Wengi hawajui kwanini tunasema 'Life begins at 40'

Wengi hawajui kwanini tunasema 'Life begins at 40'

Umeongea vizuri sana ila mfumo unaotengenezwa na viongozi wetu wa kiafrika ni wa kuwadumaza watu, at 40 mpaka leo mtu anafikiria atafikaje mjini akitoka mbagala na atarudi vipi?

Hakuna raia hata mmoja anaejua haki zake za kiraia uwe umesoma au hujasoma.

at 40 mtu anawaza 400 yake ya nauli iko salama mfukoni?

at 40 watu wanauana kwa 1000.

At 40 mtu anashabikia jambo la kipuuzi kwa kua mambo ya maana wanayajua watu wa vitengo tuu hata kama umesoma kiasi gani utabaki kama ulivo na kujiliwaza na smart yako.

Leo serikali inaona ajabu watu wanaofuata mkumbo wamekua wengi kiasi hiki walijua wakiwakosesha elimu watakua chini yao tuu kila siku.
 
Hakika umeekeza kitu ambacho kitasaidia wengi humu ndani
Angalau nawapa moyo waliochelewa wajitahidi wasifike 45yrs bila kuweka misingi bora
Itakuwa in kujichimbia kaburi mwenyewe.
Amka jipange miaka mitano inakutosha
 
Aisee umetugusa. Mungu akubariki sana kwa maneno mazuri yenye mafundisho
 
acha kudanganya nimeanza kwenda vacation na miaka 18 kila mwaka nimejiwekea kwenda nchi zisizopungua 5.

Ni malengo na kuweka akiba ila kwa wabongo ni ngumu kwa sisi cash za dolla ni kitu kidogo

Mkuu upo juu sana!hongera.
 
Ukisikia buuuuu ujue limempata.at wamemkata jina,amehamia upande wa pili.
 
7 miaka +7 elimu ya msingi + 6 sekondari + + 3 chuo = 23

40-23= 17
miaka 17 itatosha kuwa na familia, nyumba, gari ?!
 
Hongera, lakini vidole havilingani. Hayo maneno ni nazuri kuongea lakini kutenda kazi.
 
Kwamba watoto wakute akaunti imenona!upuuzi mtupu na wao wafanye nn?bora kuwajengea uwezo wajitafutie nao. Kuna ukweli kwenye uzi lkn pia kuna harufu ya majivuno naona km ni kati ya wale waliozikuta kwenye ac
 
Kwa utawala huu wa CCM nadhani itakuwa life begins at 60......maana watu mpaka wanakaribia 70 lakini bado bila bila....
 
Mtoa mada amesema vyema. Lakini si kweli kwamba life begins at 40. Mimi naona Ameweka perception yake.

Binafsi kwangu life will begin at 30. By now nina basic education i.e degree (i dont trust in masters so hata nikija kuisoma siyo achievement kwangu) and By 30, nataka niwe na kwangu, gari yangu na ya mke wangu, niwe naweza kusaidia jamii inayonizunguka.

Kuwa na mtoto au kutokuwa naye ni majaaliwa ya mwenyezi Mungu. Life is for you and your wife. Watoto ni sehemu ya jamii inayokuzunguka. Hivyo, ukijipanga vyema unaweza kuwasaidia wao na jamii nzima inayokuzunguza bila upendeleo.

Vijana in your 20s Msicheleweshwe na life begins at 40, hao wamechelewa wanajaribu kujificha humo.

Adios.
 
Watu wengi hawajui kwa nini wazungu huwa wanasema LIFE BEGINS AT 40. Yaani maisha yako ya kweli yataanza ukifika umri wa Miaka 40.

Wakati ambapo unatakiwa uwe na elimu uliyoihitaji.. Uwe na familia yako tayari.. Uwe na kwako tayari siyo umepanga bado.. Uwe na usafiri binafsi.. Uwe na kitu chako cha kukuingizia pesa na si kutegemea ajira peke yake. At 40!!

At 40 inabidi uwe unaishi. Siyo ndo unaanza kujaribu hiki na kile. At 40 inabidi uwe unasomesha zaidi kuliko kusoma wewe japo kuongeza maarifa ni vizuri.
At 40 unatakiwa uwe umeshapata exposure kwa kusafiri huku na kule dunia hii kujua wengine walioendelea zaidi wanaishi vipi na wewe ufanyeje?

At 40 utakuwa bado unaomba nauli kwa baba na mama kwani?

Sasa hivi vitu haviji ukiwa upoupo tu hutafuti fursa za kukusaidia kuwa na maisha tofauti upo tu una LIKE kila kitu facebook na Instagram unatuma tu picha za ajali za mabasi zikikosekana unatuma za migomo ya madereva mgomo ukiisha unatuma za mafuriko kama mvua zimeisha unatuma picha za Lowassa yaani umekuwa mtumwa wa simu.

Ikikosa network unalalamikia kampuni ya simu utafikiri hiyo network unafanyia kitu cha maana.

Gallery yako imejaa vitu vya ajabuajabu tu. Havikufikishi popote na umri unazidi kwenda unazidi kusogea miaka 40 hivi hivi. Maisha ya kweli yataanza ukiwa na miaka 40.

Wakati ambapo watoto wako hawatakula LIKES zako za instagram bali wanahitaji chakula. Wanahitaji ada. Wanahitaji maisha bora. Wewe inasubiri maisha bora CCM ndo wakupe. Wasipokupa unataka UKAWA waje wakupe ukiwa umekaa Instagram unaLIKE picha za Wema Sepetu.

Umeshajua wema akifika miaka 40 atakuwaje? Ulishajiuliza wanamuziki waliovuma miaka 15 iliyopita wakiwa na umri wa miaka 25 hivi au 30 wakati huo wana miaka mingapi na wako wapi sasa hivi. You see?

Unayemfuatilia kila siku kavaaje kaamkaje katembea na nani hakusaidii kuwa na maisha mazuri. Maisha bora hayaji ukiwa unafatilia nyimbo gani zimetoka udownload.

Maisha bora hayaji kwa KU-ENTERTAIN brain yako bali kwa kuifikirisha akili..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom