Wezi wenye 'leseni ya kukuibia' Kariakoo

Wezi wenye 'leseni ya kukuibia' Kariakoo

Jamani na mimi nilishapigwa hapohapo maduka yanayotizamana na Shule ya Uhuru nikawaonesha risiti ya Jina la Duka wakanikatalia kabisa.

Hawa wauzaji wao wana simu aina nyingi sasa mm nikaletewa aina mojawapo inaitwa Bundy kwa manjonjo na promotion ya kupewa fulana na Betri wakadai niwape 250,000/

Wanapenda kukaa kwenye Noah kwenye choo cha kulipia kule Samora baada ya Clock Tower tumebishana wakashuka hadi 175,000/ fulana na Betri wananinyang'anya eti wanatangazia.
Jamani nusu saa hamna kitu simu haina Network, kwa vile nina risiti iliyoelekeza kuwa wapo Plot na Block mitaa ya Uhuru nikaipata, Boss akaniruka nikajua nimepigwa.

Baada ya mwezi nikawaona tena wapo Dodoma mitaa ya Nyerere square, wakanivaa na uongo wao basi kwa hasira nikawakoromea na kuwaonesha kimeo chao cha Bundy tena imekufa kabisa,
wakaniomba msamaha wakalala kona na mm nikawaambia bora wafungashe naifuata risiti nikawakamate.

Nashangaa mpaka leo bado wanaziuza tu na hawakamatwi na Noah yao ya kijivu T ??? CBV
nitaomba ruksa yenu nikipata picha niwaweke hadharani hapa
Jamani simu tununue maduka ambayo unaweza hata kuirudisha ukabadilishiwa
Hao ni wale wanaoununua simu mbovu na kuzitengeneza ziwake tuu basi then wanaziuza kwa Mnada au promotion.
 
Hao ni wale wanaoununua simu mbovu na kuzitengeneza ziwake tuu basi then wanaziuza kwa Mnada au promotion.
huyo Jamaa analo Duka kalisajili kwa jina la TRACE ... Co Ltd ndio anawatuma na anabishara nyingi tu wanazo kwenye gari ya Noah yupo mitaa hiyo hiyo opp na Shule Uhuru mchanganyiko na bado wanazunguka na Promo zao, iko siku wataingia 18 hata kwa mwingine. Naona kaagiza mzigo kaingizwa mkenge sasa kafanya deal apoze biashara zake.

Risiti yake nimeitunza na wapo wengi naona wanarudi kuja kutucheka, bora kuwashtua wengine lkmn mm nitakula nao sahani moja Watanzania hawaibiwi x 2
 
Mwanaume kabisa nzima na ndevu zako sijui unaitwa baba nyumbani au unaitwa baby na mtu wako unaenda kununua simu imeandikwa Brand ya Bundy? Hahahaha au Vituz? Halafu unajitapa wewe ni wa mjini? Na wa Mwabhagosha wanunue simu aina gani sasa?
Kaa Kijijini tu wewe maana unajua kila kitu kinauzwa dukani, na ndio mnaojua kuna simu aina moja
hapo umeshaelezewa ni promotion ukajua ni mbuzi na kuku minadani, tembea mijini Mkuu acha ushamba
 
Mkuu inamaanisha unaweza kununua simu bila kuwasha hapo hapo Dukani?maana karibu simu zote ukiwasha lazima itokee brand/jina aina ya simu wakati wa kuwasha mfano Samsung, Nokia,Tekno,Itel,LG. Sasa unaposema unauziwa housing ya LG ndani mashine ya Itel au Tekno nadhani haupo sahihi.
Unaweza usielewe Hadi yakukute..
Nna mtu alijua kanunua Sony Ericsson kumbe
Itel ndani..ukiwaasha haitoi brand..inawaka
Lakini display Tecno kabisa..tulipoichunguza ndo tukajua ni itel ndani
 
Mkuu inamaanisha unaweza kununua simu bila kuwasha hapo hapo Dukani?maana karibu simu zote ukiwasha lazima itokee brand/jina aina ya simu wakati wa kuwasha mfano Samsung, Nokia,Tekno,Itel,LG. Sasa unaposema unauziwa housing ya LG ndani mashine ya Itel au Tekno nadhani haupo sahihi.
Simu kuibadilisha brand wakati wa kuwasha inawezekana. Usibishe.

Tunaoweza kununuwa vitu halisi ni sisi wenyewe ambao tupo hapa mjini tangu Dar ikiitwa Mzizima.

Ukienda dukani tu kwenye mapatano anajuwa wazi hizi ni shoti za umeme hufanyiwi mzaha.

Mimi hata chaja huwa hawathubutu kubadirisha tunaongea mapema hii chaja imekuja na simu? Na inachaji kwa muda gani?

Ukija mbugira kutoka Chato chaja hupewi iliyokuja na simu na zile sijui ndio hear phone au head phone wanazitowa OG wanakupiga na famfa.
 
Kaa Kijijini tu wewe maana unajua kila kitu kinauzwa dukani, na ndio mnaojua kuna simu aina moja
hapo umeshaelezewa ni promotion ukajua ni mbuzi na kuku minadani, tembea mijini Mkuu acha ushamba

Akili inayoshirikiana kwenye kona haiwezi kununua simu inaitwa Bundy. Ni akili ya bundi tu inayoweza kufanya hivyo.
 
Mama wa afya si anaanza tusubiri mpe mda atapwaya na atatolewa ngoja uone rizavu wao wengi
Mnakumbuka K alivyoanza na mkwara pale alipokua naibu waziri?
Funga mageti funguo weka kule. Mkulu akaona labda hili jembe. Duh. Alipoonjeshwa na mdada wa kipare na kujua kupanda ndege bure, akaanza kutongoza kila mrembo aliye kwenye chati.
Sasa hivi hata kwenye malumbano ya baiskeli simuoni.
Ameshajua mtu mwenye pesa si mwenzake
 
Hapo mi nafungua Bucha sitaki upumbavu mie,

Rudisha changu vinginevyo tunagawana Majengo .
 
Kwa zanzibar vipi,leteni mlejesho mana mm kule nimenunua simu zaidi ya tatu kwa nyakati tofauti ila moja ikawa haisomi network na niliirudisha wakaibadilisha ,na simu ukipewa inakuwa siridi.Nina siku sipo huko sijui hali ipoje,ila wengi wafanya biashara wa kule sio kama wa hapo kaliakoo.Uaminifu kidogo upo nazani kwa ajili ya dini
 
Hakika ni kweli kabisa... Ndiyo maana ki bora sana kununua vifaa kwa Authorised dealers...





Cc: mahondaw
 
Kuna mengi yanasononesha kwenye hii nchi polisi vituo vyote Tanzania nzima kumejaa rushwa lakini serikali ni kama vile haioni huu mchezo
Niliuziwa Flash Disk yenye GB 16 Kwa bei ya SHS 15000/= New Brand ikaCorrupt baada wiki moja. Eneo Hilo Hilo Kariakoo Kwa ndani. Inaitwa San Disk.
 
Unaropoka ropoka naona
Kkoo ni vichochoroni?
Corridor inahudumia nchi zaidi ya kumi ni vichochoroni?

Punguza ujuaji...
Kama hao wauzaji wa kariakoo au popote huko bongo sio authorize dealer au agent wa kuuza hizi simu za Samsung
Kwa kiwango changu huko ni vichochoroni tu
 
Niliuziwa Flash Disk yenye GB 16 Kwa bei ya SHS 15000/= New Brand ikaCorrupt baada wiki moja. Eneo Hilo Hilo Kariakoo Kwa ndani. Inaitwa San Disk.
Mi mwenyewe mkuu niliuziwa flash ikajaribishwa kabisa iko poa inasoma ile kufika home haioneshi kitu, duka lenyewe nikawa silikumbuki basi ikala kwangu.
 
Kariakoo ni sehemu ya kununulia vitochi tu,zaidi ya hapo ni kutafuta kuwatajirisha watu tu!.
 
Back
Top Bottom