Wengi mtanitoa akili

Wengi mtanitoa akili

Hongkong

Member
Joined
Dec 27, 2022
Posts
54
Reaction score
152
Hi

Mimi nilibahatika kupata kazi sehemu fulani mshahara ulikuwa mdogo ila nilificha mtu yoyote asijue napokea kiasi gani

Sasa siku moja katika kuongea nikajikuta nimesema kwa ndugu mshahara wangu wakaanza kunichamba hapa ushibi bora uache iyo kazi tutakutafutia sehemu nyingine acha mara moja nilisemwa sana mengine siwez ongea

Nikaacha ile kazi sasa uhuu yapata mwezi wa nane tangu niache wao wenzangu mambo yao yana nyooka mimi nimekuwa omba omba kwao nachukia kipindi kile nilikuwa napata sawa mshahara kidogo ila nilikuwa siombi
 
Ndgu achana nao kabisa aisee, akiona hajui kile unafanya atajitahidi ajue.

Akijua kama kina maslahi kidogo anaanza kukusimanga na maneno kibao huku akitoa ahadi kedekede.

Ooh unatudhalilisha kazi gani hiyo, bora uache tukupe mtaji, bora uache mjomba wako akupachike pale ofisini kwao.

Kulaleki acha uone
 
Ukiendekeza ndugu/
Utavuna magugu/
Utaachiwa na sugu/
Na mungu hautamwabudu/
Utamkataa wa moto/
Utamkataa wa baridi/
Atakuja wa vuguvugu/
Naye pia ataleta gubu/...

R.O.M.A-MKOMBOZI
 
Sasa saizi kwakuwa walishakishawishi ukaacha huo mshahara kiduchu ebu share nasisi ilikuwa sh ngp mkubwa?
 
Hi

Mimi nilibahatika kupata kazi sehemu fulani mshahara ulikuwa mdogo ila nilificha mtu yoyote asijue napokea kiasi gani

Sasa siku moja katika kuongea nikajikuta nimesema kwa ndugu mshahara wangu wakaanza kunichamba hapa ushibi bora uache iyo kazi tutakutafutia sehemu nyingine acha mara moja nilisemwa sana mengine siwez ongea

Nikaacha ile kazi sasa uhuu yapata mwezi wa nane tangu niache wao wenzangu mambo yao yana nyooka mimi nimekuwa omba omba kwao nachukia kipindi kile nilikuwa napata sawa mshahara kidogo ila nilikuwa siombi
Pata kazi kwanza ndiyo uache kazi.
 
Ulitakiwa upate kazi mpya kwanza ndo uache uliyokuwa nayo.
Uliwaamini Vipi na wewe?
Haya maisha inatakiwa kujitambua sana na kuelewa maana ya "za kuambiwa changanya na zako".

Sehemu nyingine inabidi uwe mbishi kabisa hutaki kusikia la mtu, upate lawama kuliko fedheha.

Mtu anakushawishi kabisaaa uache kazi, kama atakupa yeye kazi nyingine, halafu unamsikiliza unaacha kazi kabla ya kupata nyingine!

Unaanza anzaje kufanya kitu cha hatari hivi?
 
Hi

Mimi nilibahatika kupata kazi sehemu fulani mshahara ulikuwa mdogo ila nilificha mtu yoyote asijue napokea kiasi gani

Sasa siku moja katika kuongea nikajikuta nimesema kwa ndugu mshahara wangu wakaanza kunichamba hapa ushibi bora uache iyo kazi tutakutafutia sehemu nyingine acha mara moja nilisemwa sana mengine siwez ongea

Nikaacha ile kazi sasa uhuu yapata mwezi wa nane tangu niache wao wenzangu mambo yao yana nyooka mimi nimekuwa omba omba kwao nachukia kipindi kile nilikuwa napata sawa mshahara kidogo ila nilikuwa siombi
Heri kidogo cha jasho kuliko kidogo cha kuomba.

Acha kazi ukiwa na kazi.
 
Dha, Hizi ndo akili za pimbi, aliacha kazi kabla ajapata kazi, ikawa kazi kutafuka kazi, akaona ilivyo kazi kupata kazi kuliko ile kazi aliyoiacha.
 
Haya maisha inatakiwa kujitambua sana na kuelewa maana ya "za kuambiwa changanya na zako".

Sehemu nyingine inabidi uwe mbishi kabisa hutaki kusikia la mtu, upate lawama kuliko fedheha.

Mtu anakushawishi kabisaaa uache kazi, kama atakupa yeye kazi nyingine, halafu unamsikiliza unaacha kazi kabla ya kupata nyingine!

Unaanza anzaje kufanya kitu cha hatari hivi?
Sijui alikuwa anawaza nini huyu ndugu yetu😀
 
Sijui alikuwa anawaza nini huyu ndugu yetu😀
Haya mengine ni matatizo ya kutaka kukubalika, kutaka kuwa mtu wa kusema ndiyo kila mara ili watu wakupende.

Kuna ndiyo nyingine ukimkubalia mtu hata yeye aliyekushawishi anakucheka.

Inawezekana watu wakakushawishi uache hiyo kazi kama kukupa motisha ya kupata kazi nzuri zaidi, wewe ukaacha kabla ya kupata kazi nzuri zaidi.

Hapo ndiyo unaweza kumuomba mtu hela, ukamwambia nimefuata ushauri wako lakini sina kazi kwa sasa naomba unisaidie, halafu mtu akakuruka na kukuambia nilikuambia uache kazi, sikukuambia uache kazi kabla hujapata kazi nyingine.

Ogopa sana kukubali kitu kwa sababu ya kutotaka lawama tu, unakubali ili uonekane wewe mtu wa kukubaliana na watu.

Sehemu nyingine unatakiwa kuwa ngangali unakataa tu, halafu watu watakuja kukuelewa baadaye.
 
Back
Top Bottom