Wenje aeleza sababu za Pinda kuzomewa Mwanza

tocolyitics

Member
Feb 5, 2012
76
35
Mbunge wa Nyamagana amewaambia wananchi wa Mwanza kuwa Pinda alikuja kufanya ziara ambayo haikuwa na tija. Wenje anasema Waziri mkuu anakuja na msafara mrefu wa magari zaidi ya 50 ili kukagua mizinga ishirini ya nyuki Buhongwa. je haya siyo matumizi mabaya ya fedha za walipakodi?
 
Ni kweli, haiwezekani PM anatumia magari ya serikali tena akiwa ziara za kiserikali lakini hajui wapi pakukutana na magamba! Angekuwa anatenga muda wa kukutana na magamba wenzake tofauti na ilivyo sasa anakuwa na magamba wakati wa shughuli za kiserikali, na hapo ndipo viongozi wetu wanapoharibu!! Wanajua lakini wanafanya makusudi!!
 
Wangetakiwa kumpiga mawe kwa kuchezea pesa za walipa kodi wakati wengine hata mlo wa siku moja wanakosa magari 50 wanaenda harusini ?nawapongeza xana waliomzomea .
 
Mh;wenje ukosahihikabisa maanaviongozi wanaakili za kushikiwa tu.mizinga 20 inapaswa ikaguliwe kwabaisikeri maana gari hamsini kila gari litumie litaishirini mara hamsini mara2000 ni millioni 2 kiongozi mwenye elimu ya dalasa la 7 angetuma mtuwabaiskeri na million 2 waegenunua mizinga bora kama 40 na zaidi wangeendelea sana. Ila wasomi wa ccm wenye elimu ya zaidi ya digri moja huenda wenyewe na kuongea upuuzi wa kibambucha eti wasomi?. Hooooovyo.nawajinga wanaojuakusoma na kuandika wa ccm hutamba ati wamesheheni maprof. Wanasahau kuwa mkono wamjinga huandika kilimahali ccm oooooooooooyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Huyo ndo mtoto wa mkulima bwana sasa yuko matawi ya juu sijui tumwite mtoto wa Mabepari maana gari 50 za serikali kwenye msafala kama zingeenda ata mbili si jamaa wa nyuki wangeongezewa mtaji
 
Kuna Chumvi Kali sana Imeongezwa kwa habari hii.....Alienda Ukelewe,geita na sengerema....Haikuwa Mwanza mjini na buhongwa peke yake. Nina walakini na Wenje katika maelezo yake.
 
Mbunge wa nyamagana amewaambia wananchi wa mwanza kuwa pinda alikuja kufanya dhiara ambayo haikuwa na tija. Wenje anasema Waziri mkuu anakuja na msafara mrefu wa magari zaidi ya 50 ili kukagua mizinga ishirini ya nyuki buhongwa. je haya siyo matumizi mabaya ya fedha za walipakodi?
:clap2:
 
Kuna Chumvi Kali sana Imeongezwa kwa habari hii.....Alienda Ukelewe,geita na sengerema....Haikuwa Mwanza mjini na buhongwa peke yake. Nina walakini na Wenje katika maelezo yake.
mkuu sehemu zingine alikuwa anaenda kuzindua misingi tu ya majengo. mfano bugarika akaanza kuwauliza watoto wa primary maswali kama: katibu mkuu wa CCM ni nani? watoto wakajibu NAPE NAUYE lakini bado akawagawia 10000 kila mmoja. kisha akauliza tena, Mnafundishwa? watoto ndiyo. akauliza mlima mrefu zaidi duniani ni upi? watoto wakajb KILIMANJARO.
 
Back
Top Bottom