mkuu umenikumbusha mbalikutoroka darasan na kwenda kula matunda.niki kumbuka hii hua na cheka sana:smile-big:
mkuuuuuu....kwi kwi kwiiiiih...kufuta stamp za Posta kwa kutumia sabuni na ka kipande cha godoro ili kutuma barua bure from boarding school to home.. Halafu barua yenyewe inaomba TMO or EMO
hiyo 13 daaaaaah...1.Kumpiga mjusi halafu mnakimbiza kunywa maji kabla mkia wake haujaacha kuruka ruka.
2.Kutengeneza mpira wa nage kwa kutumia soksi za shule...
3. Kuvaa soksi za pundamilia zilizotoboka kwenye kisigino
4. Raba maarufu za losso na viatu vya chachacha...
5.kubeba madaftari ya shule na mifuko ya rambo
6 kupiga passport size yaani kuosha maeneo muhimu tu ya mwili nikiwa boarding sababu ya baridi au uhaba wa maji.
7.kuweka maharage au makande sukari blueband na peanut butter.
8.mchezo wa heshima ya ndege au mzinga bomoa...acha kabisa unaweza kubutuliwa ngumi ukaona nyota.
9.kuogelea mtoni kutwa nzima..then nakaa juani nakauka na ki.c.h.u.p.I changu narudi tena kuogelea..
10.kupanda kwenye miti ya miembe na mizambarau kama nyani
11.nikipigwa na kakaangu sinyamazi kama bi mkubwa yupo karibu mpaka aje akute nalia na kama yupi mbali sifuti machoz mpaka yanakaukia mashavuni ili bi mkubwa ajue nlipewa kipondo.
12.kubana sadaka kila jpili kwa ajili ya maandaz shule
13.kusingizia naumwa tumbo la period nisifanye mazoez asubuh boarding.
hahahaaaaaaaaa,hiyo ya kuweka mate umeniteka mbaaali mkuu!Namkumbuka mdudu flani hivi,ukimwambia Arusha wapi anaelekeza mkia,na kingine ukipoteza kitu unajaza mate mkononi af unayapiga
au kitumbua au kiazi usipowagawia wanakutenga kesho yake!1.Kupakaa mate kwenye ugoko unaporudi nyumban jion ili usionekane mchafu ukapigwa.
2. Kulilia kununuliwa nguo mpya kila inapokaribia sikukuu.
3. Kugawana kisheti kimoja au Andaz 1 watu kama kumi hivi.
hiyo namba 3 imenivunja mbavu daaah!nilifanya hvo nikapelekwa kwa mwlmu,nilitandikwa balaa1: Kugawa andaz au chochte then ukimaliza lako unawadai uliowapa kwa kilio
2:Kufunuana nan hajavaa chupi (nilikuwa mstari wa mbele kufunua wenzangu ila kuna siku nikagoma kuwafunua huku nawatetea. wajanja wakagundua na mi sjavaa. Acha nikimbizwe bana duh! )
3:Kueka kioo chini ya miguu kumchungulia mwenzio(hasa boys)
4:Njaa ikiuma Xul nalia eti naumwa tumbo ili niruhucwe kurd hm.
1. kusugua sufuria kwa mchanga,
2. kutambiana kupigana kwa kuchora msitari wa kati na kutambiana wa kuuvuka,
3. kutotaka taa izimwe wakati nataka kulala kwa hofu,
4. kuchapwa bakora na walimu (ilikuwa kama kaoperation fulani) baada ya kugundulika kuwa una mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi mwenzako
5. kuibiana penseli/kalamu mashuleni kwani sikumbuki kama kuna wanafunzi walikuwa wakimaliza wino katika kalamu zao zaidi ya kupotea
6. Kuandikiana barua za kimapenzi mashuleni
7. kuwahofu form two wakati ninyi mkiwa form one
8.Mchezo wa baba na mama ingawa mimi sikuexperience huo mchezo
hiyo 13 daaaaaah...