The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 4,780
- 8,155
Niongee machache kuhusu vitabu vya dini.
Tuna dini kubwa tatu maarufu duniani ambazo ni Ukristo (Christianity), Uislamu (Islamic) na Uyahudi (Judaism)
Dini hizo zote zina vitabu vyake vitakatifu.
Biblia Takatifu kwa Wakristo, Quran Tukufu kwa Waislamu na Tanakh kwa Wayahudi.
Tanakh ni Biblia ya Kiyahudi iliyogawanyika katika vipengele vitatu (Torah, Nevi'im na Ketuvim)
Torah ni vile vitabu vitano vya Musa (Kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Leviticus, Numbers na Deuteronomy) wenyewe wanaita 'Pentateuch'
Nevi'im ni maandiko ya manabii na Ketuvism ni maandiko ya Zaburi na mengineyo.
Quran Tukufu pia imerudia kwa kuhariri kidogo tu maandiko ya Torah, Nevi'im na Ketuvim pamoja na Evangél (Injili)
Ndio kusema vitabu vyote vitatu vya dini kubwa duniani vinafanana katika mengi na kutofautiana katika machache.
Biblia ya Wakristo imenukuu mengi kutoka kwenye Tanakh na kisha kuongezea maandishi mengine mengi ya Wakaldayo, Wakushi (kemet au Misri ya kale), Wamesopotamia, Wasumeri na Warumi.
Ndio kusema Biblia ndiyo Kitabu chenye siri nyingi zaidi hadi sasa pengine kuliko vitabu vingine vingi vya elimu ya siri (esoteric knowledge)
Lakini, hii Biblia ambayo kila mtu anayo imehaririwa zaidi ya mara 10, kuna vitu vimeongezwa na vingine kupunguzwa.
Ndio maana kwenye Theology kuna vitabu tunaambiwa ni THE LOST BOOKS (vitabu vilivyopotea) na THE STOLEN BOOKS (vitabu vilivyoibiwa)
Niliwahi kuhoji, kama kuna vitabu vinajulikana kwamba viliibiwa, NANI ALIVIIBA na kama kuna vitabu vilivyopotea NI NANI ALIVIPOTEZA?
Na ni vitabu gani?
Na kwa nini viibiwe na vipotee?
Sikupata majibu wakati huo kutoka kwa Waalimu wangu wa Theology.
Nilikuja kupata majibu sahihi wakati nikiwa kwenye safari hii ya utambuzi.
Lakini, ninachotaka kusema ni kwamba BIBLIA ni mkusanyiko wa vitabu vingi sana vyenye elimu kale, elimu ya siri na iliyowasilishwa kwa lugha ya mafumbo.
Ni mpaka uwe umeangaziwa ufahamu wako (enlightened) ndipo utakapoweza kutambua mafumbo yaliyomo kwenye maandishi ya kwenye Biblia.
Idadi kubwa ya waalimu wa Biblia, wakiwemo wachungaji hawana uwezo wa kufumbua hayo mafumbo, wanasoma na kufundisha kama yalivyo na ndio maana wafuasi wao wanafanya tu kuyakariri na hawapati matokeo.
Ni waalimu wachache sana wa Biblia wenye ufahamu wa kuvunja hiyo mihuri (kufumbua hayo mafumbo) na hawawezi kuyaeleza hayo hadharani.
Kwa hiyo ni muhimu kuzingatia hilo.
Mimi nimesoma Biblia mara nyingi zaidi kuliko Kitabu kingine chochote na nimekuja kugundua Elimu zote za siri zimo ndani ya Biblia ila 'hazioenekani' kwa urahisi.
Nina Biblia tofauti tofauti 8 na zote zimeandika siri nyingi sana ambazo zipo pia kwenye masomo yote ya kiroho na kwenye jumuiya za siri.
Wale waliokwisha fika level 3 kule Illuminant na Freemasonry watakubaliana nami kwamba huwezi kupata 'badge' ya mwanajumuhia bila kufaulu kuvunja angalau ¼ ya codes zilizomo kwenye Biblia na Biblia ndio Kitabu Kikuu kwa wanafunzi wote chipukizi wa hizi Secret socities nyingi.
Biblia zipo makanisani, misikitini, mahekaluni hadi vilingeni.
Gland Lodges zote kuna Biblia za kila aina huko.
Kwa hiyo, msichukulie kawaida hiki Kitabu.
Nitarejea . . .
Tuna dini kubwa tatu maarufu duniani ambazo ni Ukristo (Christianity), Uislamu (Islamic) na Uyahudi (Judaism)
Dini hizo zote zina vitabu vyake vitakatifu.
Biblia Takatifu kwa Wakristo, Quran Tukufu kwa Waislamu na Tanakh kwa Wayahudi.
Tanakh ni Biblia ya Kiyahudi iliyogawanyika katika vipengele vitatu (Torah, Nevi'im na Ketuvim)
Torah ni vile vitabu vitano vya Musa (Kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Leviticus, Numbers na Deuteronomy) wenyewe wanaita 'Pentateuch'
Nevi'im ni maandiko ya manabii na Ketuvism ni maandiko ya Zaburi na mengineyo.
Quran Tukufu pia imerudia kwa kuhariri kidogo tu maandiko ya Torah, Nevi'im na Ketuvim pamoja na Evangél (Injili)
Ndio kusema vitabu vyote vitatu vya dini kubwa duniani vinafanana katika mengi na kutofautiana katika machache.
Biblia ya Wakristo imenukuu mengi kutoka kwenye Tanakh na kisha kuongezea maandishi mengine mengi ya Wakaldayo, Wakushi (kemet au Misri ya kale), Wamesopotamia, Wasumeri na Warumi.
Ndio kusema Biblia ndiyo Kitabu chenye siri nyingi zaidi hadi sasa pengine kuliko vitabu vingine vingi vya elimu ya siri (esoteric knowledge)
Lakini, hii Biblia ambayo kila mtu anayo imehaririwa zaidi ya mara 10, kuna vitu vimeongezwa na vingine kupunguzwa.
Ndio maana kwenye Theology kuna vitabu tunaambiwa ni THE LOST BOOKS (vitabu vilivyopotea) na THE STOLEN BOOKS (vitabu vilivyoibiwa)
Niliwahi kuhoji, kama kuna vitabu vinajulikana kwamba viliibiwa, NANI ALIVIIBA na kama kuna vitabu vilivyopotea NI NANI ALIVIPOTEZA?
Na ni vitabu gani?
Na kwa nini viibiwe na vipotee?
Sikupata majibu wakati huo kutoka kwa Waalimu wangu wa Theology.
Nilikuja kupata majibu sahihi wakati nikiwa kwenye safari hii ya utambuzi.
Lakini, ninachotaka kusema ni kwamba BIBLIA ni mkusanyiko wa vitabu vingi sana vyenye elimu kale, elimu ya siri na iliyowasilishwa kwa lugha ya mafumbo.
Ni mpaka uwe umeangaziwa ufahamu wako (enlightened) ndipo utakapoweza kutambua mafumbo yaliyomo kwenye maandishi ya kwenye Biblia.
Idadi kubwa ya waalimu wa Biblia, wakiwemo wachungaji hawana uwezo wa kufumbua hayo mafumbo, wanasoma na kufundisha kama yalivyo na ndio maana wafuasi wao wanafanya tu kuyakariri na hawapati matokeo.
Ni waalimu wachache sana wa Biblia wenye ufahamu wa kuvunja hiyo mihuri (kufumbua hayo mafumbo) na hawawezi kuyaeleza hayo hadharani.
Kwa hiyo ni muhimu kuzingatia hilo.
Mimi nimesoma Biblia mara nyingi zaidi kuliko Kitabu kingine chochote na nimekuja kugundua Elimu zote za siri zimo ndani ya Biblia ila 'hazioenekani' kwa urahisi.
Nina Biblia tofauti tofauti 8 na zote zimeandika siri nyingi sana ambazo zipo pia kwenye masomo yote ya kiroho na kwenye jumuiya za siri.
Wale waliokwisha fika level 3 kule Illuminant na Freemasonry watakubaliana nami kwamba huwezi kupata 'badge' ya mwanajumuhia bila kufaulu kuvunja angalau ¼ ya codes zilizomo kwenye Biblia na Biblia ndio Kitabu Kikuu kwa wanafunzi wote chipukizi wa hizi Secret socities nyingi.
Biblia zipo makanisani, misikitini, mahekaluni hadi vilingeni.
Gland Lodges zote kuna Biblia za kila aina huko.
Kwa hiyo, msichukulie kawaida hiki Kitabu.
Nitarejea . . .