Weekend Story: You Can't Handle The Truth

Weekend Story: You Can't Handle The Truth

1993! DODOMA TANZANIA

Mi nampenda kweli huyu kaka wa Garage. Weeeeee acha mambo hayo mwenyewe nampenda kama nini. Akuuuuu mi ndo nampenda zaidiiiiii. Tutamalizana wenyewe kwa wenyewe. Bwanaaaa eeeh msitoshe na mikelele kaka mwenyewe huyo hana hata shida na demu. Yuko busy na mambo yake hana mda huo kabisaaaa.

Mmmmmm! Kaka mwenyewe mnaemuongelea ndo huyo Walter? Ndiooooo! Kwani unamjuaaa? Embu tupe habari zake, navompendagaaa, nampenda tu basi. Kim akawa anauliza kwa msisimuko mkubwaaa. Mmmmmmmh! usione naguna mara 5, 5 huyo kaka muone hivo leo hiii, kakua sijui, sijui ila kwa sisi tunaomjuaaaa, tuliozaliwa Dodoma hii Walter SI MTU. Ni mnyamaaaaa tena mnyama mwenyewe faru aliejeruhiwa. Muulize mtu yeyote aliekuwepo Dodoma hii 1980s atakwambia Walter ni mdudu gani." Akalimwaga Da Tausi. Wakabaki kimyaaa wanasikiliza file Walter. "Ninunulieni bia niwape sasa ubuyu kamili wa Walter. Wakaangalianaaa, wakaona sio kesi wakaweka 200, 200 zikafika 1000 noti za 100 kumi. (Kama uliziona hizi hela kaolewe ushazeeka). Wakamletea Safari larger hapo ndo iko on peak in hit.

Walter mimi nilisoma nae Mazengo Sekondari, namjua nje ndani. Walter ni mkorofiiiiiiiiiiiiiiiiii, yaaani ni mkorofiiiiiiiiii hujapata kufikiri. Leo hii hamna mtu anaejua kwanini Walter yuko vile. Hamnaaaaaaaaaa! Enzi zetu Walter alikuwa tishioa Dodoma hiii. Tunavoongea hivi ilikuwa hairuhusiwi kumuita Walter shule. Lazima uanze na Mkubwa Walter. Ukiropokaa ukamuita Walter plain unapigwaaa mpaka unatia akili.

Kuna demu pale mazengo alikuwa anajitunza weee, bikra wa shule. Walter akapata taarifa kwamba kuna bikra pale mazengo. Akasema kama ndo hivo basi yeye Walter ndo ana haki ya kumbikiri huyo bikra. Mmmmmmhhh! Kamtokea demu kachomoa kamwambia Walter wewe mkorofi sanaa mimi sitokuweza. Walter kampandia juu oooh wananisingizia usiamni wanachokisemaa juu yangu. Demu akamkazia Walter. Walter akasema coz demu amepanga kuadhiri mi nishajitangaza nambikiri afu ana nikazia manake ninii? Sasa nitatumia gharama yoyote kumpata na nikimpa ndo atanijua sasa mi nani.

Akawa busy anamfata, anamsindikiza shule mda wa kutoka, katumia kama mwezi na kwa Wlater mwezi ni mwingi sanaa sawa na karne kumtongoza demu. Demu akaanza kuona kumbe Walter ni msweet, loooooooooh, akajilegezaaa. Wlater kambembelezaaa mpaka akakubali kwenda kwao wazazi wake wakiwa wamesafiri. Msitake kujua kilichomkutaaa." Wakawa wanamsikiliza kwa makinikutaka kujua kilimkuta nini. Akawaoneshea chupa tupuu manake Safari Lager zimeishaa hivooo waongeze ndo story iendelee. Wakatikisa tu vichwa na kumkazia. Baadae kwa tamaa ya story wakamuongezea bia zingine 3 na kumchimba mkwara zitoshee mpaka mwisho wa story.

Akanywa kwanza funda 3. Demu bwana alikuwa anaitwa Lucy dada, mlokole. Kaenda kwa Walter kwao kajiandaa kutoa mchezooo. Sasa sijui alipiga makelele sanaa akambore, sijuiii. Sijui alimngataa hatujuiii. Ila Walter alifumua fumua bikraaa, demu akaanza kujiliza kudekaa anajua sasa atamkteka Walter vizuri si kampa tamuuu brand new, thubutuuuuuuuuuu! Unaambiwa mchezo umeishaa Walter kamtimuaaaaa. Vaaa chupi uende kwenu. Haaaaaaaaa! Demu hakuaminiii nawaambia." Hahahaaaaaaaaaaaaaaa Halooooooooooo! Zikasikika kwa wingi sanaaa.

Tausi akaendelea kufungua page za file la Walter. Mlokole maumivu ya kutapeliwa bikra akaenda mpaka kwa mama yake kulalamika iweje amuharibu afu amuache. Mpaka wazazi kujua Walter kambikiri mtuuu. Dada akikaa anamsononekea bikra yakeee kutapeliwa kuleee. Loooohhh! Wakaaa mpaka vikao vya wazazi kwanini Walter amtoe bikra afu asimtake? Wapi mlokole alishindwaaa. Mlokole mwenywe mnafikiria nani kwani? Si mke wa mchungaji!: Hahahaaaaaaaaa! Halooooooooooooooo! Tausi tuachee si kwa umbeaaa huuu wenye S.L.P. Weeeeeeeeeeee! Huyu Mama mchungaji wa KKT. wakauliza kwa shauku. "Kumbee jeee, mi akiwa anatoa nasaha kwa mabinti nakumbukaga VAA CHUPI UENDE. Sasa sijui alikumbuka kuivaa hio chupi au aliicha kwa Walter, sahivi anajitia mtatakatifu kuliko baba mchungaji nyooooo." Hahahaaaaaaaaaaaaa! Kasheheeeeeeeeeeee ndani ya kirobaaaa!

Sijamaliza file la Walter, Muoneni vile vile anajichetuaaa. Sasa basi hilo dogooo, kuna demu alikuwa ana mdomoo hatariii, kwao kina uwezo uwezo kiongozi wa dini. Kutwa kuchakumsemaa Walter malayaaa, Walater muhuniiii, Walter hafaiiii. Walter anapewa tu data zake akasema huyu mbwa ngojaa si ananitaka kinguvuuu? Sasa subiriiii. Akamtongoza kistaarabu kama mtu vile. Looooh! Akamkubaliaa ila wafanye siriii. Mmmmmhhhh! Si ashampakaza Walter koteee. Walter akamkubali sawa siri. Weeeeeeeeeeeeee! Siku ya siku kamuita kichakani tu hata kwao hajampeleka.

Unaambiwa kajaza watu kibao nje ya kichakaa kawaambia demu nampa boloyanki huyu mpaka atatoka chupi mkononi. Wakambishiaa. Dakika 10 nyingiii. Mbona demu alitoka chupi mkononi anapiga mayoweeee kama chiziiii.Hamna aliemkamata hizo mbio zakeee. Katoka mkukuuuuuuuuuuuuuuu. Watu mpaka leo wanajuaga Wlater ana boloyanki kubwaaa, kumbe uhuni tu hana lolote. " Wkabakia mdomo wazi. mmoja akauliza Da Tausi hana lolote unamaanisha nini sasa yule dada alikimbia nini? "Bwana weee, Walter mshenziii tu, kumbe alikuwa na pilipili mfukoni, katika fower play kajitia kumpiga dada watu vinanda kumbe ndo anampaka pilipili ndugu yangu, pili pili kumkoleaa ndo kutoka ndukiii, alienda mpaka hospitali. Mnacheka mnadhania mazuri ya kucheka hayooo?. Wakabakia wanachekaaa tu.

Kilichosikitisha Wlater alimbaka demu wa mshikaji wake anaitwa Muddy huyu muuza mitumba wa sokoni. Grace na Muddy wameanza kitambo sanaa na hawaji kuachana wale. Kipindi hiko Muddy hajamla Grace bado Walter katumia mabavu kamla Grace. Kwa jinsi kapo yao ilivokuwa talk of the town kila mtu roho ilimuuma na ndo utawala wa Walter uliishia hapo. Alivofanya hiko kitendo ndo ikawa mwisho kabisaa wa watu wa mji huu kumuendekeza Walter.

Na kitendo cha Muddy kutomuacha Grace ndo kilizidi kufana walter aonekane Msengeremaaaa. Muddy alijua, mji mzima ukamchunia Wlater ila Muddy alikuwa anaongea nae kama kawaida. Sasa ile Muddy kutomchunia na ufedhuli aliomfanyiaa vikamfanya Walter akayeyukaaa kabisaaa. Akaacha umalaya jumlaaa, akaacha ukoraaa jumla, akawa kijana mpole, anashinda Garage kwa baba yao, ukimuona mahali yuko mdogo wake yule Wayne Baaaaaas. Ila kumuona ndo mpaka uende garage kwao. Yani ni nyumbni na hapo Garage. Ndo maana nyie wakuja hamuwezi kumjua Wlater nyie.

Grace na Muddy waliendelea kuwa wote mpaka form 6 wako wote. Muddy kafeli form 4 karudi Dodoma kalostiiiii, Gile mzazi wake kamuendeleza A level akirudi likizo yuko na Muddy. Chuo tukajua tapata wa huko msomi mwenzie walaaa, ndo kwanza yuko na Muddy. Chuo akikaa kidogo utaona Muddy kaenda Dar ili wawe woteeee. Wakirudi wako wooote. Wanavopendana sasa mpaka kerooooo. Muddy yule pale anauza nguooo mademu kibaooo wanajigongaa kwake lakini huwezi kumkuta ana demu mwingine. Mpaka washkaji zake wanamtania Grace kampa libwataaa.

Grace alivomaliza O level ana nati yake anakaa london akataka kupelekwa na mzee wake, akagomaa, kisa Muddy. Angeena ulaya wangeonana vipi sasa na Muddy? Oooooohhhh! Wenzio wanavopendana wale hela wanachanga. Grace akipata hela zozote anamgea Muddy afu Muddy sasa ndo anamuhudumia Grace kidogo kidogo kama mume chezeaaaa. Sahivi wamejenga nyumba sijui banda huko nje mji Muddy anavosema yeye Grace akimaliza shule anamuoa, Wanaenda kuishi huko. Baba yake Grace alivo na hela na ule mjumba waoooo, kaka zake wako Urusi na Marekani utaamini anakuja kwa Muddy hapo uswaziii. Anashinda pale kwenye mitumbaa siku nzima na Muddy na haoni kerooo. Kweli mapenzi upofuuuuuu. Analala pale uswaziii paa liko chini, jotooo, na anaamka asubuhi karidhika kabisaaa.

Siku ya zamu ya Muddy kusafisha choo na kufagia uwanja, kama Grace yupo anakuja kumfanyiaaa. Kama baba mtu yupo ana damka asubuhiii kwao kuja kufanya zamu ya FREE P Muddy. Hahahaaaaaaaa! Mimi Tausi baba yangu maskini wa kutupwa mjini hapa ila usengerema huo sijafanya badoooo. Hahahaaa! Ila Grace mwenzio pale ndo kafika beiiii, mwisho wa reli kigoma kwake. Hapo yuko field CRDB ila lunch anakuja sokoni kumfata Muddy ana nyege mbaya nae yulee, anaacha kuwaona maboss bank huko, watu wa maana anangangana na Muddy FREE P. Yule Lawyer Rweyongeza alitaka kumuoaaa, Grace kagomaaa kisa Muddy jamaniiii. Ooooooh!

Walter muoneni kakaa pale ndo nawaambia msione kobe kainama anatatunga sheria hivoooooo. Wkashusha pumzi sio kwa story ile.

Walter akiwa garage anafanya zake kazi kumsaidia mzee wake akasikia LALA CHINI WOTEE. Tobaaaaaaaaaa! Akastukaaa. Akajua mambo ya ujambaziii maana yalikthiri sanaa hapo Dodoma karibuni, Akachungulia akaona wako na silaha zao magobole (kama uliyaona haya kaolewe ushazeeka) Akawaza mle kuna hela za mjomba wake, afu maisha yao yamekuwa magumu sanaa, biashara sio, afu mjomba wao ana deni kubwa bank, mda wowote nyumba yao inauzwaa. Akahisi mahasira yake ya zamani yamempandaaaaaaaaaa. Alikuwa hajashikwa na hio mizuka siku nyingi sanaaa.

Akaendela kubana pale alipokuwa. Zile hasira zake na ile hali hali yake ya kupiga watu ikamjia kwa kasi, akajikuta katokaa mafichoni. Akanza kupamba nao wale majambazi. Pigana pigana nao kama sterling Van Dame. Pigana na wewe na wale majambazi sio watu wa mkono. Wakachezea kichapo toka kwa teminator Walter. Aliwakungutaaaaa mpaka wakazimia. Wakaka wanne wote kunguta kungutaaa, piga piga nawewe wakwa nyang nyanga na hivi ana ugwadu hajapiga watu kwa miaka kama mi 4 hivi basi akakata kiu yake kabisaaa.

Watu wote wakaikmbia akabaki peke yake na wale mizoga wanaopumuaa, hapo akili inamchemkaaa wanamuogopa hakawiii kuwachanganya na wao. Akakusanya vile vigobole vyao vi 2, akawafunga kamba wote wannne akaanza kuwaburuza mtaani kuelekea polisi. Gobor zake begani. Njia nzima wanamtolea macho.

Kafika polisi kawaburuzia ndani. Polisi wakaitanaaa. Akatoa maelezo walikuja kutuvamia na magobole haya nimedhibitiii na ndo nimewaleta hapa. Akaulizwa peke yako akajibu ndio peke yangu. Polisi kuwaangalia kwa ukaribu si ndo kujua ndo mijambazi sugu inayotafutwa Dodoma nzimaaa. Mara ya mwisho na polisi kweny mapambo waliua polisi wa 4. Akakimbia kumuita mkuuu wa kituo. "Bosi kuna kijana kwaleta kina kanjanja kawadhibiti peke yake anawaburutaa boss njoo uone wenywe kabisaa." Boss akashangaa masihara hayo kina Kanjanja most wanated?" Ndio bosss. Boss akainuka, akauliza"Na Kanjanja klaletwa?" Akajibiwa ndio boss" Akatoka kuja kujionea akamkuta kanjanja hoii kwa kipigooo.

Wakampongeza Walter kwa ujasiri wake na kumshukuru wkawaingiza kina kanjanja mahabusuuu. Wakapiga simu kwa Mkuu wao DSM. Kesho mkuu akaja, akauliza wako wapi kina Kinjanaj? Akawaona akasema pakia nao naenda nao DSM. Njiani wakasimamisha gari porini, akaamuru washushwe. "Mimi nina lengo la kugombea ubungee staki ungese kwenye azma yangu hio. Nipe bastola Coplo" Akapewa. Akawalamba shaba kina Kanjanja wote wa 4. Wakafa hapo hapo. Akasema naomba wapige muhuri hao. Biashara ya ujambazi Dodoma imeishia hapa. Unajua cha kufanya na hio miili ianze kutokea mtaani na maadamu muhuri uko fresh sitegemei kelele zozote" Akajibiwa "Sawa mkuu"

Akaingia garini, akamwambia dereva geuza gari tunarudi Dodoma. Dreva kashangaa ila akaa kimya tu. Dodoma hakurudi kituoni akaenda kumuulizia Kijana aliekamata majambazi 4 jana na kuyaburuta. Watu wakamuelekeza kwa kina Wlater. Akafika mpaka kwao akashukia mbali kidogo na kumwambia dreva wewe nenda kalale kesho tukutane stand kwa safari kuna kazi moja ya mwisho natakiwa kuifanya.

ITAENDELEA.
 
duh! si kwa mwendokasi huo....Walter jamani nakuelewa sasa
 
Tamu tamu ila kaka police usitake tu kujichanganya Walter asije mgawa vipande vipande
 
Naandika hapa inaendelea kwa team popo. Inaendelea ya leo ukweli 200%
 
Nimeshtuka usinginz ndo nasoma ....dahh lara ww bhana so vizur ujue
 
DARESALAAM 1993.

Idriss kama nilivokwambia nimepokea simu toka Manchester kwa yule babuuu wa kule kuna posa ya Iqra. Bibi akapozi kwanza kumsoma Idriss maneno yake ameyapokeaje. Idriss akawa anamuangalia kwa jicho kali sanaa hakusema chochote. Bibi akamuuliza mbona husemi jambo Idriss nakuwa kama nazungumza mwenywe kama redio inakuwaje sasa hio.

Idriss akamuuliza kwa hio wataka niambia Babuu ndo ataka kumuo huyu Iqra wetu wa miaka hio 12 ama? Bibi akacheka kwanzaaa. Idriss wala hakuchekaaa. Bibi akasema sio babuu bwanaa, uzee ule mke atamuwezea wapi, anamposea mjukuu wake yupo huko huko London mwana wa mwanae wa kwanza. Sasa kwa miaka hio 21 kajua Iqra hana miaka 2 au mitatu anakuwa sasa hivi ndo kaona tangulize posa maana Iqra binti mzuriii, mwenye akili na anaijua dini kuwashinda hata hao wanaume.

Idriss akanyamaza kwa mda, baadae akamuuliza bibi, eti mama kwa mfano, sio kwamba ndo nasemeaaa, kwa mfano tu yaaani nauliza kimfano nisipotaka Iqra aolewe, nikata asome aendelee na shule maana hapo tumemrusha madarasa akili nyingi sana yupo form 2. Mfano nikitaka asomee mpaka chuo au atakapochoka yeye nitakuwa nakosea mama?

Bibi akatafakariii, akasema kiukweli utakuwa hujakosea manake hamna dhambi mzazi kutaka bintie asomee, lakini kama ujuavyo sisi waarabu tunaoa na kuolewa wadogo sanaa, mimi kuwaacha nyie msome ndo mmekuja kuoa wazee, mmeoa watwana, mmeoa makafiri, elim hii ya mzzungu ina faida ila ukiichunguza kwa undani in hasara nyingi sanaa. Nyie watoto wa kiume, kuipata hio elimu ya mzungu kidogoo tu mmenisumbua sio kitoto, mmeniadhiriiiii, mmenianikaa hadharani, watu wote wamenichachafya si tulisemaa tulisemaa, basi tu vile niliwazaa mwenywe ila mmejua kunikomeshaaa kabisaaa.

Nachowaza mimi nyie wanaume mmefanya hayo huyu Iqra wakike. Utasema umuache asome atajifunzaa zinaa huko shuleni mwishowe atazalia hapa hapa na asiolewe kabisaaaa. Nawaambia. Mie pia kwa akili za Iqra kukaa ndani aseme ampikie mume ni hasara tena sanaa, lakini mila zetu sisi waarabu na dini yetu ya Uislaamu inasisitiza umuhimu wa kuikwepa zinaa na kufata maagizo ya mtume.

Huyo babu ni mtu wa dini, dini anayo sanaaa, mjukuu ake huyo Jabir nilivopeleleza ni kijana katulia sanaa, ana dini mnooo mnooo, sasa sioni kwanini tuikatae posa yao. Na posa yenyewe keshawaambia baba zako wadogo na wakubwa wa Oman tutakataa vipi sasa unadhani. Manake kila siku simu hapa toka Oman, huko London, UK zaulizia inakuwajee majibu ya hio posaaa na kama bibi harusi mwenyewe ashaambiwa kapata mchumba, na ashaanza kutayarishwa kwa ndo pindi atakapo kua tu. Idriss unaelewa mziki wa hili swala si mdogo, naanzaje kukataa wakati baba zenu washaonesha dalili zote za kukubali.

Idriss akawazaa na kuwazua, akasema embu jaribu kuzungumza nae huyo Iqra uone mtaishia wapi na msimamo wake ni nini haswaa kwenye hilo swala la ndoa. Je yeye ataitaka hio ndoa ama la, na kwanini. Uzuri Iqra mwenywe dini anaijua sana, aiaelewa kwa mapana mnoo kwa hio kuelekezana nae itakuwa sio kazi mwenywe anajua dini inatakaje ngoja tuone itaamuaje.

Wakaanua jamvi lao la maongezi na bibi akakabidhiwa jukumu la kuongea na Iqra waone msimamo wake umekaaje juu ya hilo swala zima la ndoa.

Siku hio Iqra kakaa dukani, katoka shule tayari, kava zake Abaya na Nikab katulia counter dukani kwa marehemu mama yake anapokea hela. Basi wateja wanajigonga sio kdogooo. Wanashaukwaa sio kidogoo. Si waarabu wa hapo kariakoo wala wa Ilala wala Kinondoni, kila siku waja pale dukani kunua vitu hata ambavo hawaitaji ili wawe tu wanamuona Iqra na kumsalimia, kujiongeleshaa, na kutaka kumzoeaaa.

Babuu Ali ambae ni muuza duka wa hapo siku nyingi kabla Iqra hajazaliwa akamuaga Iqra mama naenda kwa mzee pale chini nina mazungumzo nae kidogo. Iqra akamjibu sawa Babu Ali ila ongozana na Fahad si unajua wateja wakijaa hapa nitashindwa kumuangalia vizuri. Babu ali aksema sawa mamangu nitaenda nae. Fahad akawa hataki kwenda na babu Ali anataka abakie na Iqra maana Iqra ndo roho yake. Iqra qkqmfanyia ukali aendel na babu Ali.

Babu Ali kufika kule akamkuta mzee anasinzia, akamwambia Babu kwema mbona mmekuja huku mda huu? babu akamwambia nina maongezi na wewe Idriss hayawezi kusubiri nimemuomba ruhusa bibie Iqra kanipatia hio ruhusa. Idriss akamuita chemba haya nambie Babu Ali, Fahad akawa anachezea mabox huko stoo. "Bwana Idriss nina taarifa kidogo sio nzuri sanaa, kule dukani binti kakua yule apendezaa, sasa vijana wanjaa jaa bila mpangilio. Wimbi la vijana wasio eleweka limekuwa kubwa sanaa pale dukani na cha kushangaza mda Iqra anaoanza kuuza hao wateja wa ajabu ajabu ndo wanjaaa. Si wahindi si waarabu mpaka wanitia shaka. Sasa mtoto mdogo yule mpaka naogopa nikasema labda nikwambie umkataze kuja dukani ama sijui tufanye vipi. Bosi wangu Idriss mie nimeangalia ile hali nikaona hataa sio sahihi vile mambo yanavyokwenda nikasema nije huku nikwambie utajua cha kufanya wewe mwenywe. Hali ni mbaya juzi kaja mkaka mtu mzima anangania Iqra aonane nae Polic Messy mpaka ikabidi niingilie kati kumfukuzaa yule mtejaaa nikamchana tu wewe una habari huyu binti hana miaka 13? Huna hayaaaa!"

Idriss akawazaaaa na kuwauzaa akamwambia sawa nimekusikia, sasa Babu Ali kama ujuavyo huyu Fahad yupo slow, huyo Iqra mi ndo namtegemea kumuongoza Fahad mbeleni hukooo, Ila hili ulionambia nalo si la kupuuza hata kidogoo. Sasa sijui nifanyaje. Sijuiiiii. Nashukuru kwa taarifa. Babu Ali akagaa akaondoka, Fahad akakomaa kubaki kwa baba yao pale pale.

Iqra akiwa hana hili wala lile jioni akaitwa na baba yake na bibi akapewa taarifa za posa akastukaaaa! Bibi anamtia moyo hata yeye aliolewa na miaka 14 sio ajabu kabisaaa mmmmmhhhh! Iqra ni mtu mwenye misimamo yake mikali pale pale akawastopisha kwamba yeye haolewi. " Akamwambia baba mie sijawahi kukukosea na sipendi iwe hivo, hio ndoa kama ni kitu ambacho unakitaka mie mwanao ningependa nikupe heshima hio lakini sasa kuna tatizo moja nyie hamliangaliiiii. Wakawa wanamsikiza kwa makini wote wa 2.

Huyu Fahad mimi na nyie ndo tunamuweza. Mtu mwengine hamuweziiii. Kumbukeni shule anaenda sababu mimi kila siku lazima nimpitishe shuleni kwao, na nimfuate bila hivo hakubali mtu yoyote. Jioni nikiwa nasoma na yeye anakuja tunasoma wote nakuwa namfundishaa na yeye. Na navomfundisha mimi anavielewa na kuvishika sanaa tofauti na walimu. Mimi ndo dunia yake, mimi ndo roho yake, mimi ndo mama yake. Sio rahisi, wenzangu wananiona naenda shule kumfata wananitania mda mwingine mdogo wake tahiraaa, mdogo wake chizi chiziii, mdogo wake mwenda wazimuuu zimeruka akili kidogo mimi navumilia sio kama wasichaa wengine wa umri wangu wana marafiki, mashosti, mi sababu ya huyu Fahad sina rafiki mimi, sina shoga niko mwenywe mwenywe.

Shule tulivokuwa wote primary mimi ndo nilikuwa namuangalia asipate matatizo yoyote, mda wote nilitaniwa mimi, nilionewa mimi, nilisimangwa, nilidharaulika il Mungu ananiona Wallahi sijawaji kumtenga Fahad Mama yangu mzazi ananiona huko alipo. Sahivi break lazima nije geti la primary kumangalia kama kakumbuka kula navitu vingine. Fahad huyu msalaba wangu mimi apa. Nikiwa hai na nasoma Fahad atafika mbali. Nyie kesho hamtokuwepo nitabakia mimi na Fahad sasa sitaki kumkatia tamaa, nitahangaika nae hivi hivi. Nataka nisome niwe na maisha ya kueleweka nimtunze huyu Fahad na mkewe maana kusema itafika siku ajitunze atunze na mke kwakweli ni kuomba Mungu.

Naweza sema niache shule, niende London nikaolewe na huyo mtu, lakini Fahad anabaki vipi sasa, shule ataacha, atasinda nmbani peke yake atazidi kuwa mjingaa, siku hampo na bibi huyo bwana atakubali kukaa na Fahad au huyu Fahad ataishi vipi sasa peke yake? Huwezi sema ndugu yetu yoyote atamtunza huyu Fahad kama mimi, haiwezekani. Mimi huyu ni msalaba wangu nitaangaika nao mpaka Mungu atavosema basi. Labdaaa Mungu akijalia nipate mtu muelewaa, anipendee sanaa ndo akubali kunioa na Fahad aishi na sisi mbeleni huko. Ila kwa sasa hivi hapana naombeni mniache nisme na Fahad.

Bibi na Idriss wakabakia kimyaaa, hamna alietia nenooo. Kikao kikaishia kwa ukimyaaa huo, kila mtu akanyanyuka kimya kimya kwenda chumbani kwake kulala pasipo kumsemesha mwenzie. Watasema nini sasa.

Kesho wakiwa shuleni class mate wake Nadya akamuuliza Iqra kesho utakuja kwenye birthday yangu? Iqra kiukweli alitaka kwenda sanaa sababu hakuwa na marafiki wengi na hao wachache hakutaka kuwadisappoint. Akamwambia Nadya mimi napenda kuja ila siwezi kuja na Fahad, si unamjua mdogo wangu yule hayupo vizuri nitakuariba sherehe yako. Atafanya mambo ambayo mtachukia kwenu. Nadya akasema bwana Iqra sasa nitamlisha keki nani kama best friend. Iqra akasema nitajitahidi.

Kesho yake akamuomba bibi amuangalie Fahad aende kwenye party, bibi akakubali. Akaenda kwenye hio party na ndo party ya kwanza iso ya darasani yeye kuhudhuria. Akafurahii kuona mapambo ya kisasa, music, cake, watoto wanafurahii, Nadya kapendezaaa, akaipendaa na kutamani kabisaaa na wao wafanye kitu kama kile kwao maana kwao hamna wageni wengi wala nini. Akalishwa keki na Nadya.

Sasa kaka yake Nadya akawa kmuona Iqra akawa kaganda kama lubaaaa. Sherehe nzima yuko nae benet, ndo keshamuelewa sasa. Na Iqra nae alishaanza kuona darasani watu wana ma BF na yeye akawa anaamani iwe hivo. Tatizo vibwana vya shule vikawa vinaogopa kuwa bullied na maduu wa shule maana walikuwa wanamuandama sanaa Iqra sababu mzuriii afu kichwaaa cha hatari darasani. Na kubwa ni Fahad ndo waliokuwa wanamuandamia.

Kaka yake Nadya alikuwa mkubwa tu anafanya kazi kama 20yrs hivi, akaona huyu labda atakuwa mulewaaa wa situation ya Fahad. Na huyo kaka alikuwa mzuriii, anaeleweka. Iqra akajiongezaa, wakazoeana akamwambia nitakuwa nakuja kukuona dukani kwenu. Party ikaisha akarudi home Fahad akawa amemisi balaa, ila yeye design akaanza kuona Fahad atambana kwenye mambo yake. Upendo ukawa umepungua kidogo.

Dukani Iqra akaenda kumuacha Fahad kwa baba yao ili apate chansi la kufanya umalaya wake aliouanza vizuri. Huyo kakake nadya, Ghadaar akawa kaja pale na wenzie masharo baro, Iqra anajitia nae mkubwa kawakaribisha soda na nini, anajitia boss lady kumtumikisha babu Ali, mmmmh! Babu akawa anamuangalia tuuu. Wakapiga piga story wakaondoka. Babu Ali hakutaka hata kumwambia Idriss angeumia akawa anamtizama tu Iqra.

Ikawa ndo mchezo huo kumuacha Fahad kwa baba yake, ama la anamtuma babu Ali ampeleke kule mpaka buzi lake liondoke. Ikaenda miezi hio tabia, akabadilika kabisaaa, babu Ali akawa anamsikitikia tu mienendo yake sio mzuri. Swala anarukaaa, yaani haeleweki kabisaaa. Nguo kila siku ananunua mpya na hivi baba yake mpole anamdanganya danganya tu.

Siku ya siku akamwambia babu Ali aondoke na Fahad, babu Ali walivofika njiani akawaza yule kijana mshenziiii tu atamuharibia Iqra maisha labda wakirudi akifanukiwa kumuonseha Iqra yule kijana sio mtu mzuri itasaidia kidogo kumrudisha kwenye mstari. Akarudi na Fahad hakuingia ndani wakwa wamekaa njee.

Iqra yupo na Ghadar counter ndani, kampani ya Ghadar wako dukani kwa nje kujishongondoaaa, utadhani duka lao, ujana mwingi na nini wakamuona Fahad anarudi akaingia dukani babu Ali akabana nyumaa. Fahad anapenda wageni sanaa kuwaona wale vijana walikuwa na mpira wao akawafata kutataka ule mpiraa. Wakaanza kuambiana yule chiziii huyu hapa.Yule tahiraa wa Aghakan kumbe anakujaga hapa dukani kwa kina Iqra.

Wakaanza kumsema Fahad vibaya wanamdhihaki na kumpiga masingi na kumkejeli sasa yeye haelewi anaona sawa tuuu. Babu Ali roho inamuuma mpaka basi. Akaingia ndani kumfata Iqra akakuta yupo kwenye maongezi ya hubaaa. Akmwambia Iqra njoo nje mara moja. Iqra akastuka Babu Ali! Heeeeeeeee! Umerudi kufanya nini? Yule mtu umemuacha kwa baba? Akapanic hatariiiii. Akamwambia Ghadar tupishe mara moja.

Ananza kumfokea babu Ali. Babu Ali akomaa njoo nje tafadhaliii. Kutoka nje ndo kuwakuta wale Ghadar na marafiki zake wanamdhihaki Fahad. Wanamsemaaa, wanamsimangaa, wanadhihaki na kumccheka. Heeee hili tahira kweli. Akili yake haiko vizuri si unalionaa, aya shika mpiraaa, Anajitia anaurusha afu haurushi, Fahad anahaha kuutafuta wanamchekaa, wanamchekaaaa. Moyo ukamchoma Iqra akashindwa kuvumilia akaingilia kati na kuwaambia huyu tahira ni mdogo wangu na nampenda sanaaa. Akamwambia Fahad njoo. Wakashangaa wale wakaka. Ghadar akamuuliza ina maana huyu chizi ni ndugu yako kabisaa? Wakaangaliana wakaanza kuwacheka. Wenzie wanamtania Ghadar kidogo ungeoa dada yake chizi. Oooohhhhhh! Shauri yako. Ghadar yuko nashangaa, afu hata hajaniambia huyu malayaaa, angeniingiza mkenge mbaya! Iqra akamwambia naomba muondokeee

Siku ikawa nzito sanaaa. Akamwambia utafunga duka na kupeleka funguo kwa baba mi naumwa naenda nyumbani kulala. Kafika kajilaza bila kula wala kuogoga. Fahad anamwambia bibi yake Iqra kagombana na mchumba wake. Bibi anashangaaa! Mchumbaaa? Ndio, mchumba ake na rafiki zake wameninyima mpira wao wa kuchezea, wakawa wananicheka na kunisemaa Iqra akaja kunitetea. Bibi akajua mazitooo.

Usiku akamfata chumbani Iqra mama kwemaa? Iqra kavimba macho kilio. Teenager. Bibi akamuuliza nini tatizo? Iqra akamjibu hivi bibi haujawahi kutamani hata siku moja huyu Fahad afe uishi maisha yako mengine bila huyu Fahad? Bibi akasikia mkuki wa moyo umemchoma. Akataka kusema kitu ila akakaa kimya dakika kadhaa, akaondoka kimya kimya

ITAENDELEA.
 
Kweli hii stori haitakiwi kuitabiri, inabadilika badilika kadri episode zinavyoendelee.....much respect lara 1
 
Back
Top Bottom