mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,421
- 1,792
Ni masikitiko kwa wana Kawe, Mbunge Halima Mdee umekuwa huonekani jimboni mwako hasa majira ya mchana. Umekuwa ni mtu wa kutoka alfajiri ili ukimbie kuonana na wapiga kura, unarudi usiku wa manane.
Kwa kweli waliokushauri uchukue ubunge wa jimbo walifanya makosa makubwa, uwezo wako ni kuwa MBUNGE wa Viti Maalum. Tunakushangaa zimebaki siku chache kwenda kikao cha BAJETI, Dodoma, HAUJATHUBUTU kupita kwa wapiga kura kukusanya maoni ili uyawakilishe BUNGENI. Kwa taarifa yako TUMEKUCHOKA SANA pamoja na chama chako!!
Tujifunze kukubali na kukabili changamoto na si kuzikwepa
yupo segerea ameenda kumtoa sero LULU MAFILILI
Simtetei sana Mheshimiwa ila ningependa kufahamu wanakawe wanataka akachukue mawazo yao kuhusu bajeti,mawazo yapi hayo? wakati hata wao hawapeleki mawazo yoyote zaidi ya kupitisha na kutopitisha kilichowasilishwa na serikali. nakushauri kama una mawazo mtafute waziri husika.
Siku moja nilitembelea maeneo ya madale nikapita kijiwe kimoja nikaweka kijiwe na mie kujua nini kinaendela vijana wanalalamika kuwa tangu Halima apate Ubunge hajaonekana huko ,Na mmoja akakazia wewe mwache tu tunasubiri 2015
Halima please fanya fanya ziara kwa wapiga kura wako
Halima kama upo jf unayasoma haya uyafanyie kazi
Yaani hapa JF kuna katabia cha kuanzisha UZI ili mtu aonekane kuwa naye anajua kuanzisha Mada. Kuna mtindo wa baadhi yetu kuharibu mijadala ya hapa kwa kuchukua mada zilizojadiliwa siku ya nyuma na kuileta upya ili tu aonekane na yeye ameanza.
HII MADA ILIJADILIWA KWA KIREFU SANA WIKI hii KABLA JF HAIJAFUNGWA KWA MATENGENEZO. NA MH. HALIMA MDEE ALIICHANGIA kwa KIREFU SANA.
Sasa kama waungwana tumekosa mambo ya kuandika, ni kwanini tusichangie au kusoma tu kwa kuhabarika mada za wengine ambazo ni mpya, kuliko kuturudisha nyuma.
TAFAKARI KABLA YA KUWEKA uzi MPYA HAPA; MNATUCHOSHA NA KUTUHARIBIA UMAKINI WETU KATIKA KUFIKIRIA MAMBO YA KUCHANGIA KWA KUWA NA HOJA ZISIZOKUWA na MIGUU WALA MASIKIO.
MIZAMBWA
INANUMA SANA!!!
Last edited by a moderator: