BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,034
- 3,945
- Thread starter
- #61
...Ndio wanavyofanya Mkuu hata kila mtu anapuyanga kivyake vyake.Kiapo cha ndoa kinasema mtaishi kwa shida na raha.
Baadhi ya Wanawake huwa wanashindwa kuishi kwenye kipengele cha shida. Kwenye kipindi cha shida ndio tabia zao halisi huonekana. Hivyo alichokifanya Mke hutokea sana kwa wale ambao waume zao ni wagonjwa wa muda mrefu au walioachishwa kazi hivyo simshangai. Ila wanaume wanaofanyiwaga hivi huwa wakipona au wakija kupata kazi 'Revenge' zao huwa sio za kitoto maana huwa wanapataga machungu sana.
Halafu kwa umri wa hao Watoto mbona ni wakubwa tu!. Wanatakiwa waanze kujitegemea na wamsaidie Baba yao, huyo wa kike nae ana umri wa kuchumbiwa.