kabila01
JF-Expert Member
- Apr 21, 2009
- 4,236
- 4,989
Hela kaficha mwenyewe,kasahau alipoficha,halafu anatulalamikia sisi,baadae,akija kujiangalia mfukoni,lahaula,anayo,atasemaaa alaaaaaa,yaani nimehangaika muda woote kumbe ni Mimi nilipunguza mzunguko wa pesa na nikawa nashangilia watu wanaposema hela imeadimika!!
Unasema unatunyoosha,sasa umeanza kunyooka na wewe pia,makusanyo puuuuu!! Chini, yameshuka,hao watumishi wa TRA wayatolee wapi kama biashara zetu mtaani zimedoda na hicho ndicho mkisikia zimedoda mnagonga chiaz huko kwenye viyoyozi!
Kadri siku zinavyokwenda yanazidi kushuka si wanataka watu waishi kama mashetani. Mashirika yakipunguza wafanyakazi wao wanakenua meno wanafurahia wanajua tunanyooka, makampuni yakifunga kampuni zao na wafanyabiashara wakifunga biashara zao wanafurahia wanajua wanatunyoosha. Wanasahau kua mapato yanapungua maana hata PAYE zinapungua pamoja na kodi mbalimbali
