Ni muda umepita nilikuja Benki kwenu kutoa Pesa kwa Western union (Hata hivyo sikufanikiwa) ukaniomba kitambulisho ikabidi nikupe Passport yangu. Leo nilitakiwa ku submitt Passport yangu ubalozini kwa ajili ya visa ndio Nahamaki kumbe sina Passport na sijui ilipo. Nimetafuta sana ndani ya nyumba na ndani ya gari na kuuliza watu mbali mbali bila mafanikio.
Nimechanganyikiwa hadi kidogo nipate ajali barabarani. Mara nikakumbuka kuwa mara ya mwisho niliitoa kule Benki.... na kukupa wewe kama kitambulisho. ikabidi nije huku nikiwa nakumbuka akilini kuwa niliichukua kutoka kwako na kurudi nayo. Hivyo nilikuja ili tu kupata uhakika kuwa niliichukua kwako. Wakati nimefika nakutana na suprise ya passport yangu hadi nashindwa kuelezea shukrani zangu.
Nakushukuru kwa kuchukua na kuitunza Hati hiyo na nakueleza kuwa maneno ya shukrani bado nayaumba ili nije nikushukuru. Labda siku moja nitakununulia Dinner pale....
Ubarikiwe sana sana sana.