Nadhani umepitiwa kidogo. Wakati wa Mwinyi inflation ilishawahi kufikia 28%.
Unakumbuka akina Bozi boziana na Inde moni watu waliingia kwa 50-100K na zilikuwa nje nje.
Wakati wa Mkapa inflation ilirudi single digit kama ilivyo sasa. Mshauri wa mambo ya fedha na uchumi wakati wa Mkapa alikuwa Ndulu.
Reform zote na ecomic recovery programs zote zilikuwa za Ndulu.
Kama qualification na experience hazina maana, ipo siku tutamsikia Mbunge Lusinde ni waziri wa fedha.
Kwavile kuna probation period and apprentice tutakaa kimya miezi 3 ikiisha ndipo tuseme.
Wenzetu hawasubiri hata kuapishwa, akitajwa tu sifa zinawekwa mezani, hazitoshi jina halirudi.
Kuhusu unyeti wa wizara, nasema kuwa MoF ni wizara kubwa popote katika uso wa dunia hii.
Kuna wizara zisizo na umuhimu.
Sifa za elimu za mama Mpendwa ambazo zilifichwa kwanza, ukosefu wa exposure, na uzoefu hakuna ni tatizo linalomkabili mama.
Hakuna ushahidi kuwa sifa zake za elimu zimewahi kupimwa kwa kiwango chochote au zimewahi kutoa matokeo hata mabovu. Hazipo! utapataje something from nothing.
Tunakuomba NasDaz utuonyeshe huyu mama ana nini mkono!
CV ya kuteuliwa kila sehemu kukiwa hakuna historia ya aina yoyote inatutia matomaso buhuti na kihereko. Inaacha nafsi zetu zikitwita kwa simanzi na kutuacha tukiwa tumetundiwaa kwa mfadhaiko.
Mtu akikuuliza Saada Mkuya ni nani uta summarize nini.
Nguruvi3,
Hilo la wakati wa Mwinyi inflation kufikia 28% ndicho nilichomaanisha labda kama sentensi yangu ina some ambiguity...nimesema since Mwinyi Era, hii nchi haijapata kushuhudia high inflation kama kipindi cha Ndulu...anyway, hii lugha imekuja na meli, wengine tumeisomea shule za uswahilini kwahiyo nilichomaanisha ni kwamba, tukiacha kipindi cha Mwinyi, high inflation ikaja kujitokeza tena sasa!
Tukirudi kwamba wakati wa Mkapa Ndulu ndie alikuwa mshauri wake kwa masuala ya fedha; I don't get it coz' for what I know masuala ya inflation yanakuwa regulated na BOT na wakati wa Mkapa, BOT Governor alikuwa Balal ambae alikuwa madarakani from 1998 to 2008, and before 1998 alikuwa Idris Radhid. Ndulu amekuwa Governor from 2008 baada ya Balali kutimuliwa na kabla ya hapo alikuwa Deputy Governor Economic and Financial Policies kwa mwaka mmoja, from 2007-2008 nafasi ambayo alimwachia Enos Bukuku. Sasa je, kwenye mjadala huu tuandike historia kwa sifa za Gavana kumpa Deputy Governor? Nina hofu kwamba hata hiyo historia ya Ndulu uliyoitoa ni kama umeichanganya na ya Balal, if possible try to check it! Beno alisimamia uanzishwaji wa consortium ya uchumi Afrika wakati akiwa wapi? It can make sense for Daudi Balali ambae before then alikuwa IMF.
Kwamba MoF ni nyeti na kubwa hakuna anayekataa! Hata hivyo MoF sio mtu mmoja; is just a team! The back team ndiyo yenye contribution kubwa kuliko hii tunayoijadili ingawaje sisemi kwamba hata jiwe linaweza kuwekwa! Mtendaji Mkuu wa MoF ni Katibu Mkuu wa Wizara; huyu nae ana timu ya watu wenye sifa zilizobobea! Na mbaya zaidi, kutokana na mfumo mbovu tulionao, huyu PS ndie mwenye nguvu zaidi kuliko Minister...hata hivyo nadhani kuna busara waliangalia katika hili! Labda waliogopa hawa ma-minister wasije wakaleta siasa zao kwenye masuala ya kitaalamu! Kwahiyo ingawaje MoF ni nyeti na mzito for any definition lakini this's not all about minister but the team building it! Na kwa sifa za Saada Mkuya, am certain can lead the team effectively!
Kwamba sifa za elimu za mama zilifichwa sidhani kama ni kauli sahihi! Ukiichunguzi kwa makini CV kwenye tovuti ya Bunge utagundua tatizo ni la watu ambao waliiandaa ku-fit bunge website na kisha kui-upload! Nasema hivyo coz' hata date of birth kwenye CV haijaoneshwa! Je, unataka kuniambia nalo lilifichwa?
Hapa narudia tena, argument zenu za CV mzito mzito zime-prove wrong kwahiyo haiwezi kuwa base of discussion! Hapa tena, ili kuonesha ni namna gani CV mzito mzito zinavyoweza ku-deliver ukaleta mfano wa Beno Ndulu, ambae nae ame-prove wrong baada ya kipindi chake inflation kuwa juu!
Ooops! Nimewakumbuka hawa nao! Kuna huyu bwana, alikuwa anaitwa Kighoma Ally Malima...huyu bwana nasikia alikuwa Profesa...akapewa MoF, alichofanya ni kuchota pesa na kuanzisha chama cha siasa!!! Kuna huyu mwingine, yeye anaitwa Profesa Msolla! Huyu bwana alipata ubunge akitokea SUA alikokuwa Deputy Vice Chancellor, namfahamu huyu bwana coz' nami nilibukua pale! JK kwa kuona huyu bwana ni profesa tena ni alikuwa DVC, akaona ampe Teknolojia na Elimu ya Juu; Profesa wangu akashindwa ku-deliver! JK akaona haiwezekani; Professor!! Akaiangalia tena CV ya Professor Msolla, akaona alaa; kumbe jamaa sio mwana-teknolojia bali ni Daktari wa Mifugo aliyebobea!! Kwa kuamini kwamba ametoka SUA...chuo cha mambo ya kilimo kilimo na mifugo, yeye mwenyewe ni mtaalamu kwenye nyanja za huko huko! Akaamua kumpa Wizara ya Mifugo....akashindwa ku-deliver! All this proves the same thing; hizo complex CVs have nothing to do with performance at ministerial level...they need something else to be embedded with!! Narudia tena, complex CV is necessary but not sufficient condition...unataka nikutajie tena sifa za huyu Mama Mpendwa Saada Binti Salum Mkuya!!! Nimekutajia lakini huzitaki...nimeamua sasa kukutajia by contrast! Ninapokutajia ma-complex CVs ya kina Professor Msollla et.al ni kukutajia CV ya Saada by contrast.
Kwamba nitamuelezea Saada ni nani, nitakuambia yeye ni miongoni mwa wanawake wachache sana hapa Tanzania ambae tabia na utamaduni wa watu wake wa ZNZ hazikumzuia kuisaka elimu popote ilipopatikana. Kutokana na kiu yake hiyo ya elimu, alifanikiwa kupata shahada ya uzamili kwenye masuala ya fedha. Saada ni miongoni mwa watu wachache kabisa ambao wamepata kuitumia elimu yao kwenye eneo husika kwani, kwa takribani miaka 8 amefanya kazi Hazina ZNZ akianza kama Afisa na baada kutokana na utendaji wake mzuri akawa Afisa Utawala. Bila shaka kutokana na utendaji wake, baadae alichukuliwa na ofisi ya rais alikoenda kuhudumu kama Kamishina wa Fedha. Baada kudumu hapo kwa takribani mwaka mmoja, akateuliwa ubunge na hapo hapo una ibu waziiri na miezi kumi nane baadae akateuliwa kuwa waziri wa fedha! Huyu ni mama ambae hajafikisha hata miaka 45 pamoja na mafanikio yote hayo! Lakini kwa kuangalia alivyopambana kuipata elimu basi bila shaka hata mafanikio haya ya sasa hayakuja by chance or by means of good luck coz' huyu mama ni mpambanaji. Kwa maelezo zaidi juu ya mafanikio yake kikazi, ningekushauri nenda Hazina ZNZ. Oh! Nilisahau, pamoja na yote hayo si kwamba Mama huyu amechoka kutafuta elimu, la hasha...hivi sasa anafanya PhD yake hapo Open University!
Are you satisfied?