We Dada kama umo humu asante sana

We Dada kama umo humu asante sana

Aaah jamani.......si ulinishukuru ya kutosha.......sasa mpaka huku......
Ukienda huko unakokwenda uniletee pafyumu..........

ah ah ah ah....ungekuwa ww ndio umetoa huo msaada ungeshakuja kutengezaza uzii....
 
Ina dili sana sometimes huwezi kufungua a/c au kudraw hela bila passport

Weee
Benki hizi hizi za tz????

Watz wangapi wenye passport mpaka hicho kiwe kigezo cha lazima???
 
Ni muda umepita nilikuja Benki kwenu kutoa Pesa kwa Western union (Hata hivyo sikufanikiwa) ukaniomba kitambulisho ikabidi nikupe Passport yangu. Leo nilitakiwa ku submitt Passport yangu ubalozini kwa ajili ya visa ndio Nahamaki kumbe sina Passport na sijui ilipo. Nimetafuta sana ndani ya nyumba na ndani ya gari na kuuliza watu mbali mbali bila mafanikio.

Nimechanganyikiwa hadi kidogo nipate ajali barabarani. Mara nikakumbuka kuwa mara ya mwisho niliitoa kule Benki.... na kukupa wewe kama kitambulisho. ikabidi nije huku nikiwa nakumbuka akilini kuwa niliichukua kutoka kwako na kurudi nayo. Hivyo nilikuja ili tu kupata uhakika kuwa niliichukua kwako. Wakati nimefika nakutana na suprise ya passport yangu hadi nashindwa kuelezea shukrani zangu.

Nakushukuru kwa kuchukua na kuitunza Hati hiyo na nakueleza kuwa maneno ya shukrani bado nayaumba ili nije nikushukuru. Labda siku moja nitakununulia Dinner pale....

Ubarikiwe sana sana sana.

Hivi unajisifiaje hadharani kwa kutokuwa makini kabisa kwenye maisha yako. Hivi dhamana uliyopewa kazini kwako au kwenye biashara yako uanaitendea haki kweli.
 
Mie nilichoelewa, una passport, una account western union,huwa unasafiri nje ya nchi, una gari,
hayo mengine mbwembwe tu maana kama kushukuru ulishamshukuru, ungetaka mengine ungechukua namba yake umshukuru weeeeee mpaka ashukurike.
 
Hivi unajisifiaje hadharani kwa kutokuwa makini kabisa kwenye maisha yako. Hivi dhamana uliyopewa kazini kwako au kwenye biashara yako uanaitendea haki kweli.

Usifikirie hivyo mkuu sisi ni binadamu kusahau huwa kunatokea
 
Mie nilichoelewa, una passport, una account western union,huwa unasafiri nje ya nchi, una gari,
hayo mengine mbwembwe tu maana kama kushukuru ulishamshukuru, ungetaka mengine ungechukua namba yake umshukuru weeeeee mpaka ashukurike.

Ni sahihi kwa uelewa wako kuelewa hivyo ndio maana hatuko sawa.
 
Nazungumzia nje,tz kutambulisho kinatosha

Nilitoa cha kazi hakikukubalika it was either driving licence or passport kwa options nilizokuwa nazo na mimi licence sikuwa nayo karibu
 
Kuna kila dalili ushamtamani, unakoelekea ni kumuomba kitu.
 
Back
Top Bottom