Wenye ujuzi naombeni USHAURI wa jambo hili.

Wenye ujuzi naombeni USHAURI wa jambo hili.

CHIEF MKULAZA

Member
Joined
Sep 10, 2024
Posts
14
Reaction score
17
Mi nataka kweny tasnia ya maafisa usafirishaji lkn nna changamoto kadhaa hivyo ningependa kupata USHAURI kutoka kwenu

Kwanza kabisa mi ninajua kuendesha pikipiki lakini sina leseni. Sasa kuna mahali NAFANYA kazi lakini ndo hivyo kipato ni cha kudunduliza, nimejimake nna akiba kama lak 8 hivi.

Nakuja kweny lengo la kuja kwenu, niliona tangazo kweny mtandao kuhusu bajaji za mkopo ambazo zinatolewa na mo finance kwa kianzio cha shilingi laki Saba lakini rejesho kwa wiki ni laki na 80 hivi.

Nikacheki vigezo baadhi navimudu ila kuna vingine MFANO lesseni ni kipengele,

Swali la kwanza
1. je inawezekana kupata lesseni kwa haraka
2. Je kulingana na muda ambao natoka job saa tisa jioni nitatoboa rejesho la wiki??
3. Gharama ya lesseni ni kiasi Gani na nianzie wapi kuitafuta
NATANGULIZA SHUKRANI NA SAMAHANI KWA MAELEZO MAREFU
 
Back
Top Bottom