watu maarufu wote Tanzania walishajua wabongo hamnazo na hawajielewi ndio maana wano busy na mambo yao kama CCM, endorsements.

Hata ukikutwa umeyawa kikatili Ubungo, they don't care hata atakayekemea
Nina hakika mwenye post ana maisha mazuri kuliko wewe hapo
 
Hili ndio lile tamasha alilo lisema atafanya siku tatu mfululizo uwanja wa Uhuru.?

Hapo awali alisema atakuwa analisha chakula mara kwa mara ,akaanzia Karume baadaye kimya.

Akasema nitafanya show uwanja wa uhuru May 27,kimya ndio akaja na hii ya show siku tatu mfululizo Uhuru mwezi huu wa November.

Bado akanzisha Label na kutambulisha wasanii watatu,hao wote awapromoti bado na yy ajipromoti na kila siku anatoa nyimbo yy.

Wakati anazindua album alisema video zote 18 zipi tayari lkn mpaka sasa kimya wakati mule kwenye album yake ana nyimbo nzuri mfano Malaika na Rhumba baada ya kuzipromoti anatoa nyimbo hizi za mafumbo.

Atulize kichwa apangilie mambo yake mimi na amini yy ni mkali ila tatizo lake anakurupuka,akifanya masihala mziki utamshinda.
Harmoniz hana ukali wowote ni kama Kiba tu,

Yani hapo walipo ndio uwezo wao ulipoishia.
 
Harmoniz hana ukali wowote ni kama Kiba tu,

Yani hapo walipo ndio uwezo wao ulipoishia.
Kwangu mimi dogo bado mzuri,ila kadri siku zinavyo enda anazidi kupoteza focus,yaani siku hizi amekuwa mtu wa kukurupuka,hajipangi kila analolipanga haliendi na ndio maana anaishia kulalamika.

Cha msingi awe makini kama akiendelea na nyimbo zake hizi za mipasho na mafumbo huko mbele atapotea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom