Wazoefu wa mambo ya familia nipeni ushauri

Justine Marack

JF-Expert Member
Jul 31, 2014
567
1,550
Huyu mwanamke tumekua kwenye mahusiano kwa zaidi ya mwaka. Katika kipindi hicho alikuwa anaishi kwao. Wakati tunaanza mahusiano alinieleza kuwa tayari ana mtoto wa kiume. Na kwasababu pia Mimi nilishapata Mtoto huko nyuma sikuona tatizo. Huyo mwanaye baba yake yupo na maisha yake mengine safi tu.

Baada ya kungoja sana mambo yake sawa, tukafikia kuamua kuishi pamoja angalau kwa kuwahusisha wazazi hasa upande wake. Binti ikabidi aje tuishinaye vkwangu. Hapo awali tulikubaliana kuwa huyo mwanaye atabaki kuishi kwa bibiyake na tutamuhudumia akiwa huko.Mimi mwanangu Yuko shuleni na akiwa likizo anakuja kusalimia na kurudi kwa mama, maana yeye ni wa kike.

Sasa baada ya miezi mitatu ya kuishi naye, huyu mwanamke alisubiri nikiwa safari akaenda kumleta huyo mwanaye aje aishi hapo. Pia hakuishia hapo akabeba na watoto wawili wa dada yake nao kaleta hapo na Sasa Kuna watoto watatu.

Nimesafiri tena na kurudi na bado nawakuta na hawana mpango wa kuondoka. Tayari anawaweja kwenye mipango na bajeti zetu kama wangu vile.

Binafsi napenda kuishi na Mtoto ambaye nakuwa huru naye. Yaani hata nikimuonya asichukulie kama namtesa. Kuna mambo yanafanyika nakaa kimya lakini nimegundua hiyo inanitesa Mimi.

Tafadhali nipe USHAURI wako. Hapo nifanyeje ili nipatie amani bila kuonekana Nina roho mbaya?
 
Pole ila kama mlishaongelea hayo maswala ya watoto kabla namna mtakavyo kuwa mnaishi nao na yy kafanya kinyume na mlichokubakiana ww wala usipanic mnafutie mda mzuri uzungumze nae anaweza kuwa na yy Hana Nia hiyo ambayo ww umeshaiamini ila umeakua na haraka tu ya kuhukumu.... Ila kama atakuwa amekiuka makubaliano yenu basi usisite kufanya maamuzi mapema kumbuka kwenye maamuzi lazima Mmoja wenu a lose zaidi ww utamuua
 
Angesubiri hata mzae mtoto wenu kwanza. Pole mkuu ila ongea naye arudishe watoto wa watu (hao wawili).
Huyo wa kwake mvumilie tu mkuu mama kukaa mbali na mwanaye wa kumzaa huku ana maisha mazuri ni mtihani sana. Anakuwa anatamani kila anachokula na mwanae angekula.
 
Huyu mwanamke tumekua kwenye mahusiano kwa zaidi ya mwaka. Katika kipindi hicho alikuwa anaishi kwao. Wakati tunaanza mahusiano alinieleza kuwa tayari ana mtoto wa kiume. Na kwasababu pia Mimi nilishapata Mtoto huko nyuma sikuona tatizo. Huyo mwanaye baba yake yupo na maisha yake mengine safi tu.
Piga chini hiyo mama haiwezekani ikiuke makubaliano huo ni utovu wa nidhamu
 
Huyu mwanamke tumekua kwenye mahusiano kwa zaidi ya mwaka. Katika kipindi hicho alikuwa anaishi kwao. Wakati tunaanza mahusiano alinieleza kuwa tayari ana mtoto wa kiume. Na kwasababu pia Mimi nilishapata Mtoto huko nyuma sikuona tatizo. Huyo mwanaye baba yake yupo na maisha yake mengine safi tu.

Ww ni mwanaume speakup man, kukaa kwako kimya ataendelea kukujaribu kidogo kidogo mwishowe familia nzima itahamia hapo
 
Screenshot_20230621-112937_(1).png
 
Huyu mwanamke tumekua kwenye mahusiano kwa zaidi ya mwaka. Katika kipindi hicho alikuwa anaishi kwao. Wakati tunaanza mahusiano alinieleza kuwa tayari ana mtoto wa kiume. Na kwasababu pia Mimi nilishapata Mtoto huko nyuma sikuona tatizo. Huyo mwanaye baba yake yupo na maisha yake mengine safi tu.


Tafadhali nipe USHAURI wako. Hapo nifanyeje ili nipatie amani bila kuonekana Nina roho mbaya?
Sipendagi sikia Kuna wanaume dhaifu kama wewe.mpaka mke anaaamua maamuzi ya kuleta watoto bila kibali chako ujue ashakupanda kichwani..

Wanaume wengi mnaongozwa na wake zenu ..mmepoteza sifa ya uongoz aliowapa Mungu.
 
Sipendagi sikia Kuna wanaume dhaifu kama wewe.mpaka mke anaaamua maamuzi ya kuleta watoto bila kibali chako ujue ashakupanda kichwani..

Wanaume wengi mnaongozwa na wake zenu ..mmepoteza sifa ya uongoz aliowapa Mungu.
Imagine,hivi kwa akili ya kawaida inaingia akilini
Kumleta mtoto haikuwa shida ndo iwe bila taarifa,umeoa au umeolewa?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Imagine,hivi kwa akili ya kawaida inaingia akilini
Kumleta mtoto haikuwa shida ndo iwe bila taarifa,umeoa au umeolewa?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
hapo mtu keshaolewa..na yajayo yanafurahisha...!!

Mke kama ana maamuzi kama hayo ktk familia bila baba kushirikishwa basi mengi anaamua mwenyewe..
 
Back
Top Bottom