Waziri wa Nishati amzuia Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO na wenzake kuhudhuria Mkutano ili washughulikie suala la Umeme

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko amesema “Tangu nimeteuliwa nimeelekezwa na viongozi wangu kuwa tufanye kila tunaloweza kuhakikisha mamivu ya mapungufu ya umeme tunayapunguza.

“Tunafahamu kuwa ukuaji wa uchumi ni mkubwa kwa watu wetu lakini vyanzo vyetu vya umeme bado ni vilevile, lazima tuongeze vyanzo vingine ili kuwa na umeme wa uhakika kwa ajili ya shughuli za kiuchumi.

“Kuna ripoti imetoka ikionesha Tanzania ni moja ya Nchi ambazo zinakua vizuri kiuchumi Afrika maana yake mahitaji ya umeme yataendelea kuwepo.

“Niwatoe wasiwasi Watanzania kuwa Rais na wasaidizi wake tunafanya kila tunaloweza upatikanaji wa umeme unakuwepo na hiki ni kipindi cha mpito wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linakamilika.”

=============

Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko amewaagiza Watendaji Wakuu wa Nishati akiwemo Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Maharage Chande kutohudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Nishati unaoendelea Jijini Dar es salaam leo na badala yake waende kutatua tatizo la upatikanaji wa umeme ambao kwa sasa unasumbua Wananchi.

Akiongea mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Biteko amesema Wananchi wanachotaka kwa sasa ni upatikanaji wa umeme wa uhakika na kumaliza mgao ambao unaendelea hivyo amewataka waende kusimamia kuhakikisha umeme unarudi katika hali nzuri kama zamani.
 
Huyo nyati mjane hana akili wakate na kwake basi ivi anajua tunavoteseka eti kipindi cha mpito sura kama nyati mjane
 
Kizimkazi hata hajui kama tarehe 19-9-2023 watanganyika walikua gizani. Nae waziri analeta ngonjera zile zile za kipara. Mpk bwawa likamilike lini? Takataka tu
Kipindi cha mpito, wanamaanisha tuendelee kuvumilia mpaka Bwawa litakapokamilika, yaani June 2024

Wanajua mtakimbilia kwenye majenereta, kule wameongeza tozo kwenye wese, na wao ndo waagizaji wa wese...mpaka November 2025, mfuko mnene, wananunua tena UONGOZI
 
Huyu wanamgombanisha na wananchi ,bado waje wamtumie wapate kura kule ziwani halafu mtoto wao mpendwa wanampeleka mafichoni asichafuke …Atafika 2025 mchovu sana
 
"Tumewaambia viongozi wa wizara ya Nishati wala huku msije na hawako humu ndani". Sasa wasipokuwepo ndiyo uzalishaji wa umeme utakidhi mahitaji? Au anataka kutiambia Kuna pahala huwa panavuja?
 
Biteko kiongizi wangu nakuamini uongozi wako! Kuwa makini na hiyo wizara itakuchafua. Hujui kuwa malope kaharibu kila kitu halafu umedondoshewa jumba bovu.
 
Kipindi cha mpito, wanamaanisha tuendelee kuvumilia mpaka Bwawa litakapokamilika, yaani June 2024

Wanajua mtakimbilia kwenye majenereta, kule wameongeza tozo kwenye wese, na wao ndo waagizaji wa wese...mpaka November 2025, mfuko mnene, wananunua tena UONGOZI
Sisi waafrika miongoni mwetu kuna watu wenye roho ngumu sana.

Hata Libya ambayo haikuwa na tatizo la umeme kwa miongo kadhaa juzi mabwawa mawili yamevunjika na kusababisha maafa watu zaidi ya 11,000 wamefariki kwa mafuriko na kusombwa hadi baharini.

Lakini kumbe zile serikali mbili moja Tripoli na ingine Benghazi zilikuwa "busy" kugombea rasilimali na kusahau kupeleka fedha kwenye mabwawa ili yafayiwe matengenezo na uboreshaji mwingine.

Yaani wale wote waloshiriki vita vya wenyewe kwa wenyewe ndo haohapo wapo na kazi ya kulihujumu taifa hilo ambalo miaka ya nyuma lilikuwa moja ya mataifa bora kabisa barani Afrika.

Nimeamini kweli hivi viinchi vidogovidogo viitwavyo Jamhuri ya Wapigaji vipo barani Afrika ni chanda na pete za nchi husika.
 
Kizimkazi hata hajui kama tarehe 19-9-2023 watanganyika walikua gizani. Nae waziri analeta ngonjera zile zile za kipara. Mpk bwawa likamilike lini? Takataka tu
Subirieni mnyolewe mlisema tatizo ni Waziri Makamba 🤣🤣
 
kwani ngosha wana man na kina kalemani walikuwa wanafanyaje, mbona kukatika kulikuwa nadra...nahisi kua kamchezo fulani, kila pian changamoto ya viongozi wa nchi hii sio watu wa kufikiri na kutafuta suluhisho, ni watu wanaokariri ufanyaji kazi kama kasuku, na mara chache kiongozi huja na new idea ya kutatua changamoto, wengi hufanya kazi kwa job description, sasa pamoja na nchi kuwa na jeographia inayoruhusu vyanzo vingi vya umeme, ila bado tunakomalia umeme wa maji tuuu, na sasa tumepata kisingizio kuwa tusubiri bwawa likamilike... nlitegemea aseme kuna proposal za kubuni vyanzo vipya vya nishati wataalamu wa wizara wana fanya tafiti ili tuanze, kwani dunia nzima chanzo cha umeme ni mabwawa tu? kwann hatujifunzi na kwingine?
tanesco ingeweza kuwa na vyanzo tofauti na sio lazma umeme huo uwe supplied nchi nzima, chanzo fulani kinaweza kutatau shida ya umeme kwenye mkoa kilipo ili kupunguza load kwenye hizo gridi za taifa... nliwahi kusikia tpc wana uwezo wa kuzalisha umeme na ku su supply kilimanjaro yote,ila hawakuruhusiwa.. wangekubaliwa na serikali moja kwa moja mkoa mmoja ungeshapunguziwa stress za umeme tubaki kupambana na maeneo mengine.

hyo mibosi imekaa tu ofisini haina plan b.
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko amesema “Tangu nimeteuliwa nimeelekezwa na viongozi wangu kuwa tufanye kila tunaloweza kuhakikisha mamivu ya mapungufu ya umeme tunayapunguza.

“Tunafahamu kuwa ukuaji wa uchumi ni mkubwa kwa watu wetu lakini vyanzo vyetu vya umeme bado ni vilevile, lazima tuongeze vyanzo vingine ili kuwa na umeme wa uhakika kwa ajili ya shughuli za kiuchumi.

“Kuna ripoti imetoka ikionesha Tanzania ni moja ya Nchi ambazo zinakua vizuri kiuchumi Afrika maana yake mahitaji ya umeme yataendelea kuwepo.

“Niwatoe wasiwasi Watanzania kuwa Rais na wasaidizi wake tunafanya kila tunaloweza upatikanaji wa umeme unakuwepo na hiki ni kipindi cha mpito wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linakamilika.”
Tumechoka na ngonjera, tangu enzi za mzee Mwinyi, ccm inaimba wimbo hu huu kwamba tatizo la umeme ni la mpito. Huu mpito mpaka lini? Naamini mgao wa umeme hautapewa kipaumbele kwa vile macho yote ya ccm ni kushinda uchaguzi ujao kwa gharama zozote zile, hata kama nchi inabaki gizani.
 
Huyu naye kiazi tu, suala la umeme wa uhakika utalishughulikia kwa siku moja? Apeleke siasa zake za maji taka kwenye mambo ya msingi utusini
 
Back
Top Bottom