Wengi hawajui kwanini tunasema 'Life begins at 40'

Wengi hawajui kwanini tunasema 'Life begins at 40'

Hongera kama ni wewe mwenyewe umefikiria hizo nondo.
Kama sio wewe, umeitoa mahali utakuwa umekosea huja aknowledge
epuka Plagiarism
 
Anasubiri mama afariki, wakarogane kwa waganga kugombania MIRATHI ya nyumba. [emoji53] [emoji18]
Hapo pana kuwaga patamu sana ... ni mwendo wakurushiana mapepo tu ...

Kuna Mkasa mmoja hivi uliwahi kumkuta jamaa yetu mmoja alikuwa anaishi ilala ... wakati wa uhai wake alikuwa ni maarufu sana hasaa kwa wasanii wakike ... alikuwa ni mfanya biashara wa nguo ...office zake zilikuwa kinondoni studio mkabala na nyumba ya kina zamaradi "

Jamaa alitupiwa mapepo kwaajili ya masuala hayo hayo ya mirathi Akafariki ...

Na kwa kukazia tu hoja ya Bujibuji ..TID na umaarufu wake wote mpaka leo bado anaishi kwao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wengi hawajui kwa nini wazungu huwa wanasema LIFE BEGINS AT 40.

Yaani maisha yako ya kweli yataanza ukifika umri wa Miaka 40. Wakati ambapo unatakiwa uwe na elimu uliyoihitaji.. Uwe na familia yako tayari.Uwe na kwako tayari siyo umepanga bado.Uwe na usafiri binafsi.Uwe na kitu chako cha kukuingizia pesa na si kutegemea ajira peke yake. At 40!

At 40 inabidi uwe unaishi. Siyo ndo unaanza kujaribu hiki na kile. At 40 inabidi uwe unasomesha zaidi kuliko kusoma wewe japo kuongeza maarifa ni vizuri.

At 40 unatakiwa uwe umeshapata exposure kwa kusafiri huku na kule dunia hii kujua wengine walioendelea zaidi wanaishi vipi na wewe ufanyeje?

At 40 utakuwa bado unaomba nauli kwa baba na mama kwani?

Sasa hivi vitu haviji ukiwa upoupo tu hutafuti fursa za kukusaidia kuwa na maisha tofauti upo tu una LIKE kila kitu facebook na Instagram unatuma tu picha za ajali za mabasi zikikosekana unatuma za migomo ya madereva mgomo ukiisha unatuma za mafuriko kama mvua zimeisha unatuma picha za Lowassa yaani umekuwa mtumwa wa simu.

Ikikosa network unalalamikia kampuni ya simu utafikiri hiyo network unafanyia kitu cha maana. Gallery yako imejaa vitu vya ajabuajabu tu. Havikufikishi popote na umri unazidi kwenda unazidi kusogea miaka 40 hivi hivi.

Maisha ya kweli yataanza ukiwa na miaka 40. Wakati ambapo watoto wako hawatakula LIKES zako za instagram bali wanahitaji chakula. Wanahitaji ada. Wanahitaji maisha bora. Wewe inasubiri maisha bora CCM ndo wakupe.

Wasipokupa unataka UKAWA waje wakupe ukiwa umekaa Instagram una LIKE picha za Wema Sepetu. Umeshajua Wema akifika miaka 40 atakuwaje? Ulishajiuliza wanamuziki waliovuma miaka 15 iliyopita wakiwa na umri wa miaka 25 hivi au 30 wakati huo wana miaka mingapi na wako wapi sasa hivi. You see?

Unayemfuatilia kila siku kavaaje kaamkaje katembea na nani hakusaidii kuwa na maisha mazuri. Maisha bora hayaji ukiwa unafatilia nyimbo gani zimetoka udownload. Maisha bora hayaji kwa KU-ENTERTAIN brain yako bali kwa kuifikirisha akili na kufanya mambo ambayo wachache tu ndo wanafanya.

Kwani wanasoka wangapi wako kama Beckham
Wanamuziki wangapi wako kama Kirk Franklin
Wacheza Tennis wangapu wako kama Roger Federer? Unadhani amekuwa champion akiwa amekaa na TECNO chumbani ana comment kuhusu migomo? No. Alikuwa ana-hussle wakati wengine wanachat.

Seriously. Diamond unayemfollow anafanya kazi hivyo. Anatoka studio saa saba usiku������ wewe uko kwenye page yake una LIKE. Huwezi kuona kuwa uko tofauti.

Anaandaa maisha akifika miaka 40 awe na kila kitu wewe utakuwa unalalamikia network ya tigo tu na kutuma picha za sijui gari limegonga treni. Kwa hiyo wewe ndio NIPASHE sasa hivi?

Anyway. Kuwa serious na maisha yako angalau basi kwa ajili ya watoto wako na wajukuu zako. Aise huyu mzazi wetu alifanya jambo la maana. Au unadhani watazikuta hizo comments na LIKES ������ zako? No. Wanapaswa wakute nyumba, viwanja, account za benki zinazopumua.

Siyo account inaingiaga mshahara tu halafu by tarehe 10 iko empty ushakomba kila kitu! ������ Wanatakiwa wakute assets za maana angalau. Siyo rundo la CD za bongo movie ambazo hazikusaidii wewe wala wao.

Miezi hii 6 iliyobaki kumaliza mwaka huu 2015 umeweka mikakati gani kuweka msingi wa maisha tofauti sana na kuhakikisha ufikapo umri wa miaka 40?

Au bado unategemea mshahara wa laki 8 (tena hapo kabla ya makato) uje ubadili maisha yako).

Kwa waajiriwa, Microsoft ya Bill Gates inapunguza wafanyakazi 800. Kama ulikuwa hujui. Unadhani kampuni yako ndo utakaa hapo milele?

Be careful my friend

Natafuta watu ambao wako tayari kupunguza kuchat na kutuma picha za vichekesho na waanze kufanya vitu serious kwa ajili ya future. Natafuta watu ambao wako tayari kujifunza na kufundishika na kuweka bidii katika kujiletea maisha bora badala ya kuyasubiria yaletwe na UKAWA au Lowassa.

Haya sasa wamemkata jina.Utagoma kula au? Yaani mi huwa nawashangaa watu. Kabisa unadhani kuna mtu atakupa maisha ya ndoto zako?

Ukweli ni kwamba maisha ni ya kwako na ni wewe utakayeyabadilisha. Bill Gates huyo huyo anasema

"KAMA ULIZALIWA MASKINI HILO SI KOSA LAKO LAKINI UKIFA MASKINI HILO NI KOSA LAKO"
WEWE NI MZUNGU?
 
Watu wengi hawajui kwa nini wazungu huwa wanasema "LIFE BEGINS AT 40". Yaani maisha yako ya kweli yataanza ukifika umri wa Miaka 40. Wakati ambapo unatakiwa uwe na elimu uliyoihitaji... Uwe na familia yako tayari... Uwe na kwako tayari na sio umepanga bado... Uwe na usafiri binafsi... Uwe na kitu chako cha kukuingizia pesa na si kutegemea ajira peke yake. At 40!!View attachment 1049533

At 40 inabidi uwe unaishi. Sio ndio unaanza kujaribu hiki na kile. At 40 inabidi uwe unasomesha zaidi kuliko kusoma wewe japo kuongeza maarifa ni vizuri. At 40 unatakiwa uwe umeshapata exposure kwa kusafiri huku na kule katika dunia hii kujua wengine walioendelea zaidi wanaishi vipi na wewe ufanyeje??? At 40 utakuwa bado unaomba nauli kwa baba na mama kwani???

Sasa hivi vitu haviji ukiwa upo upo tu, unashangaa shangaa hovyo magorofa Posta na Kariakoo. Hutafuti fursa za kukusaidia kuwa na maisha tofauti. Upo tu una "LIKE" kila kitu Facebook, Twitter, JamiiForums na Instagram. Unatuma tu picha za ajali za mabasi zikikosekana, unatuma za migomo ya madereva, mgomo ukiisha unatuma za mafuriko, kama mvua zimeisha unatuma picha za Lowassa. Yaani umekuwa mtumwa wa simu.

Ikikosa network unalalamikia kampuni ya simu utafikiri hiyo network unafanyia kitu cha maana. Gallery yako imejaa vitu vya ajabu ajabu tu. Havikufikishi popote na "UMRI UNAZIDI KWENDA", unazidi kusogea miaka 40 hivi hivi.

Maisha ya kweli yataanza ukiwa na miaka 40. Wakati ambapo watoto wako hawatakula "LIKES" zako za Instagram bali wanahitaji chakula. Wanahitaji ada shule na si "LIKES" zako za Facebook. Wanahitaji wewe kua mfano bora wa maendeleo katika maisha yao. Wanahitaji maisha bora. Wewe unasubiri maisha bora "CCM" au "CUF" ndio wakupe. Wasipokupa unataka "UKAWA" waje wakupe ukiwa umekaa Instagram una "LIKE" picha za Wema Sepetu. Umeshajua wema akifika miaka 40 atakuwaje??? Ulishajiuliza wanamuziki waliovuma miaka 15 iliyopita wakiwa na umri wa miaka 25 hivi au 30 wakati huo wana miaka mingapi na wako wapi sasa hivi. You see???

Unayemfuatilia kila siku kavaaje kaamkaje katembea na nani hakusaidii kuwa na maisha mazuri. Maisha bora hayaji ukiwa unafatilia nyimbo gani zimetoka udownload. Maisha bora hayaji kwa "KU-ENTERTAIN" brain yako bali kwa kuifikirisha akili na kufanya mambo ambayo wachache tu ndo wanafanya.

Kwani wanasoka wangapi wako kama David Beckham na Zinedine Zidane. Wanamuziki wangapi wako kama Kirk Franklin. Wacheza Tennis wangapi wako kama Roger Federer??? Unadhani amekuwa champion akiwa amekaa na "TECNO" na "POWER BANK" chumbani ana comment kuhusu migomo au mafumanizi ya wanandoa??? No. Alikuwa anapambana, alikua ana hustle wakati wengine wako bussy wanachat.

Diamond unayemfollow anafanya kazi hivyo. Anatoka studio saa saba usiku, wewe uko kwenye page yake una "LIKE". Huwezi kuona kuwa uko tofauti??? Anaandaa maisha akifika miaka 40 awe na kila kitu, wewe utakuwa unalalamikia network ya tigo tu, na kutuma picha za sijui gari limegonga treni. Kwa hiyo wewe ndo NIPASHE sasa hivi???

Kuwa serious na maisha yako, angalau basi kwa ajili ya watoto wako na wajukuu zako. "Aise huyu mzazi wetu alifanya jambo la maana". Au unadhani watazikuta hizo "COMMENTS" na "LIKES" zako??? No. Wanapaswa wakute Nyumba, Viwanja, Account za benki zinazopumua (sio Account zipo ICU au MORTUARY). Siyo account inaingiaga mshahara tu halafu by tarehe 10 iko empty ushakomba kila kitu!!!! Wanatakiwa wakute assets za maana angalau. Siyo rundo la "CD" za bongo movie ambazo hazikusaidii wewe wala wao.

Siku zilizobaki kumaliza mwaka huu umeweka mikakati gani kuweka msingi wa maisha tofauti sana na kuhakikisha ufikapo umri wa miaka 40???

Au bado unategemea mshahara wa laki 8 (tena hapo kabla ya makato) uje ubadili maisha yako???

Kwa waajiriwa, Microsoft ya Bill Gates inapunguza wafanyakazi 800. Kama ulikuwa hujui. Unadhani kampuni yako ndo utakaa hapo milele???

Kua mwangalifu rafiki yangu, maisha yanakwenda mbele na kamwe hayaarudi nyuma.

"Kuzaliwa MASIKINI si kosa, ila kufa MASIKINI ni dhambi"

#UKUMBUSHO
Post nzuri sana hii, ina kila sababu za kumfikirisha mtu, kama utasoma na kutokuwa na fikra ya nini unapaswa kufanya (kama hujafanya), basi utakuwa na shida. Ila kwa lifestyle yetu, uwezo wetu mmoja mmoja, familia tunazotoka, elimu tunazopata, its so not easy kuwa na hayo yote at 40.

Mwisho, you need to give credit to the source, naamini kabisa sio kutoka kwenye ubongo wako coz ilishaandikwa.
 
Niliungwa kwenye group LA whatssapp la watu tuliomaliza mwaka mmoja shule ya sekondari.nilijuta. mpaka simu inakata mlio message zinaingia kimya kimya.

Hahaha group letu si tukaomba kila mtu atume picha yake? Wadada wote walituma picha wakiwa wanaendesha gari! Sisi wanaume picha zilizotawala zilikuwa za shamba! Huyu analima nanasi, Yule Tikiti mwingine anafuga nyuki. Haya magroup ni hatari sana
 
At 40 ukamilishe yote hayo kwa hapa TZ bado. Labda sijui uwe umezaliwa ktk familia bora ama ya kati flani hv. Nje ya hapo at 40 utakuwa bado hujakamilisha hayo kwa asilimia zaidi ya nusu.
Kweli kabisa kwa bongo hayo unaweza kuwa umeyakamilisha kama ni mpambanaji at the age of 50

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha group letu si tukaomba kila mtu atume picha yake? Wadada wote walituma picha wakiwa wanaendesha gari! Sisi wanaume picha zilizotawala zilikuwa za shamba! Huyu analima nanasi, Yule Tikiti mwingine anafuga nyuki. Haya magroup ni hatari sana
Sasa unajikinganisha na akina Dada? Wakati huko shule unajisomea wao wamelala anasomewa na mtu fulani mahali fulani! Don't compare yourself with ladies broo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamba watoto wakute akaunti imenona!upuuzi mtupu na wao wafanye nn?bora kuwajengea uwezo wajitafutie nao. Kuna ukweli kwenye uzi lkn pia kuna harufu ya majivuno naona km ni kati ya wale waliozikuta kwenye ac
Yaan uache kujitengenrzea fainali uzeeni eti uanze kuwapa watoto,wao watafanya nn sasa,watoto watajengewa uwezo tu
 
Dah...at 40 hata "mabao" huwa matamu sana....[emoji41]

Sent using Beretta ARX 160
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom