What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

What has Halima Mdee done for Kawe (2010-2015)?

Wana Kawe twamshangaa mbunge wetu kwa vile suala la madaktari alivalilia mbuga kuvunjwa kwa haki za binadamu wakati suala la jeshi la polisi kuwapiga mabomu wapiga kura wake kule Madale yuko kimya??

kwa hapa ni lazima atueleze kwanini anaona hili tatizo ni sawa, wakati diwani, mwenyekiti wa mtaa, na wajumbe wa nyumba kumi hawakamushirikishwa?namshangaa, watu wa kituo cha hakiza binadamu , wako benga kwa benga kusaidia angalao wahanga wapate haki za kibinadamu za kuishai, kuwa hawana chakula hwana malazi hawana vitu wanalala nje,lakini yuko kimya tu.Je hata yuko safarini , hana msaidizi?tumtafute msemaji wa chadema kujua kulikoni, hapa kama ni mbunge bure, ndo wabunge wa msimu.Suala la lulu alivalia bango utafikiri nini leo watu 1000 hawana makazi yuko kimya, ajabu sana.
 
MAFILILI ulitaka Halima Mdee aingie misikitini huko ununio kuwahamasisha waislamu kuwa tayari kushiriki sensa ili apigwe kama walivyomfanyia mkuu wa wilaya ya kilwa!?
Si kila jambo linalotokea lazima mbunge atoe kauli. Mambo mengine ni ya utendaji zaidi kuliko porojo za majukwaani.
Halima Mdee ni mbunge makini sana kiasi cha kuwapandisha pressure manyang'au wa ccm.
 
Last edited by a moderator:
kumbe tatizo hilo hata kwa wabunge wa dar es salaam? huku mikoani tumeshazoe mkimchagua anahamia dsm anangoja wakati wa kampeni!
 
MAFILILI ulitaka Halima Mdee aingie misikitini huko ununio kuwahamasisha waislamu kuwa tayari kushiriki sensa ili apigwe kama walivyomfanyia mkuu wa wilaya ya kilwa!?
Si kila jambo linalotokea lazima mbunge atoe kauli. Mambo mengine ni ya utendaji zaidi kuliko porojo za majukwaani.
Halima Mdee ni mbunge makini sana kiasi cha kuwapandisha pressure manyang'au wa ccm.
Mwita nakubaliana na wewe kuwa Mbunge Mdee ni makini akiwa mjengoni LAKINI hana utashi wa kufuta kero za wapiga kura wake. Nitamsifia iwapo amesoma alama na kuona hana tena mvuto kwa wapiga kura hivyo anajiwekea mazingira mazuri ya kutogombea mwaka 2015.
 
- Sensa ni kazi ya serikali kuwaeleimisha watu wake. - Pia wanaogoma kuhesabiwa na matakwa hayo wenyewe na si kukosa kuelimishwa. - Swala la Wakazi wa Madale mahakama ilishaamua wavamizi hao kuondolewa mapema kabla ya uchaguzi wa 2010 lakini CCM ilikaa kimya kwa kigezo ni wapiga kula. -
 
Mbunge wa CCM wa tarime amepora uwanja wa mpira wa miguu mbezi beach eneo la jogoo. Halima mdee uko wapi?
Kweli aisee,huu uwanja hapa jogoo wa mpira,umewekewa fensi kubwa!alikua alishiriakiana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa aitwae Juma mnanka!jamaa ana tamaa sana ya mali za wananchi!mbunge tusaidie wapige kuraa wako
 
Mwita nakubaliana na wewe kuwa Mbunge Mdee ni makini akiwa mjengoni LAKINI hana utashi wa kufuta kero za wapiga kura wake. Nitamsifia iwapo amesoma alama na kuona hana tena mvuto kwa wapiga kura hivyo anajiwekea mazingira mazuri ya kutogombea mwaka 2015.

MAFILILI kabla ya kukimbilia kurundika lawama kwa mbunge umechukua hatua gani kuwahamasisha waislamu kushiriki sensa? Ulichukua hatua gani kuwakemea wale wote waliokuwa wanahamasisha wenzao wasishiriki sensa?
Je umetoa msaada gani kwa hao wananchi waliovunjiwa nyumba zao na serikali ya chama unachokihusudu cha mabwepande?
 
Last edited by a moderator:
Mbunge wa CCM wa tarime amepora uwanja wa mpira wa miguu mbezi beach eneo la jogoo. Halima mdee uko wapi?

Wakati mnamsubiri mbunge, mmechukua hatua gani za kulifikisha suala hili katika vyombo husika vya kiserikali?
 
Huo uwanja wa Jogoo,ndio uwanja pekee ambao wakazi wa mbezi walikua wanafanyia mazoez,hata kama kuna vikao ndio mikusanyiko inakuwa pale,sasa umeuzwa!mbunge njoo hapa utueleze,manake 2015 utakosa pa kufanyia kampeni.
 
Wakati mnamsubiri mbunge, mmechukua hatua gani za kulifikisha suala hili katika vyombo husika vya kiserikali?
Mkuu utalifikisha wapi wakati wenye serikali ndio wamepora?mwenyekiti wa serikali ya mtaa ndio kinara wa uvamizi!
 
Mchezo wa draft ukiwa pembeni mitego yote unaiona. Ukiingia uliongoni mmh...
 
Siamini maneno haya yanatoka kwako. Uyatoe tena September 015

Kwahiyo unawashauri waendelee kukaa kimya wakimtazama nyambari akiwadhulumu uwanja kisa mbunge hajasema neno?
September 015 kutakuwa na nini bibie hadi ujiwekee malengo?
 
Huyu mtu yaani Halima kwa kweli sisi wana Kawe hatujaridhishwa kabisa na utendaji wake jimboni haonekani tangu nimuone kipindi cha kampeni hapa Boko sijawahi muona tena sasaatambue siku zake zinakuja hukuhatutaki lelemama wala tusije laumiana hata kuja kuongea tu na wananchi walau wakakuona haji,asije unakampeni ngumu za 2015 akatulaumu huku mimi huwa nashindwa kuwaelewa wabunge wetu yaani hata kujichanganya tu kwenye mkusanyiko wa watu kama madreva bodaboda,sokoni nakuwasalimia tu wanashindwa haya tutaonana 2015 Halima.
 
Kwahiyo unawashauri waendelee kukaa kimya wakimtazama nyambari akiwadhulumu uwanja kisa mbunge hajasema neno?
September 015 kutakuwa na nini bibie hadi ujiwekee malengo?

Kuhusu kuna nini utajua muda ukifika.

Unajua fika kuwa wamechukua hatua kadhaa na kuna first responders wako.nao bega kwa bega.

Hii haiondoi haja ya wananchi hawa kumwulizia mwakilishi wao. Yupo wapi wananchi wanamuhitaji kuliko walivyowahi kumhitaji.
 
Wakati mnamsubiri mbunge, mmechukua hatua gani za kulifikisha suala hili katika vyombo husika vya kiserikali?

hatukukukaa kimya kama unavyodhania. Tumepeleka malalamiko yetu kwa viongozi wote tuliowachagua yaani diwani, mbunge, wizara et al.
Kama ulikuwa hujui sasa ujue pia kuwa mbunge ni moja ya chombo husika. Moja ya tatizo kubwa la jimbo la kawe ni uvamizi wa maeneo ya wazi na ni moja ya pledge zake mdee kwenye kampeni ya ubunge.
Usijaribu kutetea kutokuwajibika kisa ni mbunge wa CDM.
Kwenye hii thread kuna madai ya ukweli kama unafahamu halima mdee mwambie.
Awe anaonekana jimboni na awe anapatikana.
So far performance yake jimboni kama ya rita mlaki
 
Samahani kwa kutoa malalamiko dhidi ya mbunge wangu. Mie mambo ya Temeke, Ilala, Ubungo nk hayanihusu nimezungumzia mbunge wetu. Wapiga kura wamepigwa na polisi pia wakachomewa nyumba na mashamba yeye ameshindwa kuwasaidia wala kuwapa pole. Kuwa mkweli Halima Mdee hatupi haki yetu wana Kawe

cdm walishasema wao sio wahamasishaji wa uvunjaji wa sheria. Kama watu wamevamia mashamba ya watu acha waondolewe japokuwa siyo kwa utaratibu uliotumika. Mbona hamkumuita kutetea waliobomolewa ufukweni? Mnataka muanze kusema wanatetea uvunjaji wa sheria? Cdm wanatetea wale waliochukuliwa viwanja vyao wakiwa wamiliki halali kama wale wa kituo cha mafuta ambao baada ya kukataa pesa akala mkubwa manispaa.
 
Najua fika kuwa mheshimiwa Halima anafuatilia uzi huu under guest,tunakuomba fuatilia hii isssue,wasiliana na viongozi wa mtaa mbezi juu,haswa mwenyekiti!ule uwanja wameuza!usidanganyike dada yetu.
 
Back
Top Bottom