What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

Millenium tower hadi shoppers plaza ndo ipi hiyo? Au unamaanisha kawe hadi shoppers?
 
Uko juu Kaka Mphamvu!! Shukrani za pekee kwa update mkuu.
PAMOJA TUTASHINDA!!
 
Mimi binafsi nimezungumza.
Nimesema kuhusu barabara ya lami nyepesi, itakayopita kwa matajiri pekee na sio kwa masikini.
Nimeshauri utaratibu wa recycling ya takataka uwekwe ili kudeal na takataka hapa Mikocheni na Tanganyika kwa ujumla.
Mwisho nimehoji mustakabali wetu as mpango wa makazi utakapofika kwetu kwa hisani ya Tibaijuka!
 
Ndugu John amezungumzia hoja ya shule ya kata kujengwa Mikocheni 'B' badala ya Mikocheni 'A'
 
Ndugu Ellias anazungumzia njia ya MIKOCHENI 'A' kuwa shorcut ya foleni na umuhimu wa kujengwa!
 
Daraja la kisiwani limegusiwa, halina alama ya kulitambulisha hivyo kupelekea ajali za kutosha.
 
Mdau mwingine anazungumzia mustakabali wa mdau anayejenga ghorofa pale CHAMA, anahoji amepata wapi kibali!
 
Dogo mmoja anazungumzia Capitation Grant kwa shule za msingi, miksa mpango wa MMES 2 na jinsi tulivyofaidika nao...
Pia anazungumzia hoja ya SAKos na complication zake!
 
Mdau mwingine anazungumzia mchakato wa katiba mpya na uhusika wake.
Amezungumzia pia maisha magumu na wabunge kuongezwa posho kinyemela!
 
Mwenda anazungumzia mpango wa makazi. Anasema ni vigumu kuendeleza uswahilini kwa kuwa mradi uko njiani. Maybe he's right...
 
Kuhusu shule ya sekondari anazungumzia ugumu wa kujenga shule ya sekondari kwetu! Eneo halitoshi mazee...
 
Anasema kuwa ofisi ya kata itajengwa karibuni...
 
Anasemea uhalali wa mfumo unaotumika kwenye SACCoS na faida zake!
 
Anakiri kuwa kosa lilifanyika kuhusu ubomozi wa ukuta wa makaburi by mwekezaji. Titamwajibisha!
 
Kuna mpango wa upanuzi wa barabara ya old bagamoyo, na urekebishaji wa daraja la kisiwani!
 
Naona Mwenda anaelekea kukamilisha ngwe yake...
 
Dada Halima ameshika kipaza...
Anahimiza vijana kufanya kazi!
 
Anasema tumtumie mstahiki meya ambaye ni diwani wetu!
 
Anazungumzia ugumu wa kusapoti makundi ambayo hayana malengo ya kimaendeleo!
 
Back
Top Bottom